slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Friday, July 14, 2017

MAAJABU YA UHIFADHI TANZANIA: SIMBA AMNYONYESHA MTOTO WA CHUI


Simba apatikana akimnyonyesha mwana wa Chui Tanzania                                                                                                                     JOOP VAN DER LINDE/NDUTU LODGE
Image captionSimba apatikana akimnyonyesha mwana wa Chui Tanzania

Mwana wa chui hawezi kubadili madoa doa katika ngozi yake lakini simba huyo hajali hilo.
Picha hizi ni za kwanza kuchukuliwa simba akimnyonyesha mwana wa chui kutoka jamii nyengine ya wanayama, kisa kisicho cha kawaida.
Wawili hao walionekana na Joop Van Der Linde mgeni katika katika eneo la Ndutu safari Lodge nchini Tanzania katika eneo la uhifadhi la wanyma pori la Ngorongoro.

Simba Nasikitok akimnyonyesha mwana huyo wa chui katika Ngorongoro
Image captionSimba Nasikitok akimnyonyesha mwana huyo wa chui katika Ngorongoro

Eneo hilo ni la Serengeti. Simba huyo amepewa jina Nosikitok na ana umri wa miaka mitano.
Simba huyo amewekewa mfumo wa GPS katika shingo yake ili kutambua anakokwenda na ana watoto watatu waliozaliwa kati ya mwezi Juni 27-28.

Daktari Hunter anasema Nosikitok ana watoto wachanga walio na umri sawa na mwana huyo wa chui wakiwa na wiki mbili hadi tatu hivi.
Image captionDaktari Hunter anasema Nosikitok ana watoto wachanga walio na umri sawa na mwana huyo wa chui wakiwa na wiki mbili hadi tatu hivi.

Daktari Luke Hunter , ambaye ni rais muhifadhi mkuu wa Panthera ,shirika kuu la ufugaji wa wanyama aina ya paka aliambia BBC kwamba kisa hicho ni cha kipekee.

Simba huyo alikuwa kilomita moja kutoka kwa nyumba yao ambapo kuna maficho ya watoto wake alipokutana na chuo huyo mdogo.Haki miliki ya pichaJOOP VAN DER LINDE/NDUTU LODGE
Image captionSimba huyo alikuwa kilomita moja kutoka kwa nyumba yao ambapo kuna maficho ya watoto wake alipokutana na chuo huyo mdogo.

Sio kitu ambacho nilijuwa ambapo simba angeweza kuwalea watoto wa simba mwengine.,...hiki ni kisa tofauti sana.
Sina kisa chengine chochote nikijuacho kati ya familia ya mnyama paka kwa mfano pale ambapo mnyama mmoja amechukua mwana wa mnyama mwengine katika familia hiyo hiyo na kumnyonyesha.
Simba wengi wa kike huwauwa watoto wa chui wanapokutana nao, na huwaona kama wapinzani katika mapambano ya kutafuta chakula.
Daktari Hunter anasema Nosikitok ana watoto wachanga walio na umri sawa na mwana huyo wa chui wakiwa na wiki mbili hadi tatu hivi.

Chui mtoto anayeishi na simbaHaki miliki ya pichaJOOP VAN DER LINDE/NDUTU LODGE
Image captionChui mtoto anayeishi na simba

Simba huyo alikuwa kilomita moja kutoka kwa nyumba yao ambapo kuna maficho ya watoto wake alipokutana na chuo huyo mdogo.
Alimchukua mwana huyo na kumlea kama wake na humlindi dhidi ya shambulio lolote.

No comments:

Post a Comment