slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Thursday, June 13, 2019

SERIKALI YAAHIDI KUUPIGA JEKI MCHEZO WA WAVU MKOANI MWANZA



Serikali imeahidi kuendelea kutatua changamoto mbalimbali zinazoukabili mchezo wa wavu ambao ni miongoni mwa  michezo iliyosahaulika licha ya kuwa ni mchezo wenye kuvutia watu wengi na unaweza kutumika kama sehemu ya watu kujiajiri

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu wakati alipokuwa akifungua mashindano ya wavu ya Afrika Mashariki katika viwanja vya Milongo   yajulikakanayo kwa jina la Jembe Mirjan East Africa Volleyball Championship yanayofanyika jijini Mwanza.


Mashindano hayo yana shirikisha timu sita  na yatafanyika ndani ya muda nne ambapo mashindano hayo yameanza kati ya timu ya MTC Nyegezi dhidi ya Polisi Zanzibar ambapo mchezo  umemalizika huku Zanzibar Polisi wakiongoza kwa goli 39 kwa 30

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mashindano hayo, Mhe.Kanyasu amewataka wachezaji wawe wavumilivu kutokana na changamoto wanazozipitia kwa vile mchezo wa wavu mbali na mchezo wa mpira wa miguu ni mchezo ambao umekuwa ukikosa Wadhamini kwa sababu haujaweza kufahamika kiasi cha kuwashawishi Wadhamini kuweza kuweka pesa zao.

Amewaeleza wachezaji hao kuwa  lazima wakubali kuumia  kwanza kwa hiki kipindi cha mwanzo ili baadaye wadhamini waweze kujitokeza.


Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu amewahakikishia waandalizi wa mchezo huo kuwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro itadhamini mchezo huo kama ilivyokuwa imeahidi mwanzo

Naye,  Meneja wa Jembe FM, Fredy Kikoti amesema mchezo huo umekuwa ukikabiliwa na changamoto nyingi ikiwa pamoja na kukosekana kwa wadhamini hali iliyopelekea baadhi ya timu kushindwa kushiriki katika mashindano hayo.

Amesema mashindano hayo tangu yalipoanzishwa mwaka jana yamekuwa chanzo cha  kuibua vipaji kwa vijana wa Kanda ya ziwa pamoja na Tanzania kwa
 Ujumla

Mashindano hayo ya Afrika Mashariki yameanza Juni 12 mwaka huu yanatarajia kumalizika Juni 16 mwaka huu katika viwanja vya Milongo



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akisalimiana na kocha wa timu ya Polisi ya Zanzibar, Zuberi Ahmad mara baada ya kuzindua mashindano ya Kikapu ya Afrika Mashariki yanayofanyika jijini Mwanza kabla ya mchuano kuanza kati ya timu hiyo ya Polisi na MTC ya Mwanza


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu (wa pili kushoto)  akisitiza jambo wakati akiangalia mpira wa kikapu kati ya timu ya Polisi Zanzibar na MTC ya Mwanza ambapo timu ya Polisi Zanzibar waliibuka washindi. Wa kwanza kushoto ni Meneja Masoko wa Jembe Fm, Domina Erasto na kulia ni Meneja wa Jembe FM , Fredy Kikoti.




Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiwa kwenye picha ya pamoja na wachezaji wa mpira wa wavu ya MTC Mwanza  kabla ya kufungua mashindano ya wavu ya Afrika mashariki yanayofanyika jijini Mwanza





Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiwa kwenye picha ya pamoja na wachezaji wa mpira wa wavu ya Polisi Zanzibar kabla ya kufungua mashindano ya wavu ya Afrika mashariki yanayofanyika jijini Mwanza




Baadhi ya wananchi waliojitokeza  kushuhudia mtanange kati ya timu ya  Polisi ya Zanzibar na MTC ya Mwanza mara baada ya mashindano hayo ya wavu ya Afrika Mashariki kufunguliwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu katika viwanha vya Milongo jijini Dar es Salaam.





Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akisalimiana na baadhi ya wachezaji wa timu ya MTC ya Mwanza wakati wa kufungua Mashindano ya wavu ya Afrika Mashariki  kabla ya mechi kuanza kati ya timu ya MTC ya Mwanza  na Polisi Zanzibar.







Baadhi ya wananchi na wapenzi wa mpira wa wavu wakiwa wameshika bango wakiwa wanaelekea kwenye viwanja vya Milongo kwa ajili ya ufunguzi wa Mashindano ya wavu ya Afrika Mashariki yanayofanyika jijini Mwanza.


Tuesday, May 7, 2019

NAIBU WAZIRI MHE. KANYASU ASISITIZA WANANCHI WAFUATE SHERIA ZA UHIFADHI



Naibu  Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amewataka wananchi wafuate sheria  kwa kujiepusha kuendesha shughuli za kibinadamu ndani ya Hifadhi ili kujenga mahusiano mazuri baina yao na Wahifadhi.


Pia, amewataka  wananchi kuwachukulia Wahifadhi hao   kama rafiki wa umma na watendaji waliotumwa na Serikali kulinda Maliasili  kwa niaba yao.

Akizungumza na  Watumishi  wa Pori la Akiba la Swagaswaga katika wilaya ya Chemba  jijini Dodoma,  Mhe. Kanyasu amesema Wahifadhi wamepewa jukumu la   kulinda hifadhi za Taifa na wamekuwa  wakifanya kazi nzuri ya kuifanya Tanzania iendelee kuwa na maeneo mazuri yaliyohifadhiwa.



''Sisi ni wa moja hakuna haja ya kujengeana uhasama kati  yetu,  Wananchi wafuate sheria za Uhifadhi  na Wahifadhi fuateni sheria wakati mnapokabaliana na Wananchi'' amesisitiza Kanyasu.



Amesema Wahifadhi wa Wanyamapori na Misitu wanazilinda rasilimali hizo kwa ajili wote, vitu kama mvua, hali ya hewa safi pamoja na mvua ni moja ya faida za moja kwa moja zinazopatikana kutokana na maeneo yaliyohifadhiwa vizuri.



Amesema Wahifadhi hao wameajiriwa kwa mujibu wa sheria hivyo hutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maadili ya kazi zao na pale wanapokiuka sheria mamlaka zinazohusika huwachukulia hatua.

“Sisi kama Wizara tunaamini kwamba wahifadhi wetu wanafanya kazi nzuri, pale ambapo wamekuwa wakilaumiwa kwa kuwapiga na kuwanyanyasa watu kwa namna yoyote ile tumetuma Tume maalum kuchunguza na kuchukua hatua” Amesema

Mhe, Kanyasu amesema uchunguzi unapofanyika na ikathibitika kuwa tukio lililofanyika halikuongozwa na matumizi ya sheria na kuwepo kwa haki wizara imekua ikichukua hatua.

Ameeeleza kuwa Wahifadhi ni watu muhimu saba kwa vile bila wao hakuna uhifadhi unaoweza kuendelea nchini akibainisha kuwa baadhi ya watu wamekuwa wakipinga juhudi za uhifadhi kwa kuwatetea watu wanaovunja sheria.

Kuna watu wanatamani kuona  misitu na wanyamapori wote tunawamaliza ili wapate maeneo ya malisho na kilimo, Nawambieni tukithubutu kufanya hivyo huu ndo utakuwa mwisho wetu wa maisha" Amesisitiza Mhe.Kanyasu



Amesema yapo madhara makubwa yanayoweza kutokea kama hakutakuwa na uhifadhi imara ikiwemo maeneo mengi ya nchi kugeuka kuwa jangwa kutokana na uharibifu wa misitu, ukosefu wa mvua, ukosefu wa maji, chakula na ukosefu wa hewa safi.

Kwa upande wake, Meneja wa Pori la Akiba la Swagaswaga, Alex Choya  amesema kuwa kumekuwa na tuhuma za vitendo vya ukatili dhidi ya raia vinavyofanywa na baadhi ya askari wa hifadhi za Taifa na kutoa wito kwa wananchi wote wenye ushahidi na taarifa juu ya vitendo hivyo kuziwasilisha ili hatua stahiki zichukuliwe.

Amesisitiza kuwa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) hairuhusu askari kufanya vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya raia badala yake imekua ikiwahamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika ulinzi wa rasilimali zinazowazunguka.





  Naibu Waziri wa Maliasili  na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akizungumza na watumishi wa Pori la Akiba la Swagaswaga mara baada ya kutembelea michoro ya mapangoni iliyochorwa zaidi ya miaka 1000 na kabila la Wasandawe  katika wilaya ya Chemba mkoani Dodoma


   Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu ( wa pili kulia) akioneshwa michoro ya mapangoni na Askari Wanyamapori iliyochorwa zaidi ya miaka 1000 iliyopita na kabila la Wasandawe ambayo ni miongoni mwa vivutio vya Utalii wakati alipotembelea  mara baada ya kuzungumza na watumishi wa Pori la Akiba la Swagswaga katika ziara yake ya  kikazi wilayani Chemba jijini Dodoma. Wa kwanza kulia ni Naibu Kamishna wa Uhifadhi wa TAWA, Mabula Misungwi.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu (wa tatu ) akiangalia baadhi michoro ya mapangoni iliyochorwa zaidi ya miaka 1000 iliyopita na kabila la Wasandawe ambayo ni miongoni mwa vivutio vya Utalii katika ziara yake ya kikazi wilayani Chemba jijini Dodoma. Wa kwanza kulia ni Meneja wa Pori hilo,  Alex Choya.
  
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu (wa tatu) akiwa na baadhi ya watumishi wa Pori la Akiba la SwagaSwaga wakitoka kuangalia michoro ya miambani ambayo imechorwa zaidi ya miaka 1000 iliyopita
 Baadhi ya watumishi wa Pori la Akiba la SwagaSwaga wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhe, Constantine Kanyasu  wakati alipokuwa akizungumza nao.
 Meneja wa Pori la SwagaSwaga , Alex Choya akitoa taarifa kwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhe, Constantine Kanyasu, Kushoto ni Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA)



Monday, April 22, 2019

WAZIRI KANYASU AAGIZA MINADA YA MIFUGO ILIYOKAMATWA IFANYIKE NJE YA HIFADHI




Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu ameagiza minada yote ya mifugo iliyokamatwa Hifadhini baada ya Serikali kushinda kesi mahamakani ifanyike nje ya Hifadhi ili kuondoa dhana mbaya iliyojengeka miongoni mwa jamii kuwa  Wahifadhi hukamata mifugo hiyo ili waweze kujiuzia wenyewe.


Pia, Ameagiza minada hiyo itangazwe katika vijiji kabla ya tarehe ya kufanyika kwa lengo la kuwajulisha Wananchi hata kwa wale walioshindwa kesi hizo ili waweze  kushiriki katika minada hiyo huku Mkuu wa Wilaya husika ashirikishwe ipasavyo kwenye minada hiyo.

Akizungumza na viongozi wa vijiji 15 katika kijiji cha Kisondoko ambavyo ni miongoni mwa vijiji vilivyokutwa ndani ya Pori la Akiba la Mkungunero lililopo katika wilaya ya Kondoa  Mkoani Dodoma, Mhe.Kanyasu amesema minada hiyo isifanyike kwa usiri badala yake iwe wazi nje ya Hifadhi ili kutoa fursa kwa yeyote kushiriki.

Akizungumzia kuhusu  ugumu wa kupata vibali vya kuingilia hifadhini wakati minada ilipokuwa ikifanyikia ndani,  Mhe.Kanyasu amesema kabla ya agizo hilo wananchi waliokuwa wakishiriki katika minada hiyo  walihitajika wawe na vibali vya kuingilia hifadhini  la sivyo walikuwa  wakikatwa kwa kosa la kuingia hifadhini bila kibali.

Amebainisha kuwa endapo minada hiyo itafanyika kwa uwazi na nje ya Hifadhi kutasaidia kuepusha shutuma nyingi zikiwemo za rushwa zinazowakabili  Wahifadhi kuwa wamekuwa wakishiriki kuwatafuta wanunuzi wa Ng'ombe kutoka mikoa ya mbali kwa makubaliano ya kulipwa mara baada ya mnada.


Amesema kitendo cha minada hiyo kuanza kufanyika nje ya Hifadhi  kutasaidia kuondoa malalamiko kutoka kwa wananchi ambao wamekuwa wakidai kuwa pindi mifugo yao inapotaifishwa wamekuwa hata hawajulishwi lakini wafanyabiashara wakubwa ndo wamekuwa na taarifa.


Amesema wananchi ambao mifugo yao imekuwa ikikamatwa na baadaye kutaifishwa wamekuwa na chuki na Wahifadhi huku wakiwatuhumu kuwa wamekuwa wakishirikiana na wafanyabiashara hao  kwa kuwajulisha ili wafike Hifadhini kwa ajili ya kuinunua.

Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu amewaonya askari wanyamapori wenye tabia ya kuvizia ng'ombe wakiwa mpakani kati ya  kijiji na Hifadhi na kisha kuwasukumia ng'ombe hao ndani ya Hifadhi ili wazikamate kuwa vitendo hivyo havikubaliki na sio kazi waliyotumwa na Serikali.

Akizungumza mbele ya Naibu Waziri huyo, Mwenyekiti wa kijiji cha Ikengwe, Ismail Hamis amesema licha ya huo utaratibu mpya wa kufanyia minada nje ya Hifadhi, anaiomba serikali iangalie upya sheria ya kutaifisha mifugo kwani imepelekea wafugaji wengi kuwa maskini.

Ameshauri kuwa mifugo ikikamatwa ndani ya Hifadhi, waruhusiwe kulipa fidia kwa sababu mifugo hiyo ndo imekuwa tegemeo lao kwa kuwasaidia kusomeshea watoto wao.


Kwa upande wake, Naibu Kamishina wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania,( TAWA)Mabula Misungwi amemuahidi Naibu Waziri hiyo kuwa agizo lake litatekelezwa ipasavyo ili wananchi wa maeneo ya mifugo ilikokamatwa waweze kujulishwa.

Aidha, Misungwi amewataka watumishi hao kujiepusha na vitendo vya rushwa pindi wanapokamata mifugo kutoka kwa wafugaji kuwa yeyote atakayebainika atawajibishwa kikamilifu ili iwe funzo kwa wengine.

Saturday, April 20, 2019

NAIBU WAZIRI KANYASU ATOA ONYO KWA WAHIFADHI NCHINI KUHUSU WANANCHI




Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amezionya na kuzitaka Taasisi za Uhifadhi kuacha tabia ya kuwabughudhi wananchi wanaoishi katika vijiji na vitongoji 366 vilivyokutwa ndani ya Hifadhi katika maeneo mbalimbali nchini mpaka hapo maamuzi ya Kamati ya Mawaziri saba iliyoundwa kushughulikia suala hilo itakapokamilisha kazi iliyopewa na kuwasilisha ripoti  kwa Mhe. Rais.


Hatua hiyo ni kufuatia  malalamiko kutoka  kwa baadhi ya  wananchi wakiwemo wakulima na wafugaji  wanaoishi katika vijiji na vitongoji hivyo kudai kuwa wamekuwa wakisumbuliwa  na mifugo yao kukamatwa mara mara kwa madai ya kukutwa imeingia ndani ya Hifadhi.

 Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kisondoko ambacho ni miongoni mwa vijiji vilivyomo ndani ya Pori la Akiba la Mkungunero katika wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma, Mhe. Kanyasu amezitaka taasisi hizo kufuata na kuzingatia  maelekezo yaliyotolewa na Serikali kuhusu wananchi wanaoishi katika maeneo hayo.

 Aidha, Mhe. Kanyasu ametumia fursa hiyo kuwaonya wananchi  ambao wamekuwa wakivamia maeneo mapya ya Hifadhi  kwa kisingizio cha kauli aliyoitoa Mhe. Rais kuacha mara moja na kwamba yeyote  atakayekamatwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.


" Wananchi ninao walenga ni wale tu ambao walikuwa wakiishi Hifadhini  kabla ya kauli ya Rais aliyoitoa mwanzoni mwa mwaka huu" Alisisitiza.


 Hata hivyo, Mhe Kanyasu amebainisha kuwa Kamati ya Mawaziri saba iliyoundwa na kuzunguka nchi nchi nzima imebaini kuwa kuna zaidi ya vijiji 820 ambavyo vimo ndani ya Hifadhi mbali ya vile 365 vilivyobainishwa awali na kuwasihi wananchi  wasiendelee kuvamia maeneo mengine.


 Mhe.Kanyasu  ameowanya baadhi ya askari wa wanyamapori  wanaoomba rushwa Kutoka kwa wafugaji pindi wanapokamata  mifugo yao ili waweze kuiachia waache mara moja tabia hiyo akisisitiza kwamba  askari yeyote atakayethibitika atachukuliwa hatua kali za kinidhamu kwa mujibu wa Sheria za utumishi wa Umma.


