slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Monday, February 8, 2016

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII PROF. JUMANNE MAGHEMBE AONANA NA BALOZI WA UJERUMANI NCHINI MHE. EGON KONCHANKE

Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe (wa pili kulia) akizungumza na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Egon Konchanke (kushoto) alipomtembelea ofisini kwake Mpingo House jijini Dare s Salaam tarehe 08 Februari 2016. Kulia ni Bi.Lena Thiede kutoka Ubalozi wa Ujerumani nchini ambaye ni MKuu wa Kitengo cha Shirikisho la Kikanda Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka kundi la Wshirika wa Maendeleo sekta ya Mazingira, Maliasili na Mabadiliko ya Tabia ya nchi. Lengo la ziara hiyo ilikuwa ni kufahamiana na kuendeleza mashirikiano baina ya Ujerumani na Tanzania katika kulinda na kuhifadhi maliasili zilizopo nchini. Wa pili kulia ni Katibu wa Waziri Bw. Imani Nkuwi. 
 Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mhe. Egon Konchanke (wa pili kulia) akizungumza Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe (wa kwanza kulia ) walipoonana ofisini kwake Mpingo House jijini Dare s Salaam  tarehe 08 Februari 2016. Wengine kushoto ni Bi.Lena Thiede kutoka Ubalozi wa Ujerumani nchini,  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Generali Gaudence Milanzi.

No comments:

Post a Comment