slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Tuesday, July 31, 2018

SERIKALI KUKUZA UTALII KUPITIA MCHEZO WA GOLF – DK. KIGWANGALLA

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akimkabidhi Mcheza Golf mashuhuri zaidi duniani, Jack William Nicklaus wa nchini Marekeni zawadi ya kinyago cha Makonde walipoagana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere Jijini Dar es Salaam baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku 10 ya kutembelea vivutio vya utalii hapa nchini.

Na Hamza Temba-WMU
........................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla amesema Serikali itatumia fursa ya ujio wa Mcheza Golf mashuhuri zaidi duniani, Jack William Nicklaus kutoka nchini Marekeni kubuni viwanja vya mchezo huo karibu na maeneo ya vivutio vya utalii nchini ili kuvutia watalii wengi wa kimataifa na hivyo kukuza pato la sekta hiyo.

Dk. Kigwangalla amesema hayo jana mara baada ya kumuaga mchezaji huyo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere Jijini Dar es Salaam alipokuwa akirudi nchini kwao baada ya kumaliza ziara yake ya siku kumi yeye na familia yake katika vivutio mbali mbali vya utalii hapa nchini.

“Tutatumia utaalamu na uzoefu wake kwenye mchezo wa Golf kwa kumtaka aje na kampuni yake atusaidie kutengeneza plan (mpango) ya kujenga viwanja vya golf.

“Amedesign viwanja zaidi ya 300 kwenye nchi zaidi ya 50 duniani na nchi hizo zimefaidika, amesema katika project zake zaidi ya asilimia 90 zinafanya vizuri pamoja na kwamba ni uwekezaji wa gharama kubwa bado imelipa kwa kiasi kikubwa na hakuna hata kiwanja kimoja kimepata hasara na vimekuwa vinasaidia kukuza utalii katika nchi hizo.

“Lengo letu ni kutengeneza ukanda maalum wa viwanja vya golf ambao utakuwa na viwango vya kimataifa na utavutia wacheza Golf kutoka nchi mbalimbali duniani, kwahiyo hii ni aina nyingine ya utalii wa watu wenye uwezo ambao wataleta pesa nyingi kwa wakati mmoja.

 “Tutaendelea kuwa na mawasiliano nae na kampuni yake ili tuweze kuona anawezaje kutusaidia na sisi walau tuwe na hiyo plan (mpango) lakini pia tukapata wawekezaji wakaja kuwekeza kwenye viwanja vya golf vitakavyojengwa karibu na fukwe, karibu na mito au hifadhi za Taifa ambapo tutavutia sio tu watalii ambao wanaokuja  kufanya utalii wa wanyamapori au beach lakini tutavutia watalii wanaokuja mahsusi kwa kwa ajili ya utalii wa golf” alisema Dk. Kigwangalla.

Wakati huo huo Dk. Kigwangalla amesema Serikali itaendelea kuheshimu na kujali maslahi ya wageni mashuhuri wanaokuja nchini ikiwemo ya usiri wa safari zao na kwamba atakayetaka aje kimya kimya na aondoke kimya kimya atapata heshma hiyo na atakayekubali kuwa wazi naye pia atapata heshma hiyo.

Kwa upande wake Jack Nicklaus alisema amefurahishwa sana na vivutio mbalimbali vya utalii alivyovishuhudia katika safari yake hapa nchini pamoja na ushirikiano na ukarimu mzuri kutoka kwa watanzania na ameahidi kuwa balozi wa utalii wa Tanzania huo aendako.

Jack Nicklaus ndiye mchezaji mwenye tuzo nyingi kuliko wachezaji wengine wa mchezo huo hapa duniani kwa sasa, ameweka rekodi ya kushinda mashindano ya kulipwa 117 na mashindano makubwa 18 (major champions). 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiagana na Mcheza Golf mashuhuri zaidi duniani, Jack William Nicklaus wa nchini Marekeni katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere Jijini Dar es Salaam baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku 10 ya kutembelea vivutio vya utalii hapa nchini.
  Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiwa na Mcheza Golf mashuhuri zaidi duniani, Jack William Nicklaus wa nchini Marekeni katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere Jijini Dar es Salaam muda mfupi kabla ya kuondoka kurudia kwao baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku 10 ya kutembelea vivutio vya utalii hapa nchini.
  Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla na Mcheza Golf mashuhuri zaidi duniani, Jack William Nicklaus wa nchini Marekeni wakitumbuizwa na kikundi cha ngoma katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere Jijini Dar es Salaam muda mfupi kabla ya kuondoka kurudia kwao baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku 10 ya kutembelea vivutio vya utalii hapa nchini.
  Picha ya pamoja ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, Mcheza Golf mashuhuri zaidi duniani, Jack William Nicklaus wa nchini Marekeni na familia yake na uongozi wa Bodi ya Utalii Tanzania ukiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi, Jaji Mst. Thomas Mihayo muda mfupi kabla ya ugeni huo kuondoka na kurudi kwao.

Sunday, July 29, 2018

WAZIRI KIGWANGALLA AMETOA SIKU 7 KWA KAMPUNI YA UCHIMBAJI MADINI YA TANZAM 2000 KUONDOKA KATIKA PORI LA AKIBA

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akikagua mazingira ya Pori la Akiba Moyowosi/Kigosi alipotembelea pori hilo juzi katika wilaya ya Bukombe mkoani Geita ambapo amegiza itolewe ilani ya siku 7 kwa kampuni ya Tanzam 2000 iliyokuwa ikifanya utafiti wa madini ya dhahabu ndani ya pori hilo iondoe mali zake zote na endapo itakaidi zitaifishwe kuwa mali ya Serikali. Kushoto kwake ni Meneja wa Pori hilo, Benjamin Kijika na Kaimu Mkurugenzi Mkuu TAWA, Mabula Misungwi.

Na Mwandishi Wetu
..........................................................
Kampuni ya uchimbaji madini ya Tanzam 2000 iliyokuwa ikifanya utafiti wa madini ya dhahabu katika eneo la Luahika ndani ya Pori la Akiba Moyowosi/Kigosi imetakiwa kuondoa vifaa na mitambo yake katika eneo la hilo ndani ya siku saba kwa amri ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla.

Dk. Kigwangalla ameiagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA kutoa ilani ya siku saba kwa kampuni hiyo iondoe vifaa na mitambo yake katika eneo hilo na endapo muda huo utapita bila kufanya hivyo mali hizo zitataifishwa na kuwa mali ya Serikali kwa kuwa wao ni wavamizi kwa mujibu wa sheria.

Waziri Kigwangalla ametoa agizo hilo juzi alipotembelea pori hilo katika wilaya ya Bukombe mkoani Geita ambapo alihitimisha ziara yake ya siku 25 aliyoipa jina la Pori Kwa Pori kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi nchini na kutatua changomoto zake.

Alisema uwepo wa vifaa na mitambo ya muwekezaji huyo ndani ya hifadhi hiyo imekuwa kishawishi kikubwa kwa wachimbaji wadogo wa madini kuvamia maeneo hayo wakiamini kuwa eneo hilo lina dhahabu na kwamba bado linaruhusiwa kwa shughuli za uchimbaji.

Awali Meneja wa Pori hilo, Benjamin Kijika alisema kampuni hiyo ilipewa kibali na Wizara ya Malisili na Utalii kwa ajili ya kufanya utafiti wa madini ya dhahabu katika eneo hilo kwa mwaka 2005 hadi 2010 na kuongezewa muda hadi 2012.

Alisema wakati kibali hicho kinatolewa Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori namba 5 ya mwaka 2009 ambayo inazuia tafiti kama hizo na shughuli nyingine za kibinaadamu kwenye maeneo ya hifadhi ilikua bado haijatoka.

Alisema baada ya hapo wizara haikutoa tena kibali kwa kampuni hiyo licha ya wizara ya madini kuipa kibali cha kuchimba dhahabu katika eneo hilo mwaka 2013. Aliongeza kuwa kwa nyakati tofauti Wizara ya Maliasili imeitaka kampuni hiyo iondoe mali zake zote ndani ya eneo hilo, agizo ambalo bado halijatekelezwa mpaka sasa.

Kwa upande wake aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Josephat Paulo Maganga alisema atasimamia utekelezaji agizo hilo la Waziri Kigwangalla ili eneo hilo liendelee kuhifadhiwa kwa mujibu wa sheria.

Alisema hifadhi hiyo inakabiliwa na changamoto kubwa ya uvamizi wa mara kwa mara wa wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu hususan katika eneo la Kigosi Kaskazini na hivyo kupelekea uharibu mkubwa wa mazingira katika hifadhi hiyo.

Alisema ili kukabiliana na changamoto hiyo pori hilo limeanzisha kambi mbili za ulinzi katika eneo hilo kwa ajili ya kudhibiti uharibifu huo ambapo mpaka sasa kesi 24 zenye wachimbaji haramu 52 zimeshafikishwa mahakamani huku kukiwa na vielelezo kadhaa ambavyo ni pamoja na baiskeli 102, viroba vya mchanga unaosadikika kuwa na madini ya dhahabu na vifaa vya uchimbaji.

Pori la Akiba Moyowosi/Kigosi ni muunganiko wa mapori mawili yenye ukubwa wa kilometa za mraba 21,060. Pori la Moyowosi lipo katika wilaya za Kibondo na Kakonko (Kigoma) na Pori la Kigosi katika wilaya ya Biharamulo (Kagera), Bukombe na Mbogwe (Geita), Kahama (Shinyanga) na Kaliua (Tabora).

Pori hili lina umuhimu mkubwa kiikolojia na kiuchumi kwakuwa pia ni ardhi oevu ambayo ni chanzo kikubwa cha maji ya ziwa Nyamagoma na Sagara ambayo huingiza maji mto Malagarasi na hatimaye ziwa Tanganyika, maji hayo hutumika kwa matumizi mbalimbali ya majumbani na kilimo. Pia hifadhi hiyo ni  makazi muhimu ya wanyamapori adimu kama Nzohe ambao huliingizia Taifa fedha za kigeni.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akimuagiza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA, Mabula Misungwi (Kulia) kutoa ilani ya siku 7 kwa kampuni ya uchimbaji madini ya Tanzam 2000 ili itoe mali zake zote katika eneo la Pori la Akiba Moyowosi/Kigosi alipotembelea pori hilo juzi katika wilaya ya Bukombe mkoani Geita na endapo muda huo utapita zitaifishwe kuwa mali na Serikali.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akikagua vifaa na mitambo ya kampuni ya uchimbaji madini ya Tanzam 2000 katika eneo la Luahika ndani ya Pori la Akiba Moyowosi/Kigosi alipotembelea pori hilo juzi katika wilaya ya Bukombe mkoani Geita ambapo amegiza itolewe ilani ya siku 7 kwa kampuni hiyo iondoe mali zake zote na endapo itakaidi zitaifishwe kuwa mali ya Serikali,  Nyuma yake ni Meneja wa Pori hilo, Benjamin Kijika.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akikagua vifaa na mitambo ya kampuni ya uchimbaji madini ya Tanzam 2000 katika eneo la Luahika ndani ya Pori la Akiba Moyowosi/Kigosi alipotembelea pori hilo juzi katika wilaya ya Bukombe mkoani Geita ambapo amegiza itolewe ilani ya siku 7 kwa kampuni hiyo iondoe mali zake zote na endapo itakaidi zitaifishwe kuwa mali ya Serikali,  Kulia ni Meneja wa Pori hilo, Benjamin Kijika.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akioneshwa vielelezo (mchanga wa madini ya dhahabu na baiskeli) walivyokamatwa navyo wachimbaji wadogo wa madini katika eneo Pori la Akiba Moyowosi/Kigosi na Meneja wa Sekta ya Kigosi Kaskazini, Salum Kulunge alipotembelea pori hilo juzi katika wilaya ya Bukombe mkoani Geita ambapo amegiza itolewe ilani ya siku 7 kwa kampuni ya Tanzam 2000 iliyokuwa ikifanya utafiti wa madini ya dhahabu ndani ya pori hilo iondoe mali zake zote na endapo itakaidi zitaifishwe kuwa mali ya Serikali.

Thursday, July 26, 2018

DK. KIGWANGALLA AAGIZA WAVAMIZI MAENEO YA HIFADHI MKOANI KIGOMA WAHAME MARA MOJA

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akifuatilia Sokwe Mtu kwenye mapito yao ndani ya Hifadhi ya Taifa Gombe alipotembelea hifadhi hiyo jana wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani Kigoma.

Na Hamza Temba-Kigoma
........................................................

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla ameagiza wavamizi wote waliopo ndani ya Pori la Akiba Kigosi/Moyowosi na Hifadhi ya Msitu wa Makere mkoani Kigoma waondoke mara moja kupisha maeneo hayo yaendelee kuhifadhiwa kwa mujibu wa Sheria.

Dk. Kigwangalla ametoa agizo hilo jana alipokuwa akizungumza na uongozi wa mkoa wa Kigoma, ukiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Brigedia Jenerali Mstaafu Emanuel Maganga ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake ya kikazi mkoani humo. 

Alisema taarifa za kiitelijensia zinaonyesha kuwa wengi wa wavamizi hao ambao wameanzisha makazi, kilimo na ufugaji ni raia kutoka nchi jirani ambao pia wamekuwa wakijihusisha na uharibifu wa mazingira na vitendo vya ujangili.

"Haivumiliki kwa kiongozi yeyote mzalendo kwa nchi yake ambaye anajua kabisa maeneo yetu yamewekwa akiba kwa ajili ya uhifadhi na tunawazuia hata wananchi raia kuyatumia alafu wanakuja raia wa nchi nyingine wanaachiwa wafanye wanavyotaka, hapana hili halikubaliki" alisisitiza Dk. Kigwangalla huku akiutaka uongozi wa Mkoa huo usaidie kusimamia Sheria na wavamizi hao waondoke mara moja. 

Aidha, ametoa kipindi cha miezi mitatu kwa watu wote waliovamia maeneo ya kinga za hifadhi (bafa) ambayo ni mita 500 kutoka mpaka wa hifadhi na vijiji waondoke kwa hiari yao wenyewe kabla ya kuondolewa kwa nguvu.

Katika hatua nyingine, Waziri Kigwangalla ameliagiza Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania TANAPA  kushirikiana na uongozi wa mkoa wa Kigoma na Halmashauri husika pamoja na Wakala wa Huduma za Barabara TANROADS katika ujenzi wa barabara inayounganisha Hifadhi ya Taifa ya Gombe na Mkoa huo na maeneo mengine.

Alisema, Serikali ya awamu ya tano imepanga kufungua Sakiti mpya za utalii ikiwemo ya Kanda ya Magharibi ambayo inaujumuisha mkoa wa Kigoma, hivyo ni lazima miundombinu ya barabara ijengwe na kuimarishwa ipitike muda wote ili hifadhi hizo zitumike zaidi kibiashara na ziweze kuchangia ipasavyo kwenye pato la Taifa kuliko ilivyo hivi sasa.

Ameuagiza pia uongozi wa Wakala wa Huduma za Misitu TFS kupima maeneo ya misitu ya vijiji jirani na Hifadhi ya Taifa ya Gombe ili kuona uwezekano wa kuyahifadhi kwa kutumia sheria za misitu na hivyo kutengeneza mapito muhimu ya Sokwe Mtu yatakayounganisha Hifadhi ya Taifa ya Gombe na Mahale na hifadhi za Misitu ya Tongwe East, Tongwe West, Masito East na Masito West. 

Kwa upande wake Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi hiyo, Donatus Bayona alisema changamoto kubwa iliyopo katika hifadhi hiyo ni miundombinu ya barabara ya kuunganisha hifadhi hiyo na maeneo mengine ikiwemo mji wa Kigoma ambapo amesema kwa sasa hifadhi hiyo inafikika kiurahisi kwa kutumia usafiri wa boti.

Akiwa katika hifadhi hiyo, Waziri Kigwangalla alizindua tukio la kuadhimisha miaka 50 ya kuanzishwa kwa Hifadhi hiyo na kuzindua rasmi kituo cha utafiti wa Sokwe Mtu ambacho kimefadhiliwa na Taasisi ya Jane Goodal, pia alitembelea Maporomoko ya Maji ya Kakombe ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii ndani ya hifadhi hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akipata maelezo kutoka kwa, Muongoza Watalii wa Hifadhi ya Taifa ya Gombe, Iddi Kaluse kuhusu Maporomoko ya Maji ya Kakombe ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii ndani ya  Hifadhi ya Taifa ya Gombe alipotembelea hifadhi hiyo jana wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Kigoma.
Baadhi ya Sokwe Mtu katika Hifadhi ya Taifa Gombe.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiangalia Sokwe Mtu katika Hifadhi ya Taifa Gombe alipotembelea hifadhi hiyo jana wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani Kigoma.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiangalia Sokwe Mtu katika Hifadhi ya Taifa Gombe alipotembelea hifadhi hiyo jana wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani Kigoma.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akipanda mlima kwa ajili ya kuwaona Sokwe Mtu katika Hifadhi ya Taifa Gombe alipotembelea hifadhi hiyo jana wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani Kigoma.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa Gombe alipotembelea hifadhi hiyo jana wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani Kigoma.
 Msafara wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ukielekea Hifadhi ya Taifa Gombe kwa kutumia usafiri wa boti.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akishuka kwenye boti alipotembelea Hifadhi ya Taifa Gombe wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani Kigoma jana.
 Mandari ya Hifadhi ya Taifa ya Gombe.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akicheza ngoma na kikundi cha Mwamgongo alipotembelea Hifadhi ya Taifa Gombe wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani Kigoma jana.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akizindua rasmi kituo cha utafiti wa Sokwe Mtu katika Hifadhi ya Taifa Gombe ambacho kimefadhiliwa na Taasisi ya Jane Goodal, alipotembelea hifadhi hiyo jana wakati wa ziara yake mkoani Kigoma.
  Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akikata keki kama ishara ya kuzindua hafla fupi ya kuadhimisha miaka 50 toka kuanzishwa kwa Hifadhi ya Taifa Gombe alipotembelea hifadhi hiyo jana wakati wa ziara yake mkoani Kigoma. Anaeshudia kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu, TANAPA, Nyamakumbati Mafuru na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi hiyo, Donatus Bayona.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiwa kwenye picha ya pamoja wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa Gombe katika Maporomoko ya Maji ya Kakombe alipotembelea hifadhi hiyo janawakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani Kigoma jana.

Sunday, July 22, 2018

WAZIRI KIGWANGALLA AAGIZA UJENZI WA VIWANDA VIDOGO VYA ASALI KWA WILAYA ZOTE ZA MIKOA YA TABORA NA KATAVI

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Skonge, Peres Magiri kukagua eneo la mradi wa umwagiliaji wa Ulua ambao ulijengwa kimakosa ndani ya eneo la Hifadhi ya Msitu wa Ipembampazi wakati wa ziara yake wilayani humo jana. Ameigiza Halmashauri ya wilaya hiyo kukamilisha taratibu za Tathmini ya Athari za Kimazingira (EIA) ili Serikali ifanye uamuzi wa kuendelea au kusitisha mradi huo. Wengine kwenye msafara huo ni Naibu Waziri wa TAMISEMI na Mbunge wa Skonge, Joseph Kakunda (wa nne pichani ).

.............................................................

*Ahamasisha kilimo cha Korosho kama zao mbadala la kuinua uchumi na uhifadhi wa mazingira

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla ameuagiza Mfuko wa Ruzuku wa Misitu Tanzania (TAFF) kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kuanzisha mradi wa viwanda vidogo vya kusindika na kufungasha asali katika mikoa ya Tabora na Katavi ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo na kujenga uchumi wa viwanda.

Ametoa agizo hilo jana kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Mtakuja wilaya ya Skonge mkoani humo ikiwa ni muendelezo wa ziara zake mikoani kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi na kutatua changamoto zake.

