slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Thursday, June 16, 2016

MKURUGENZI WA IDARA YA UTAWALA NA RASILIMALI WATU (DARHM) WIZARA YA MALIASILI, SAID A.S MSAMBACHI ASTAAFU RASMI UTUMISHI WA UMMA, AACHA WOSIA KWA WATUMISHI WA WIZARA HIYO

Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi akizungumza na watumishi wa Idara ya Utawala (hawako pichani) katika ukumbi wa Ngorongoro alipowaaga rasmi jana tarehe 16 Juni, 2016 kwa kukamilisha safari yake ya utumishi wa umma. Amewaasa watumishi wote wa wizara kuimarisha ushirikiano kazini, kufanya kazi kwa bidii, kuwa wabunifu,  kupendana, kusalimiana,  kudumisha uaminifu, utii wa amri halali za viongozi, uadilifu, usawa, usiri wa taarifa za serikali, kuwahi kazini na kujiendeleza kielimu. Amewaasa pia kujiepusha na vitendo vya rushwa, majungu, uchochezi, chuki, ubaguzi na upendeleo wa aina yeyote.
Mkurugenzi Msaidizi Usimamizi wa Rasilimaliwatu, Bi. Aurelia Matagi akizungumza na watumishi wa Idara hiyo wakati akimkaribisha Bw. Msambachi kuzungumza nao.
 Kikao kikiendelea katika ukumbi wa Ngorongoro.
Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment