slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Sunday, July 30, 2017

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII MHANDISI RAMO MAKANI, AMUAGIZA MKUU WA WILAYA YA MUHEZA KUSHUULIKIA MGOGORO WA HIFADHI YA MSITU WA DEREMA WILAYANI HUMO

Na Hamza Temba - WMU - Muheza, Tanga
.............................................................................

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani ameuagiza uongozi wa Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga kukutana na wakulima 879 wa vijiji vitano katika Tarafa ya Amani Wilayani humo kwa ajili kufanya uhakiki wa malipo ya fidia ya mazao waliyolipwa na Serikali ili kupisha eneo la hifadhi ya msitu wa Derema.

Mhandisi Makani ametoa agizo hilo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Msasa IBC, Tarafa ya Amani, Wilayani Muheza kufuatia malalamiko ya wananchi hao kupunjwa malipo yao wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo kwa ajili kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa zaidi ya miaka 15 baina Serikali na wananchi wa vijiji hivyo vya Kisiwani, Kwemdim, Msasa IBC, Antakae na Kambi.

Akisoma risala ya wakulima hao mbele ya Naibu Waziri Makani, Mwenyekiti wa Kamati ya wakulima hao, Mohammed Rama Shesha alidai kuwa jumla ya wakulima 1,128 wa vijiji hivyo wanailalamikia Serikali kwa kuwalipa viwango pungufu vya malipo ya fidia ya mazao yao tofauti na viwango vilivyolipwa na Serikali mwaka 2002 kupitia mradi wa FINIDA. Aidha, alidai kuwa kuna baadhi ya mazao pia hayakulipiwa kabisa fidia hizo.

Akizungumzia viwango vya fidia hizo Shesha alisema wananchi walilipwa Shilingi 28,800 kwa mche mmoja wa iliki na Shilingi 11,000 kwa mche mmoja wa mgomba. Alidai viwango hivyo vilibadilika kuanzia mwaka 2005 ambapo walilipwa Shilingi 3,315 kwa kila mche mmoja badala ya Shilingi 5,100 kama ilivyoainishwa kwenye viwango vya Serikali hivyo akaomba walipwe kiasi kilichobakia cha shilingi 1,785.

Akitolea ufafanuzi wa malalamiko hayo, Naibu Waziri Makani alisema idadi kamili ya wananchi waliohakikiwa katika eneo hilo ni 879 na sio 1,128 kama alivyodai mwenyekiti huyo. Aidha, alisema viwango vilivyotumiwa kuwalipa wananchi hao mwaka 2002 sio vya Serikali na kwamba vilitumiwa na mradi wa FINIDA uliofadhiliwa na Serikali ya Finland kwa ajili ya kulipa fidia wananchi wa mpakani na hifadhi hiyo ili kufanikisha zoezi la kuanisha mpaka wa hifadhi hiyo na kusaidia Serikali kutimiza azma ya kuhifadhi eneo hilo.

Alisema viwango halali vya Serikali vilivyopo kisheria kwa ajili ya kulipa fidia ya mimea hiyo ni kuanzia Shilingi 5,100 kwa kiwango cha juu kwa mmea uliokoma kufikia kiwango cha uzalishaji, Shilingi 3,315 kwa mmea wenye mwaka mmoja na Shilingi 2,040 kwa mmea wenye mwezi mmoja. Alisema viwango vingine vya malipo kwa kiwango cha chini ni Shilingi 204, Shilingi 102 na Shilingi 51.

Alisema Serikali iliamua kulipa kiwango cha Shilingi 3,315 kwa mazao yote ikiwemo yale yaliyostahili kulipwa kiwango cha chini kabisa cha Shilingi 51 ili kuweka uwiano na kurahisha zoezi hilo la malipo. Alihoji kama kuna mwananchi yeyote aliyelipwa chini ya kiwango hicho japokuwa kulikuwepo na wengine mazao yao yalistahili kulipiwa viwango hivyo, hakuna aliyejitokeza.

Kufuatia ufafanuzi huo aliuagiza uongozi wa Wilaya ya Muheza kutumia kipindi cha mwezi mmoja kuanzia leo Jumatatu kuonana na wakulima hao ili kuhakiki malipo yao na hatua zaidi ziweze kuchukuliwa kama kuna yeyote aliyezulumiwa apewe haki yake. 

"Kwa wale ambao tayari wana kumbukumbu zao vizuri wazilete mbele ya Serikali, kupitia wao pengine tunaweza kupata picha ya jumla pengine kulikua na mapungufu kwenye malipo. Kuanzia jumatatu ijayo Mhe. DC tulitekeleze hilo la kukusanya nyaraka kwa wale walizonazo tuweze kuzilinganisha na zile tulizokua nazo Serikalini tujadiliane nao kwamba ni kitu gani kimebaki tofauti katika maeneo yale yale mliyofanyiwa uhakiki", alisema Mhandisi Makani.

Alisema kwa wale ambao wamepoteza nyaraka zao za malipo wataandaliwa utaratibu maalum wa uhakiki kwa kuwa kumbukumbu zote za malipo zipo kwenye Kompyuta za halmashauri ya Wilaya ya Muheza.

Alisema lengo la Serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha inamaliza kabisa migogoro ya ardhi nchini. “Tutahakikisha tunaboresha zaidi usimamizi wa uhifadhi wa rasilimali zetu za misitu, wanyamapori na nyinginezo kuhakikisha migogoro hiyo inapungua kwa kasi kuelekea kwenye sifuri, zero rate", alisema Makani.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mwanaisha Tumbo alisema, Serikali ya Wilaya imepokea maelekezo hayo na itayafanyia kazi na kwamba maafisa wa Halmashauri watafika katika kila kijiji siku ya Jumatatu na Jumatano kwa ajili ya kuendesha zoezi hilo la uhakiki.

Akizungumzia zoezi la fidia Mkuu huyo wa Wilaya alisema pamoja na wananchi hao kulipwa fidia za mazao yao ambayo yalilipwa kwa awamu tatu, asilimia 50 mwaka 2005, asilimia 25 mwaka 2006 na asilimia 25 mwaka 2008, pamoja na asilimia 23 kama fidia ya ucheleweshaji wa deni, Serikali pia itawapa maeneo ya fidia ambapo kila mwananchi aliyeathirika eneo lake atapewa ekari tatu.

Alisema eneo ambalo limeanishwa kwa ajili ya kuwagawia wananchi hao ni lililokuwa shamba la mkonge Kibaranga ambalo lina ukubwa wa hekta 1370 sawa na ekari 3425 na lilikua likimilikiwa na Bodi ya Mkonge, eneo hilo lilitolewa tamko ya kufutiwa umiliki wake na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli mwezi Julai, 2016.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (katikati), akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Msasa IBC wilaya ya Muheza mkoani Tanga jana wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo kwa ajili kutatua mgogoro wa hifadhi ya msitu wa Derema. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mwanaisha Tumbo. 
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (katikati), akimuonesha mwenyekiti wa kamati ya wakulima wa vijiji vitano vya tarafa ya Amani, Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga, Mohammed Ramadhani Shesha viwango halali vya serikali vya kulipia fidia za mazao kwa wananchi waliondolewa katika eneo la hifadhi ya msitu wa Derema wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo jana kwa ajili ya kutatua migogoro wa hifadhi hiyo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mwanaisha Tumbo.  
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (kulia), akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Msasa IBC wilaya ya Muheza mkoani Tanga jana wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo kwa ajili kutatua mgogoro wa hifadhi ya msitu wa Derema.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani, (wa tatu kushoto), akiangalia eneo la Msitu wa hifadhi ya Derema na viongozi wa wilaya ya Muheza Muheza wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo jana kwa ajili ya kutatua mgogoro wa hifadhi hiyo. 
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (kulia), akisalimiana na wananchi wa Kijiji cha Msasa IBC wilaya ya Muheza Mkoani Tanga jana wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo kwa ajili ya kutatua mgogoro ya hifadhi ya msitu wa Derema. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (kushoto), akimuonesha mwenyekiti wa kamati ya wakulima wa vijiji vitano vya tarafa ya Amani, Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga, Mohammed Ramadhani Shesha (kulia) viwango halali vya serikali vya kulipia fidia za mazao kwa wananchi waliondolewa katika eneo la hifadhi ya msitu wa Derema wakati wa ziara yake ya siku moja wilayani humo jana kwa ajili ya kutatua migogoro wa hifadhi hiyo. 

