slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Saturday, April 22, 2017

VOTE for Mt Kilimanjaro #Tanzania as Africa's Leading Tourist Attraction in World Travel Awards 2017.


DID YOU KNOW? Mount Kilimanjaro is the 2016 Africa's Leading Tourist Attraction.

HOW TO VOTE? Click link below, register&vote

Pigia kura Mt Kilimanjaro katika Tuzo za World Travel Awards 2017 kama Kivutio Bora Afrika.

JE WAJUA? Mlima Kilimanjaro ndio kivutio bora Afrika mwaka 2016.

Jinsi ya kupiga kura: bonyeza link hapa chini, jisajili (register), nenda kwenye majina (Africa nominees) kisha piga kura kwa kubonyeza kiduara pembeni mwa jina.

LINK

Sunday, April 16, 2017

360 YA CLOUDS TV KWENDA MUBASHARA NDANI YA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI KESHO

TANAPA kwa kushirikiana na Clouds TV 360 kesho Jumatatu ya Pasaka watakuwa Mubashara kutoka Hifadhi ya Serengeti kuanzia saa 12 asubui hadi saa 4 asubui.Fuatana nasi katika kuhamasisha Utalii wa Ndani.

Thursday, April 13, 2017

KIPINDI CHA 360 KURUSHWA MUBASHARA KUTOKA KATIKA HIFADHI ZA SERENGETI NA NGORONGORO

Watangazaji wa kipindi cha 360 kinachorushwa na Clouds Tv wamewasili mkoani Arusha jana kwa ajili ya ziara katika hifadhi za taifa za Serengeti na Ngorongoro kwa lengo la kutangaza utalii wa ndani. 

Kipindi hicho kinachoendelea kujizolea umaarufu cha 360 kinataraji kurushwa moja kwa moja kutoka katika hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro na Serengeti kikiongozwa na watangazaji wake Baby Kabaye, Sam Sasali, Hassan Ngoma na James Tupa tupa. 

Leo Ijumaa na Jumamosi kitarushwa LIVE kutokea hifadhi ya Ngorongoro na Jumatatu kutokea hifadhi ya Serengeti.

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAANZA KUKUSANYA MAONI KUTOKA KWA WADAU WA UTALII YA KUBORESHA SERA YA TAIFA YA UTALII YA MWAKA 1999


Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki akizungumza katika mkutano huo.
 Picha ya pamoja.
Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Zahoro Kimwaga akizumza katika mkutano huo.

Na. Lusungu Helela - WMU
......................................................
Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imewataka wadau wa Utalii nchini kutoa maoni yenye tija itakayopelekea upatikanaji wa Sera bora itakayoleta ufanisi katika uendeshaji wa huduma zinazotolewa katika sekta ya Utalii. 

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni miaka 17 sasa tangu Sera ya Taifa ya Utalii iliyopo ifanyiwe mapitio kwa mara ya mwisho mwaka 1999.  

Katika kutambua hilo, Wizara imeanza kupitia upya Sera hiyo ili kuhakikisha kuwa Sekta ya Utalii inakwenda sambamba na mabadiliko mbalimbali yanayotokea duniani yakiwemo ya kiteknolojia, kijamii, kiuchumi, kisiasa na mazingira

Akizungumza katika mkutano  uliofanyika kwa muda wa siku mbili  Jijini Arusha kwa mikoa ya kanda ya Kaskazini, Naibu Katibu Mkuu  wa Wizara hiyo, Dkt. Aloyce Nzuki alisema Sera hiyo inafanyiwa marekebisho kwa kuwa imepitwa na wakati kutokana na mabadiliko makubwa yaliyotokea katika sekta hiyo kwa sasa. 

Aidha, alisema kwa kutambua mchango wa utalii kiuchumi , ni wazi kuwa sera wezeshi ya utalii yenye kutoa mwongozo wa utaratibu bora na sahihi wa usimamizi, uendelezaji na utendaji katika sekta hiyo  unahitajika.

"Tunataka kuibadilisha sera hiyo ili iweze kujibu changamoto za aina ya utalii wa sasa ambao kipindi cha nyuma haukuwepo", ametea mfano utalii mikutano pamoja na utalii wa kiutamaduni ambao umekuwa ukikua kwa kasi hapa nchini.

Kutokana na hali hiyo,  Dkt. Nzuki amesema marekebisho ya Sera hiyo yanahitaji mchango mkubwa kutoka kwa wadau kwa kuwa  inaendeshwa kwa kiasi kikubwa na Sekta Binafsi katika kutoa huduma na kufanya biashara za utalii hapa nchini.

Awali, Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Zahoro Kimwaga alisema uhuishwaji wa Sera hiyo utazingatia namna ambavyo wazawa wataweza kuwa wanufaika namba moja kwa kuwaandalia mazingira rafiki ya kuendesha biashara ya utalii tofauti na sasa ambapo makampuni mengi ya utalii ni ya watu kutoka nje. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TATO, Wilbert Chambulo alisema suala la kuifanyia marekebisho ya sera hiyo ni jambo jema ila sasa serikali iangalie namna ya kuboresha mashirikiano katika utoaji wa maamuzi kwa wafanyabiashara wa utalii nchini badala  ya kuamua peke yake.

Mkutano huo wa kukusanya maoni kutoka kwa wadau umeanza kufanyika mkoani Arusha kwa kuwashirikisha wadau kutoka mikoa minne ya Kanda ya Kaskazini na badaaye utafanyika katika kanda zingine kwa muda wa siku mbili kila kanda kwa ushirikiano kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii,   Shirikisho la Vyama Vya Utalii Tanzania  (TCT) pamoja na Benki ya Dunia chini ya uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu

Wednesday, April 12, 2017

WAZIRI MKUU MSTAAFU WA ISRAEL, EHUD BARAK AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KUTEMBELEA VIVUTIO VYA UTALII, APOKELEWA KIA NA WAZIRI WA MALIASILI, PROF. JUMANNE MAGHEMBE

Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) akisalimiana na familia ya Waziri Mkuu Mstaafu wa Israel, Ehud Barak (kulia) alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) jana kwa ajili ya ziara ya kutembelea vivutio vya utalii nchini. Waziri Mkuu huyo wa 10 wa Israel aliliongoza taifa hilo mwaka 1999 - 2001.
Waziri Mkuu Mstaafu wa Israel, Ehud Barak (wa pili kushoto) akimueleza jambo Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe muda mfupi baada ya kuwasili na ndege ya shirika na ndege la Israel (Israel Air) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro jana kwa ajili ya kutembelea vivutio vya utalii hapa nchini.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) akimuongoza mgeni wake, Waziri Mkuu Mstaafu wa Israel, Ehud Barak (kushoto kwake) kuelekea kwenye maandalizi ya ziara yake ya kitalii nchini baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro jana. (Picha na Wizara ya Maliasili na Utalii)

MAAZIMIO YA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
TAARIFA KWA UMMA

Wizara ya Maliasili na Utalii imesitisha utoaji wa vibali vya kusafirisha mkaa kutoka Wilaya moja hadi nyingine kuanzia terehe 01 Julai mwaka huu.

Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe na kuungwa mkono na Baraza la wafanyakazi la Wizara wa Maliasili na Utalii kwa lengo kupunguza uharibifu mkubwa wa mazingira hususan ukataji wa miti hovyo.

Baraza hilo lililofanyika mjini Dodoma tarehe 10 Aprili, 2017 pia lilijadili umuhimu wa kutumia mkaa mbadala kwa miji mikubwa kama Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya ambapo mpango mahususi wa kutumia mkaa mbadala utakaozalishwa na kiwanda cha Mufindi – Iringa utawasilishwa ifikapo mwezi Julai mwaka huu.

Baraza la Wafanyakazi wa Maliasili na Utalii pia limepitisha kwa kauli moja kuongeza jitihada katika kukabiliana na ujangili hasa katika Pori la Akiba la Selous, Pori Tengefu la Loliondo, Rungwa na Yaeda Chini. Nguvu zaidi ya kukabiliana na changamoto ya uingizaji wa mifugo katika maeneo ya hifadhi ambao unachangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la ujangili pia ilijadiliwa.

Aidha, Baraza liliazimia mali za majangili pamoja na mifugo itakayokamatwa katika maeneo ya hifadhi yataifishwe kwa mujibu wa sheria.

Katika kukabiliana na changamoto ya usafirishaji wa magogo nje ya nchi, Baraza liliazimia kuwa usafirishaji wa magogo ufanyike kwa kutumia nyaraka halisi (Original Documents) badala ya vivuli vya nyaraka (Photocopy).

Baraza hilo la Wafanyakazi pia liliazimia kuwa watumishi wote wa wizara wazingatie sheria na kanuni za utumishi wa umma katika maeneo yao ya kazi pamoja na utoaji wa huduma kwa Umma.

Mkutano huo wa Baraza la Wafanyakazi hufanyika mara mbili kwa mwaka kwa lengo la kupitia utekelezaji wa bajeti ya mwaka uliopita na kutoa maoni yao kwa bajeti ya Wizara inayotarajiwa kuwasilishwa bungeni pamoja na kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili na kuweka mkakati wa kukabiliana nazo. Wajumbe wa Baraza hilo ni wawakilishi wa watumishi kutoka katika Idara, Vitengo, Taasisi na Vituo vya Wizara.

Imetolewa na;

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Wizara ya Maliasili na Utalii,
11 Aprili, 2017
Dodoma. 

Monday, April 10, 2017

NI MARUFUKU KUSAFIRISHA MKAA KUTOKA WILAYA MOJA KWENDA NYINGINE KUANZIA MWEZI JULAI. MAJANGILI WACHUKUE MATREKTA WAKALIME LAA SIVYO WAJIANDAE NA KIFUNGO CHA MIAKA 25 JELA - PROF. MAGHEMBE

 Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (katikati) akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 24 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika leo terehe 10 Aprili, 2017 katika ukumbi wa LAPF mjini Dodoma. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Aloyce Nzuki na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Esther Malima.

NA HAMZA TEMBA - WMU
...................................................................................

Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe ametangaza mabadiliko makubwa katika biashara ya mkaa nchini na kusema kuwa kuanzia mwezi Julai mwaka huu hakuna mkaa wowote utakaosafirishwa kutoka wilaya moja kwenda nyingine ili kunusuru misitu inayoteketea kwa kasi hapa nchini.

Amesema hayo leo wakati akifungua mkutano wa 24 wa baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Maliasili na Utalii uliofanyika katika ukumbi wa LAPF mjini Dodoma na kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali kutoka kwenye Idara, Vitengo na Taasisi mbalimbali zilizopo chini ya Wizara hiyo.

“Kuanzia mwezi Julai hakuna ruhusa ya kutoa vibali vya kuhamisha mkaa kutoka wilaya moja kwenda wilaya nyingine, mkaa utachomwa, utauzwa ndani ya wilaya kwa ajili ya matumizi ya watanzania wanaohitaji nishati ya mkaa, lakini biashara ya mkaa ya kutoa Dodoma kwenda Dar es Salaam mpaka Zanzibar marufuku.

“Wamekata misitu yetu yote, mito yetu imekauka, tunashindwa kupata maji ya umwagiliaji kwasababu watu wengi huko nje wanataka mkaa wetu, Tanzania jamani sio shamba la bibi, wale wote watakaotoa mkaa kutoka eneo moja hadi jingine kinyume na sheria hii watashuulikiwa kwa utaratibu wa uhujumu uchumi”, amesema Maghembe.

Amesema kuwa kwa upande wa miji mikubwa kama Dar es Salaam, Dodoma, Morogoro na Tanga vitaanzishwa viwanda maalumu vya kuzalisha mkaa ambao utauzwa kwa vibali maalumu katika mikoa mbalimbali hapa nchini. Amesema mkaa huo hautakuwa na athari nyingi za kimazingira kwa sababu utazingatia taratibu za uzalishaji endelevu.

Wakati huo huo, Waziri Maghembe amemuagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kumuhamisha kituo cha kazi Mkuu wa Kikosi cha Kufuatilia na Kuzuia Uharibifu wa Misitu wa Wakala hiyo, Arjason Mloge kutoka Makao Makuu ya Taasisi hiyo kwenda chuo cha Viwanda vya Misitu (FITI) kilichopo mkoani Kilimanjaro na badala yake atafutwe mtu mwingine muaminifu.

Amesema uamuzi huo ni kufuatia udhaifu uliojitokeza katika usafirishaji wa rasilimali za misitu ndani na nje ya nchi ikiwemo usafirishaji kwa kutumia nyaraka ambazo sio halisi "zilizodurufiwa". “Agizo hili litekelezwe mara moja kabla ya saa sita mchana wa leo na niwe nimepewa nakala ya barua hiyo ya uhamisho” amesema.

Kufuatia uamuzi huo amepiga marufuku kuanzia leo usafirishaji wa mazao ya misitu ndani na nje ya nchi kwa kutumia nyaraka zisizo halisi (Photocopies). Ameongeza kuwa katika kuunga mkono Sera ya Uchumi wa Viwanda ya Serikali ya awamu ya tano hakuna gogo litakalosafirishwa kwenda nje ya nchi.

“Wawekezaji wanahimizwa kujenga viwanda vya kuchakata magogo hayo hapa nchini ili kutoa ajira kwa Watanzania pamoja na kutoa faida halisi inayotokana na rasilimali hizo kwenye uchumi wa taifa”, amesema.

Akizungumzia changamoto ya mifugo kwenye maeneo ya hifadhi nchini amesema Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009 sehemu ya 21 (1) hairuhusiwi kabisha kuchunga mifugo katika Hifadhi za Taifa, Mapori ya Akiba, Mapori Tengefu na Hifadhi za Misitu. Amewataka watumishi wa Maliasili kusimamia Sheria hiyo pamoja na kutoa wito kwa wananchi kuifuata kikamilifu.

Katika hatua nyingine, Waziri Maghembe amewataka majangili wote nchini kuachana na biashara hiyo haramu ambayo hailipi kwa sasa na badala yake wachukue matrekta wakalime.