Mkuu wa wilaya ya Kondoa, Mhe. Sezaria Makota  amewataka wananchi hao kuendelea kuwa walinzi wa maeneo hayo huku wakisubili hatma ya taarifa ya kamati ya Mawaziri saba itakayotolewa hivi karibuni.

" Baada ya taarifa hiyo  mtajua hatma yenu na kama hapa mtabaki au mtahamishwa na kama mtahamishwa tutajua tutawapeleka eneo gani kwa ajili ya malisho na kilimo." Alisema.

Akizungumza kwa niaba ya Wananchi, Mwenyekiti wa kijiji cha Kisondoko, Ismail Said amemueleza Naibu Waziri huyo kuwa baadhi ya askari wa wanyamapori wamekuwa wakikamata mifugo yao na kuomba rushwa na pale makubaliano yanaposhindikana huondoka na mifugo yao.

Amesisitiza kuwa vitendo hivyo vimekuwa vikichochea chuki baina ya wananchi na askari hao jambo linalorudisha nyuma jitihada za Uhifadhi nchini.



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine  Kanyasu wa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kisondoko ambacho ni miongoni mwa vijiji vilivyomo ndani ya Pori la Akiba la Mkungunero katika wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma ambapo ameagiza wananchi hao wasibughuziwe hadi hapo maamuzi yatakapotolewa juu ya hatma yao. Wengine ni kmati ya Ulinzi na Usalama wa wilaya hiyo pamoja na Maafisa wa kutoka  Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania, Kulia ni Mkuu wa wilaya hiyo, Sezaria Makota.



  Mkuu wa wilaya ya Kondoa, Sezaria Makota akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kisondoko kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu katika kijiji  ambacho ni miongoni mwa vijiji vilivyoomo ndani ya Pori la Akiba la Mkungunero katika wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma ambapo ameagiza wananchi hao wasibughuziwe hadi hapo maamuzi yatakapotolewa juu ya hatma yao.  



.Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Kisondoko wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii alipokuwa akizungumza nao kuhusu mifugo yao kukamatwa mara kwa mara na askari wanyamapori wa Pori la Akiba la Mkungunero katika wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma.


 Diwani wa kata ya Kisondoko, Mhe. Ismail Juma akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kisondoko kabla ya kumkaribisha Mkuu wa wilaya  Mhe. Sezaria Makota katika kijiji  ambacho ni miongoni mwa vijiji vilivyoomo ndani ya Pori la Akiba la Mkungunero katika wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma.

Monday, March 25, 2019

SERIKALI KUNYANG'ANYA HOTELI ILIZOZIBINAFSISHA




Serikali imeanza ukaguzi wa hoteli za Kitalii ilizozibinafsisha  kwa Wawekezaji na wale watakaobainika kuziendesha chini ya kiwango, watanyang'anywa na kupewa wawekezaji wengine walio tayari kuziendesha kwa manufaa ya kukuza utalii nchini.

Hatua hiyo inafanyika kufuatia  kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa watalii na wadau mbalimbali wa utalii juu ya  huduma  zisizoridhisha zinazotolewa na hoteli hizo.

Akizungumza mara baada ya kukagua baadhi ya hoteli za Kitalii ikiwemo ya   Soronera na Lobo, zilizo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara, Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe Constantine Kanyasu  amesema lengo la kubinafsishwa kwa Hoteli hizo ilikuwa  ni kuboresha huduma.

Pia,  Hoteli ya Musoma ya mkoani Mara  pamoja na Ngorongoro Wildllife iliyopo ndani ya Mamlaka ya Eneo la Ngorongoro ni  miongoni mwa hoteli   zilizofanyiwa ukaguzi.

Amesema  Mwekezaji asiyefanya hivyo atanyang'anywa umiliki ili apewe mwekezaji   mwingine mwenye uwezo wa kutoa huduma bora.

 Aidha, amesema  kumekuwa na tuhuma kwa baadhi ya hoteli zilizobinafsishwa kukwepa kodi ya tozo ya huduma pamoja kuwalipa wafanyakazi wazawa mishahara midogo huku wale wa kigeni wakilipwa mishahara mikubwa kwa kazi ya aina moja.

Mhe. Kanyasu amesisitiza kuwa, Serikali ilizibinafsisha hoteli hizo ili zilete mapinduzi katika nyanja ya ajira, huduma bora kwa watalii, kodi pamoja kuziboresha ili zikidhi soko la watalii kwa sasa.