Friday, July 28, 2017

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII INJINIA RAMO MAKANI AFUNGA RASMI MKUTANO WA SITA WA TANAPA KWA WAHARIRI NA WANAHABARI WAANDAMIZI MKOANI TANGA


Naibu Waziri Maliasili na Utalii Injinia  Ramo Makani akimkabidhi
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006)Ltd, Absalom Kibanda cheti cha ushiriki wa Mkutano wa Mwaka na Wahariri na Wanahabari Waandamizi nchini uliohitimishwa jioni ya leo jijini Tanga.Katika hatua hiyo ya kukabidhiwa vyeti,washiriki wote walikabidhiwa vyeti vya ushiriki wao kwa ukamilifu katika mkutano huo.

Mgeni rasmi,Naibu Waziri Maliasili na Utalii Injinia  Ramo Makani(wanne kulia) akiwa katika picha ya pmoja na washiriki wa Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika jana kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'. 
Naibu Waziri Maliasili na Utalii Injinia Ramo Makani leo akizungumza jambo wakati akifunga rasmi Mkutano wa Mwaka na Wahariri na Wanahabari Waandamizi nchini jijini Tanga.

Sehemu ya Meza kuu,kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF),Theophil Makunga,Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO),Dkt.Hassan Abbas,Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa TANAPA,Bwa.Ibrahim Mussa ,Mgeni rasmi-Naibu Waziri Maliasili na Utalii Mhe. Ramo Makani,Mkuu wa Wilaya ya Tanga,Mhe.Thobis Mwilapa.

Baadhii ya washiriki wa mkutano huo wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo kabla ya kufungwa rasmi jioni ya leo.
Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa TANAPA,Bwa.Ibrahim Mussa akiwashukuru washiriki wa Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika jana kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga ,na kuhitimishwa rasmi jioni ya leo na Naibu Waziri Maliasili na Utalii Mhe. Ramo Makani .
Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mh.Thobias Mwilapa akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mh.Martin Shigella wakati wa kutoa salamu za shukurani kabla ya kufungwa rasmi kwa Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika jana kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'.

 Meneja Mahusiano wa TANAPA,Pascal Shelutete akizungumza jambo kabla ya mgeni rasmi kufunga Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika jana kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga.












Thursday, July 27, 2017

WAZIRI WA MALIASILI, PROF. JUMANNE ABDALLAH MAGHEMBE AFUNGUA MKUTANO WA MWAKA WA WAHARIRI NA WANAHABARI WAANDAMIZI ULIONDALIWA NA TANAPA JIJINI TANGA, AWATAKA KUTUMIA KALAMU ZAO KUELIMISHA JAMII KUHUSU UHIFADHI ENDELEVU

