slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Thursday, November 26, 2015

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAFANYA MKUTANO NA WADAU WA SEKTA YA MALIASILI NCHINI KUJADILI MAENDELEO YA SEKTA HIYO

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru akitoa hotuba ya ufunguzi wa Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Maliasili nchini leo tarehe 26 Novemba 2015 katika Ukumbi wa Chuo cha Utalii Kampasi ya Bustani Jijini Dar es Salaam. Mkutano huo umeshirikisha wadau mbalimbali wakiwemo wa Wizara zenye muelekeo wa Maliasili, Sekta binafsi, NGOs, Waandishi wa habari na wadau wengine. Mada mbalimbali kutoka katika Sekta ndogo za Wanyamapori, Misitu, Utalii, Mambo ya Kale na Uvuvi zimewasilishwa. 
Baadhi ya Washiriki wa mkutano huo wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru wa pili kulia akiwa kwenye picha ya pamoja na balozi wa Ujerumani hapa nchini Mhe. Egon Kochanke wa pili kushoto muda mfupi baada ya kufungua Mkutano huo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mkambusho ya Taifa Prof. Audax Mabula.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru akihojiwa na Mwandishi wa Habari wa Azam TV, Jamal Hashim muda mfupi baada ya ufunguzi wa Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Maliasili nchini uliofanyika leo tarehe 26 Novemba 2015 katika Ukumbi wa Chuo cha Maliasili Jijiji Dar es Salaam. Mkutano huo umejadili mambo mbalimbali ikiwemo mafanikio, changamoto na fursa zinazopatikana katika sekta hiyo muhimu inayochangia kwa kiasi kikubwa katika pato la taifa. Miongoni mwa changamoto kubwa alizozieleza Katibu Mkuu huyo ni Ujangili na Uharibifu wa misitu jambo ambalo amesema Serikali na Wizara imejiapanga kupambana nalo na kuwaomba wadau kushirikiana na Serikali katika vita hiyo.   
 Baadhi ya wadau walioshiriki Mkutano huo.
Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Sera Bi. Mary Faini kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii akiwasilisha mada kuhusu Mafanikio, Changamoto na Fursa zinazopatikana katika Sekta ya Maliasili nchini Tanzania. 
Picha ya pamoja.

Tuesday, November 24, 2015

TANZANIA YACHAGULIWA NA UNESCO KUWA MJUMBE WA KAMATI YA URITHI WA DUNIA

 
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru akizungumza na Waandishi wa Habari (hawako pichani) leo tarehe 23/11/2015 katika Ofisi za Wizara hiyo ambapo amesema kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imechaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Urithi wa Dunia kwa kipindi cha miaka minne. Uchaguzi huo umefuatia uamuzi wa Mkutano Mkuu wa 20 wa nchi Wanachama wa Mkataba wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) unaohusu Urithi wa Dunia uliofanyika mjini Paris, Ufaransa tarehe 18-20 Novemba 2015. (Habari Kamili SOMA TAARIFA KWA UMMA HAPO CHINI)
 
 Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru kushoto akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Tanzania kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Urithi wa Dunia. Alieleza kuwa katika Kamati hiyo Tanzania itawakilishwa na Bw. Donatius Makamba ambaye ni Mkurugugenzi Idara ya Mambo ya Kale Wizara ya Maliasili na Utalii akisaidiwa na Dkt. James Wakibara, Mwikolojia Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Taifa (TANAPA) na Dkt. Mohammed Juma, Mkurugenzi wa Mipango Miji na Vijiji kutoka Zanzibar.
 Bi. Eliwasa Maro Mkurugenzi Msaidizi Utafiti Mafunzo na Takwimu Wizara ya Maliasili na Utalii akitoa ufafanuzi wa baadhi ya mambo katika Mkutano huo na Waandishi wa Habari.
 Sehemu ya washiriki wa Mkutano huo kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii wakinukuu baadhi ya mambo muhimu.

KOBE 201 WALIOKUWA WAKISAFIRSHWA NJE YA NCHI WAKAMATWA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA J.K NYERERE

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru akikagua mabegi matano yenye Kobe 201 yaliyokamatwa usiku wa kuamkia leo na askari wanyamapori kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika uwanja wa Kimataifa wa J.K. Nyerere jijini Dar es Salaam.  

Watuhumiwa hao wa usafirishaji wa wanyamapori wametajwa kuwa ni David Mungi mkazi wa Muheza Mkoani Tanga na Mohammed Suleiman (43) mkazi wa Zanzibar ambao katika tukio hilo walishafanikiwa kupita kwenye mitambo ya ukaguzi lakini mbwa maalum (sniffer dogs) wakasaidia kugundua uhalifu huo. Kwa pamoja watuhumiwa hao walikamatwa na tiketi za kusafiria kuelekea nchini Malaysia. 
Kobe wapatao 201 waliokamatwa na askari wanyamapori kwa ushirikiano na vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutumia mbwa maalum (sniffer dogs).   
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Maliasili na Utalii Bi. Dorina Makaya kulia na Mmoja wa Askari wanyamapori wakiangalia kobe 103 waliotelekezwa eneo la Tabata hivi karibuni baada wahalifu waliohusika kuhofia kukamatwa na vyombo vya dola.