“Mtu ambaye alikuwa anaishi kwa kutegemea ujangili sasa atafute trekta akalime, kwa sababu akifanya ujangili tukamkamata tu, na tukimkamata atakaa kwenye hoteli ya mkuu wa magereza (magereza) kwa zaidi ya miaka 25”.

Aidha, Waziri Maghembe ametoa pongezi kwa watumishi wote wa Wizara ya Maliasili kwa kazi nzuri wanayofanya ya kupambana na ujangili nchini pamoja na ulinzi wa maliasili za taifa (Misitu, Wanyamapori na Mambo ya Kale) ambazo kwa pamoja zinachangia asilimia 20.5 kwenye pato la taifa. Amesema matokeo chanya ya kupambana na ujangili yameanza kuonekana japo ujangili bado upo.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Aloyce Nzuki amemueleza Waziri Maghembe kuwa maelekezo yote aliyoyatoa yamepokelewa kwa ajili ya kuyafanyiwa kazi, huku Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Prof. Alexandre Songorwa akimueleza Waziri huyo kuwa watalinda na kusimamia Malisili za Taifa na kwamba katu hawapo tayari kuandikwa kwenye vitabu kuwa walishiriki katika kutoweka kwa maliasili hizo.
Picha ya pamoja kati ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (katikati waliokaa) na wajumbe wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo baada ya kufungua mkutano huo leo terehe 10 Aprili, 2017 katika ukumbi wa LAPF mjini Dodoma.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 24 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika leo terehe 10 Aprili, 2017 katika ukumbi wa LAPF mjini Dodoma.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (katikati) akiimba wimbo wa Umoja wa Wafanyakazi (Solidarity Forever) muda mfupi kabla ya kufunga mkutano huo leo terehe 10 Aprili, 2017 pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa Baraza hilo, Esther Malima (wa pili kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Prof. Alexandre Songorwa (wa kwanza kulia) na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Mrimia Mchomvu.

 Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki (wa pili kshoto) akizungumza katika mkutano huo leo terehe 10 Aprili, 2017.
 Baadhi ya wajumbe wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Maliasili na Utalii wakisikiliza hotuba ya ufunguzi wa baraza hilo kutoka kwa Waziri wa Wizara hiyo, Prof. Jumanne Maghembe (hayuko pichani) katika ukumbi wa LAPF mjini Dodoma leo. 
 Baadhi ya wajumbe wa mkutano huo.
 Baadhi ya wajumbe na wageni waalikwa katika mkutano huo.
 Baadhi ya wajumbe katika mkutano huo.
 Baadhi ya wajumbe na wageni waalikwa katika mkutano huo.
 Baadhi ya wajumbe wa Sekretarieti.
 Baadhi ya wajumbe Sekretarieti wakiteta jambo nje ya ukumbi.

Tuesday, April 4, 2017

VACANCY ANNOUNCEMENT...


TANZANIA NATIONAL PARKS
Vacancies Announcement
Tanzania National parks (TANAPA) is a Parastatal Organization whose mandate is to manage and regulate the use of areas designated as National Parks. The organization currently manages sixteen National Parks which form part of larger protected ecosystems set aside to preserve Tanzania’s rich natural heritage.
In her endeavor to promote professionalism, the organization seeks to recruit high caliber, results oriented and self-driven professionals with integrity to fill Ninety-Two (92) posts of Park Rangers to work in various National Parks.
Park Rangers Grade IV (92 POSTS)
Reporting Relationship:Report to Park Wardens / Heads of Protection Department in the Respective Parks
Duty StationNational Parks
(i)        Qualifications:
Form IV Certificate with Basic Certificate in Wildlife Conservation from Pasiansi Wildlife Conservation Training Institute. Candidates with Certificate in basic military training from the National Service will be considered for recruitment after a successful completion of a three months field training conducted by TANAPA.
(iii)      Duties and Responsibilities:
• Conducting patrol activities
• Providing guard services in the Park
• Receiving and sending radio messages during patrols
• Undertaking cleaning functions at the ranger posts
• Arresting offenders
• Attending cases/court hearings, giving evidence in wildlife cases
• Participating in early fire burning and suppression activities
• Collecting information on unusual events and monitoring activities
• Writing patrol reports
• Participating in rescue operations.
(iv)      Age limit:Not above 25 years of age
(v)       Salary ScaleTAN 01
MODE OF APPLICATION
Only qualified applicants should submit their application with copies of relevant academic, professional certificates, copy of Birth certificate and testimonials so as to reach the undersigned within period of 21 days from the first date of appearance of this advertisement.

USIKOSE KIPINDI HIKI LEO.......

Image may contain: text and outdoor