NA HAMZA TEMBA -WMU - TANGA
...................................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe amevipongeza vyombo vya habari nchini kwa mchango wake katika vita dhidi ya ujangili huku akitoa rai kwa vyombo hivyo kuongeza bidii katika kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa uhifadhi endelevu wa maliasili za taifa kwa faida ya jamii iliyopo na vizazi vijavyo.
Prof. Maghembe ametoa pongezi na rai hiyo leo wakati akifungua mkutano wa sita wa mwaka wa wahariri na wanahabari waandamizi wa vyombo vyote vya habari nchini ulioandaliwa na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) jijini Tanga huku kaulimbiu ya mkutano huo ikiwa UTALII WA TANZANIA YA UCHUMI WA VIWANDA.
"Ujangili bado upo, Majangili tumepambana nao kweli kweli, na ninyi wanahabari mmetusaidia sana katika kuhabarisha jamii juu ya matukio ya kukamatwa kwao na hukumu wanazozipata, jambo ambalo limesaidia kujenga uoga kwa watu kushiriki katika vitendo hivyo", alisema Maghembe.
Alisema hofu hiyo pamoja na jitihada za Serikali za kupambana na ujangili imesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza matukio ya ujangili nchini hasa katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita ambapo mizoga ya tembo inayotokana na ujangili imepungua kwa kiasi kikubwa ukilinganisha ni miaka iliyopita.
Akizungumzia changamoto ya mifugo kwenye maeneo ya hifadhi nchini amesema sheria za uhifadhi zinakataza watu kuingiza mifugo kwenye maeneo yaliyohifadhiwa kisheria, hivyo ni wajibu kwa wanahabari kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa kutii sheria hizo.  "Ni vema wanahabari wakatumia kalamu zao vizuri kuelimisha jamii juu ya athari za muingiliano wa binadamu, mifugo na wanyamapori".
Alisema wanyamapori wanabeba virusi vya magonjwa mbalimbali ikiwemo homa ya bonde la ufa, ndigana, kifua kikuu, homa za vipindi (brucolosis) na kimeta, Magonjwa ambayo yanaweza pia kuambukiza mifugo na binaadamu wanaoishi karibu na wanyamapori. Alisema kuwa endapo muingiliano huo utaendelea kuwepo kwa muda mrefu unaweza kusababisha mlipuko mkubwa wa magonjwa hayo kwa binaadamu na mifugo hivyo kusababisha vifo vingi kwa wakati mmoja.
Prof. Maghembe alisema kumekuwepo na kisingizio cha kumega maeneo ya hifadhi nchini kwa ajili ya matumizi ya kawaida kutokana na ongezeko la wananchi jambo ambalo sio sahihi na kwamba njia pekee na salama ni kubadili mfumo wa matumizi ya rasilimali zilizopo ikiwepo ya ardhi kwa kutumia sayansi na teknolojia na kuweka matumizi bora ya ardhi kwa kulenga matokeo chanya.
Akizungumzia sekta ya utalii, Prof. Maghembe alisema wanahabari wanapaswa kuwa sehemu ya kukuza uchumi wa nchi kwa kushiriki moja kwa moja katika utoaji wa taarifa sahihi kwa Watanzania na wageni kuhusu sekta hiyo bila ubaguzi wa aina yeyote.
"Tuipende nchi yetu, tuitangaze na kuilinda, na katika habari hizi za uchumi tuweke itikadi zetu pembeni tuandike habari za kujenga nchi yetu", alisema Prof. Maghembe.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa, Alan Kijazi amesema sekta ya utalii inachangia asilimia 17.2 ya pato la taifa na asilimia 25 ya mapato yote ya fedha za kigeni. Alisema asilimia 80 ya wageni wanaokuja nchini wanatembelea hifadhi za Taifa hususan za ukanda wa Kaskazini jambo ambalo linaweka msukumo wa kuendeleza na kutangaza hifadhi za nyanda zingine ili kuongeza idadi ya watalii na pato la taifa.
Akizungumzia mchango wa TANAPA katika uchumi wa taifa, Kijazi alisema mchango huo umeongezeka ambapo katika mwaka 2015/2016 ilichangia Shilingi bilioni 27 katika mfuko mkuu wa Serikali na mwaka 2016/2017 ikachangia bilioni 34 sawa na ongezeko la bilioni saba.
Pamoja na mafanikio hayo alisema jukumu la kuendeleza uhifadhi nchini haliwezi kufanikiwa kwa jitihada za Serikali pekee bila kushirikisha wananchi kupitia vyombo vya habari, Hivyo akatoa rai kwa wanahabari kuiunga mkono Serikali katika kunadi sera za uhifdhi endelevu kwa maslahi ya taifa.
Waziri wa Utalii na Maliasili Prof.Jumanne Maghembe akizungumza jambo alipokuwa akifungua Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika leo kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga, ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'.
 
Baadhi ya Wahariri na Wanahabari waandamizi wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye mkutano wa Wahariri wa Vyombo vya Habari na Waandishi Waandamizi ulioanza kufanyika leo kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga, ulioandaliwa na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA),ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mh Martin Shigella akiwakaribisha wageni mbalimbali waliofika kuhudhuria mkutano wa mwaka wa Wahariri na Wanahabari waandamizi,uliofanyika kwenye ukumbi uliopo kwenye ofisi zake.Mkutano huo umebeba kauli kuu ambayo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'.
Mkurugenzi Mkuu wa Shrika la Hifadhi za Taifa,(TANAPA),Allan Kijazi akimkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Utalii na Maliasili Prof.Jumanne Maghembe kufungua Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika leo kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'.
Mkurugenzi Mkuu wa Shrika la Hifadhi za Taifa,(TANAPA),Allan Kijazi akimkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Utalii na Maliasili Prof.Jumanne Maghembe kufungua Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika leo kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'.
Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete akiwakaribisha wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye Mkutano wa Sita wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa Wahariri na Waandishi waandamizi ulioanza kufanyika leo kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa jijini Tanga, ,ambapo kauli mbiu ya mkutano huo ni 'Utalii na Tanzania ya Viwanda'.
Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Ltd.Absalom Kibanda akitoa salamu za shukurani kwa waandaji wa mkutano pia na kueleza changamoto kadhaa zinazopaswa kurekebishwa/kufanyiwa kazi na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA).
Baadhi ya Wahariri wakibadilishana mawazo kabla ya kuanza kwa mkutano huo.
Picha ya pamoja ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe, viongozi wa Serikali, Wahariri na Waandishi Waandamizi walioshiriki mkutano huo.