Akizungumza mara baada ya kukagua hoteli hizo,Mhe Kanyasu amebainisha  baadhi vitu alivyoviona ikiwemo uchakavu wa miundombinu pamoja na udanganyifu wa idadi ya watalii wanaofikia katika hoteli hizo .

Amesema Wizara  itapeleka idadi ya hoteli zitakazobainika kwenda kinyume  ili Msajiri wa Hazina  aweze kuzifutia  umiliki.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Kanyasu  amewataka viongozi wa Hoteli hizo kukaa na kuona ni namna watakavyoongeza idadi ya Watanzania wanaotembelea hifadhi na kupata mapumziko katika Hoteli hizo.

 Kuhusu Tozo ya huduma ya Mapato amezielekeza Halmashauri mbalimbali ikiwemo ya Serengeti kupata taarifa sahihi kutoka  Hifadhi za Taifa ( TANAPA)

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya  Serengeti,  Victor Tonesha  amesema changamoto inayoikabili Halmashauri hiyo ni ya  kushindwa kubaini kiwango halisi cha fedha zinazotolewa na Wawekezaji hao.




Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,  Constantine Kanyasu (katikati)  akizungumza na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya y Serengeti ikiongozwa na  Mkuu wa wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu  mara baada ya kukagua hoteli ya Soronera  iliyopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti  mkoani Mara kwa lengo la kubaini hoteli zilizobinafsishwa na serikali ambazo zimekuwa hazifanyi vizuri.

  


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,  Constantine Kanyasu (kulia) akiwa pamoja na  Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa ( TANAPA), Martin Looiboki wakiwa wameambatana kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya  Serengeti  wakiwa katika hoteli ya Soronera  iliyopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti  mkoani Mara wakiwa wanaikagua kwa lengo la kubaini hoteli zilizobinafsishwa na serikali ambazo zimekuwa hazifanyi vizuri.



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,  Constantine Kanyasu (kulia) akizungumza na Meneja wa Hoteli ya Soronera,Asram Narwat  katika jiko la hoteli hiyo wakati Naibu Waziri huyo alipokuwa akiikagua hoteli ambayo ni miongoni mwa hoteli ambazo zilibinafsishwa na Serikali kwa Wawekezaji kwa lengo la kuboresha Huduma kwa watalii. Hoteli hiyo ipo ndani ya Hifadhi ya Serengeti mkoani Mara kwa  lengo la kukagua ili  kubaini hoteli zilizobinafsishwa na serikali ambazo zimekuwa hazifanyi vizuri.





Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,  Constantine Kanyasu (kulia) akiwa pamoja na  Mkuu wa  wa wilaya  ya Serengeti, Nurdin Babu wakiongozwa na  Meneja wa Hoteli  ya Soronera, Asram Narwat katika Hoteli ya Soronera  iliyopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti  mkoani Mara, Hoteli hiyo ipo ndani ya Hifadhi ya Serengeti mkoani Mara kwa  lengo la kukagua ili  kubaini hoteli zilizobinafsishwa na serikali ambazo zimekuwa hazifanyi vizuri



Muonekanao wa hoteli ya Soronera kwa upande wa ndani kati vyumba vya hoteli hiyo iliyopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara amabayo ni moja ya Hoteli ilyobinafsishwa na Serikali kwa Wawekezaji.


Friday, March 22, 2019

WAVAMIZI SHAMBA LA MITI BIHARAMULO WAPEWA MIEZI 3



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu ametoa muda wa miezi mitatu kwa wananchi waliovamia na kuanzisha shughuli za kibinadamu ndani ya Shamba la miti la Biharamulo kuondoka mara moja kwa hiari yao bila shuruti kabla ya mwezi Juni mwaka huu.

Ametoa muda huo ili wananchi  waliolima   mazao mbalimbali yakiwemo  mahindi na pamba  waweze kuvuna mazao yao  kabla ya kuanza kwa oparesheni maalum ya kuwaondoa, iliyopangwa kufanyika mwanzoni mwa mwezi Julai mwaka huu itakayofanywa na Wakala wa Huduma ya Misitu Tanzania ( TFS) kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya hiyo.

Mhe.Kanyasu  ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake ya kikazi ya   kutembelea shamba la miti Biharamulo lililopo katika wilaya ya Chato mkoani Geita.