 (PICHA NA MICHUZI JR BLOG)

Monday, July 24, 2017

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, PROF. JUMANNE MAGHEMBE APOKEA MABILIONEA 26 KUTOKA MABARA YOTE DUNIANI KATIKA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI

Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na Mabilionea 26 kutoka taasisi ya Young Presidents Organisation  (YPO) wakiwa na wenza wao katika moja ya hoteli ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wakati wa mapokezi yao jana kwa ajili ya ziara yao ya siku tatu nchini Tanzania.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Alan Kijazi (katikati waliosimama) akizungumza na Mabilionea hao. Kulia kwake ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe .
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na Mabilionea hao jana katika moja ya hoteli ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Alan Kijazi.

Kiongozi wa msafara wa Mabilionea hao, Perry Amber akizungumza wakati wa mapokezi hayo jana katika moja ya hoteli ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. 
Mabilionea hao kutoka taasisi ya Young Presidents Organisation (YPO) wakimsikiliza Waziri Maghembe.
................................................................................

Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe amewapokea Mabilionea 26 wa taasisi ya Young Presidents Organisation  (YPO) wakiwa na wenza wao katika Hifadhi ya Taifa  Serengeti kwa ajili ya kutembelea vivutio vya utalii katika ziara yao ya siku 3 nchini Tanzania.

Mabilionea hao ambao wanatoka katika mabara yote duniani wapo nchini Tanzania kama sehemu ya ziara yao katika nchi 8 duniani ikiwemo Uingereza, Rwanda, Maldives, Nepal, Bhutan na Rajastan.

Katika hafla ya Chakula cha jioni alichowaandalia Wageni wake,  Prof. Maghembe aliwakaribisha Tanzania na kwenye Maajabu ya Dunia yanayobebwa na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Alisisitiza "hakuna eneo lolote katika uso wa Dunia lenye mkusanyiko wa wanyama wanaokula majani (herbivores) na wale wanaokula nyama (canivores) kama Serengeti". 

Prof. Maghembe aliwaeleza Wageni wake kuwa kuhifadhi ni gharama kubwa inayobebwa na Tanzania kwa niaba ya Dunia. Hivyo akawaomba wageni hao wawe mabalozi wa kuitangaza Tanzania kama eneo lenye  amani na vivutio vyenye ubora wa pekee. Hatua hiyo italeta watalii wengi na kuiongezea Tanzania mapato.

Aidha, aliwaomba warudi tena kuwekeza nchini ili washiriki kwenye uchumi unaokua kwa wastani wa 7% kwa kipindi cha miaka 15 sasa.

Wednesday, July 19, 2017

RAIS DKT MAGUFULI AWATAKA WENYE MIFUGO MINGI KUIUZA BADALA YA KUICHUNGA HIFADHINI





TANZANIA IS RATED THE BEST SAFARI COUNTRY OF 2017 IN AFRICA


THE NETHERLANDS – SafariBookings.com has conducted an in-depth analysis of reviews from safari tourists and acclaimed Africa experts to determine the continent’s best country for safaris. And the winner? TANZANIA came out on top – the country is the clear winner and has been awarded our best safari country for 2017.

More than 2,500 reviews were used in this comprehensive research. Contributions came from safari-goers all over the world. And 22 reputable guidebook authors – working for Lonely Planet, Rough Guides, Frommer’s, Bradt and Footprint, who make-up the SafariBookings expert panel – also contributed reviews.

Tanzania with its teeming wildlife and astounding natural beauty on average had the highest scores. The country won only by a slim margin though from Zambia. Interestingly, when the results are broken down, members of the expert panel rated Tanzania the highest while safari tourists had a preference for Zambia.

In 2013 SafariBookings conducted its first-ever review analysis to determine the best country for safaris in Africa. Tanzania won that contest clearly. However, because things change so rapidly in Africa we conducted another analysis in 2017, using new reviews from safari tourists and from the guidebook authors on our expert panel. One thing that hasn’t changed is Tanzania’s popularity, once again voted the best safari country in Africa.

Best country for wildlife

SafariBookings analysis also determined that Tanzania was the best country in Africa for spotting wildlife. Given the exceptional wildlife-viewing opportunities in parks such as the superlative Serengeti and the wildlife-rich Ngorogoro Conservation area, this was unsurprising.


Recently, Tanzania has received a good number of famous superstars from around the Globe visiting her tourist attractions. Those visitors includes the former Israel Prime Minister, Ehud Barak, football superstars such as David Beckham, Morgan Schneiderlin, Mamadou Sakho, Victor Wanyama, Christian Erikssen, Wayne Rooney and Everton Football Club. Others who fall under the category of Musician and Actors includes Will Smith, Usher Raymond, Harrison Ford and Sanjay Dutt of India.


Indeed, Tanzania is the Africa Tourist Destination.


WELCOME/KARIBU ! #visittanzania The land of #kilimanjaro#zanzibar and the #serengeti

YOU MAY ALSO REFFER THE NEWS FROM SAFARIBOOKINGS BY CLICKING THE LINK BELOW: https://www.safaribookings.com/blog/best-safari-country-2017

Monday, July 17, 2017

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, PROF. JUMANNE MAGHEMBE AKABIDHI TUZO YA HESHIMA KWA DKT. JANE GOODALL

Ministry of Natural Resources and Tourism through Tanzania National Parks (TANAPA) has awarded Dr. Jane Goodall a Sokwe Conservation Award in recognition of her incredible work of almost 60 years towards Chimpanzees research in Gombe National Park. The award was presented to her yesterday in Dar es Salaam by the Minister of Natural Resources & Tourism, Hon. Prof. Jumanne Maghembe.


Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) limetoa tuzo maalum ijulikanayo kama Sokwe Conservation Award kwa Dkt. Jane Goodall kutokana na mchango wake mkubwa wa takriban miaka 60 ya utafiti wa Sokwe katika Hifadhi ya Taifa ya Gombe.Tuzo hiyo ilikabidhiwa kwake jana Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia), akimkabidhi Tuzo ya Uhifadhi Wanyama aina ya Sokwe, Dkt. Jane Goodall, aliyekuwa akifanya utafiti wa Wanyama hao kwa miaka 60 katika hifadhi mbalimbali na baadaye kujikita katika Hifadhi ya Gombe.  Dkt. Jane Goodall akionyesha cheti chake cha kutambua mchango wake katika Uhifadhi Wanyama aina ya Sokwe.  Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe, akimkabidhi Tuzo ya Uhifadhi Wanyama aina ya Sokwe, Dkt. Jane Goodall, aliyekuwa akifanya utafiti wa Wanyama hao kwa miaka 60 katika hifadhi mbalimbali na baadaye kujikita katika Hifadhi ya Gombe. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Tanapa, George Waitara na Bi. Gertude Mongella.  Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe Profesa Maghembe akizungumza wakati wa hafla ugawaji wa tuzo kwa Dk. Jane Goodall ambaye ametoa mchango mkubwa kwenye sekta ya uhifadhi na kubainisha tabia za sokwe ambazo watu wengi hawazijui. Profesa Maghembe aliongeza kuwa mtafiti huyo ambaye ni raia wa Uingereza amebainisha katika tafiti zake kwamba sokwe wana fikiri na wana hisia kama walivyo binadamu. Picha zote na Kajunason Blog/Cathbert Kajuna.  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Alan Kijazi akitoa machache wakati wa hafla ya ugawaji wa tuzo kwa Dk. Jane Goodall ambaye ni muhifadhi Wanyama aina ya Sokwe aliyekuwa akifanya utafiti wa Wanyama hao kwa miaka 60.  Dkt. Jane Goodall, ambaye aliyekuwa akifanya utafiti wa Wanyama aina ya Sokwe kwa miaka 60 akitoa shukrani za pekee.    Wageni waalikwa waliofika kuhudhuria hafla hiyo.