Amesema Oparesheni hiyo haitasubiri taarifa ya Wizara tano inayoendelea kufanyiwa kazi kwa kuwa eneo hilo halihusiani na vile vijiji 366  vilivyokutwa ndani ya Hifadhi.

Amesema  haiwezekani wananchi waliovamia eneo hilo waendelee kuachwa kwa kisingizio cha Kauli ya Rais aliyoitoa Januari 15 mwaka huu kuhusiana na vijiji 366 vilivyokutwa ndani ya maeneo ya Hifadhi.

Amebainisha kuwa wananchi waliovamia eneo hilo wameitafsiri visivyo Kauli hiyo na kuongeza kuwa baada tu ya tamko la Mhe. Rais , baadhi ya wananchi hata wale waliokuwa wakiishi  katika maeneo mengine nje ya hifadhi waliendelea  kuvamia na kuanza kujimilikishia  maeneo makubwa  wakidai kuhalalishwa na tamko la Rais.

Amefafanua kuwa taarifa inayoendelea kufanyiwa kazi  na timu ya Mawaziri na Makatibu Wakuu kutoka Wizara tano imebainisha kuwa mpaka sasa zaidi ya vijiji 700 vimekutwa ndani ya Hifadhi badala 366 vilivyoripotiwa awali.

Kufuatia hali hiyo amesema baadhi ya wavamizi wa Hifadhi katika maeneo mbalimbali wataendelea kuondolewa bila kusubili kukamilika kwa zoezi linaloendelea kwa kuwa walieendelea kuvamia maeneo ya Hifadhi kwa kisingizio cha tamko la Rais huku maeneo hayo yakizidi kuharibiwa kwa miti kukatwa na shughuli nyingi za kibinadamu

Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu ameiagiza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ( TFS) kutenga Bajeti ya kugharamia operesheni ya kuwaondoa  wavamizi ndani ya Shamba hilo.

Ameitaka TFS kuendesha oparesheni za mara kwa mara ili wavamizi hao wajue Serikali ipo kazini kulinda rasilimali za Taifa muda wote.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Chato,  Mtemi Simeoni akizungumza katika ziara hiyo  alisema kuwa  baadhi ya wananchi kutoka nje ya wilaya hiyo wamekua wakivamia na kuanzisha shughuli za kibinadamu ndani ya Shamba hilo, suala ambalo ni kinyume cha sheria.


Mkuu huyo wa wilaya amebainisha kuwa wananchi katika maenro hayo wana mahitaji makubwa ardhi na kuiomba Wizara iangalie  namna ya kuwasaidia  hekari 5000 ili wapate maeneo ya kulima na kuchungia mifugo yao.

Kwa upande wake Meneja wa Shamba hilo Bw. Thadeus Shirima  amemweleza Naibu Waziri huyo kuwa hadi sasa zaidi ya hekari 900 zimepandwa miti licha ya Shamba hilo  kukabiliwa  na changamoto ya uhaba wa watumishi pamoja na vitendea kazi.




 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu (katikati)  akizungumza   na Mkuu wa Wilaya ya Chato, Mhe.  Mtemi Simeoni (kushoto)   wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea Shamba la Miti la Biharamulo mara baada  ya kukagua maendeleo ya miti iliyopandwa katika shamba hilo kwa  ukubwa  wa hekari 900 katika wilaya ya Chato mkoani Geita., Kulia ni Meneja wa shamba hilo, Edward Nyondo.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akimsikiliza  Mkuu wa Wilaya ya Chato,  Mhe. Mtemi Simeoni (kushoto)  alipotembelea Shamba la Miti la Biharamulo mara baada  ya kukagua maendeleo ya miti iliyopandwa katika shamba hilo  kwa  ukubwa hekari 900 katika wilaya ya Chato mkoani Geita. Wengine ni watumishi pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo





 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu  akizungumza na  wananchi pamoja na watumishi wa shamba la miti la Biharamulo ambalo mara baada ya kukamilika kwa kupandwa miti katika eneo lote litakuwa ndio  shamba la pili kwa ukubwa kati ya mashamba  20 yanayomilikiwa na Wakala wa Hudumza Misitu Tanzania lililopo wilayani Chato mkoani Kagera.




 Mkuu wa wilaya ya Chato, Mhe. Mtemi Simeon akipanda mti wakati alipotembelea Shamba la Miti la Biharamulo mara baada  ya kukagua maendeleo ya miti iliyopandwa katika shamba hilo lenye ukubwa wa  hekari 900 katika wilaya ya Chato mkoani Geita
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa wilaya na watumishi wa Shamba la Miti la Biharamulo lililopo katika wilaya ya Chato mkoani Geita.



.Baadhi ya watumishi wa Shamba la Miti la Biharamulo wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii wakati Naibu Waziri huyo alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja katika shamaba hilo hukuakiwasisitizan umuhimu wa kufanya kazi kwa kushirikiana na wananchi wanaoishi karibu na shamba hilo.



















Monday, March 18, 2019

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUJA NA MKAKATI MAALUM WA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu amesema Wizara ya Maliasili na Utalii  inatarajia kuja na mkakati maalum wa kutangaza utalii ndani na nje ya nchi kwa kunadi  maeneo ya vivutio vya utalii badala ya kuinadi nchi kwa ujumla na  vivutio vyake

Pia,Amesema  maeneo hayo yatakuwa yakinadiwa  kwa mfumo wa vifurushi (Packages) hali itakayopelekea mtalii akija nchini ataweza kutembelea maeneo ya  Hifadhi,  Misitu ya Mazingira asilia pamoja na  maeneo ya utalii wa kiutamaduni.

Amesema lengo la kuja na mkakati huo ni kusaidia maeneo hayo kuweza kujulikana pamoja na kumuwezesha mtalii kuweza kuvifahamu vivutio vinavyopatikana katika eneo hilo kwa undani badala ya kuitangaza nchi kwa kujumuisha vivutio vya utalii vilivyopo  kwa ujumla wake.

Amesema mkakati huo utasaidia  kuongeza idadi ya watalii katika maeneo yenye vivutio ya utalii lakini kwa sasa yamekuwa yakipata idadi ndodgo ya watalii kwa vile yamekuwa hayafahamiki ipasavyo.

Amesema mkakati huo utalenga zaidi katika maeneo yenye utalii wa kiutamaduni pamoja na maeneo ya Misitu asilia, Ni utalii mpya ambao kwa Tanzania haufahamiki sana unaojikita kuangaliia viumbe ambao wapo hatarini kutoweka.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri huyo mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakati Kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi pamoja na Msitu Asilia wa Chome katika wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro.

Ameeleza kuwa aina hiyo ya kutangza vivutio vya utalii katika eneo fulani badala ya nchi italeta manufaa makubwa kwa Hifadhi na maeneo yale ambayo kwa sasa yamekuwa yakipokea idadi ndogo ya watalii hasa katika ukanda wa Kusini na Magharibi.

Amesema ukizungumzia utalii kwa sasa unalenga mikoa ya Kaskazini ambako zaidi ya asilimia 80 unafanyika ukanda huko huku kanda nyingine kama vile kanda ya ziwa, Magharibi pamoja na Kusini zikiwa bado idadi ya watalii wanaotembelea ni ndogo ukilinganisha na uwingi wa vivutio vya utalii vilivyopo katika maeneo hayo.

Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Shabani Shekilindi amesema Tanzania imejaliwa kuwa na vivutio vingi vya utalii lakini mapato yatokanayo na utalii hayaakisi ualisia wa vivutio vilivyopo nchini hivyo mikakati mipya ya kutangaza vivutio inahitajika.


 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii, Shabani Shekilindi (wa kwanza kushoto) akiwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu ( wa pili kushoto) wakiwa pamoja na Wajumbe wa kamati hiyo wakipewa maelezo mafupi kuhusu mradi wa kuzalisha faru weusi na mbwa mwitu kutoka kwa Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa (TANAPA) unaofanyika katika Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi wakati Kamati ilipofanya ziara katika Hifadhi hiyo iliyoko mkoani Kilimanjaro.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu akipigiwa saluti na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi wakati alipokuwa ameongozana na Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii ilipotembelea eneo hilo kwa ajili yamradi wa kuzalisha faru weusi na mbwa mwitu
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii kutembelea eneo la maradi wa kuzalisha faru weusi na mwitu katika Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi mkoani Kilimanjaro. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki.



 Baadhi ya Wajumbe wa  kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii walipotembelea ofisi ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania iliyopo katika wilaya ya  Same