Alisema kwa kiwango kikubwa wananchi wa mikoa hiyo wamekuwa wategemezi kwenye zao moja tu la tumbaku ambalo sio rafiki kwa mazingira kwakuwa miti mingi hukatwa kwa ajili ya kukausha zao hilo jambo ambalo ni muhimu sasa kuwekeza zaidi kwenye mazao mengine ikiwemo viwanda vya kusindika na kufungasha asali ili kuongeza uzalishaji, ubora na hatimaye kuongeza kipato na faida zaidi.

"Mwaka huu ule mfuko wa misitu, kwa kiasi kikubwa tuamue tuwekeze ukanda huu wa magharibi  ambapo kuna zaidi ya asilimia 60 ya misitu yote hapa nchini, na tuanze kwa kujenga kiwanda kimoja katika kila wilaya, ikiwemo Nzega, Skonge, Uyui, Tanganyika, Mlele, Mpanda na Kaliua.

"Tuwawezeshe wananchi wajiunge katika vikundi, tuwagawie mizinga ya kisasa, wafuge nyuki kisasa, warine asali kisasa, wakisharina wapeleke kwenye viwanda, ifungashwe kisasa, ipate bei kubwa, na mwisho wa siku wataona faida ya kuwa na misitu.

"Hapo tutakuwa tumewasaidia, watapa kipato mbadala lakini watakua wakali sana kwa watu wanaoharibu misitu na tutatengeneza jeshi kubwa la wananchi la ulinzi wa misitu yetu, hivyo nataka mradi huu uanze mara moja bila kusuasua ili na sisi tuchangie jitihada za Serikali ya awamu ya tano katika ujenzi wa uchumi wa viwanda. " alisema Dk. Kigwangalla.

Wakati huo huo, Waziri Kigwangalla amewashauri wananchi wa mikoa hiyo kuanzisha kilimo cha korosho kama zao jingine mbadala la kuongeza kipato na kunusuru misitu badala ya kujikita kwenye zao moja la tumbaku ambalo ni chanzo kikubwa cha uharibifu wa misitu ya mikoa hiyo.

Amesema ni muhimu walau kwa kila kaya moja kuanza kwa kupanda ekari moja ya mikorosho ili kuongeza zao jingine mbadala la biashara ambalo lina tija zaidi kiuchumi na kiuhifadhi wa mazingira. 

"Kilimo cha tumbaku sio rafiki kwa mazingira tumejaribu kuleta mabani banifu yanayotumia kuni chache,  tumejaribu kuwashawishi wananchi wapande miti lakini tumechemsha, miti mingi imeendelea kukatwa misitu nayo inateketea siku hadi siku, ni lazima tutafute mbinu mbadala ya kukabiliana na changamoto hii, na hii ni kupitia zao hili la korosho" alisema Dk. Kigwangalla.

Amesema tafiti zinaonyesha kuwa zao la korosho katika mikoa hiyo lina uwezo wa kustawi zaidi na kuzalisha mara mbili kuliko mikoa ya kusini ambayo inasifika zaidi kwa uzalishaji huo hapa nchini.

Aidha ameziagiza halmashauri zote za mikoa hiyo kufanya utaratibu wa kupata mbegu na miche ya zao hilo mapema iwezekanavyo kwa ajili ya kuwagawia wananchi kabla ya msimu wa mvua kuanza na wataalamu wa kilimo wawaelimishe wananchi njia bora ya kupanda na kutunza miche hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Skonge, Peres Magiri alisema kiwango cha mvua kwa mwaka katika wilaya hiyo kimeshuka na kufikia 600mm kutokana na mabadiliko ya tabia nchi na uharibifu wa mazingira. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Skonge, Peres Magiri kukagua eneo la mradi wa umwagiliaji wa Ulua ambao ulijengwa kimakosa ndani ya eneo la Hifadhi ya Msitu wa Ipembampazi wakati wa ziara yake wilayani humo jana. Ameigiza Halmashauri ya wilaya hiyo kukamilisha taratibu za Tathmini ya Athari za Kimazingira (EIA) ili Serikali ifanye uamuzi wa kuendelea au kusitisha mradi huo. Wengine pichani ni Naibu Waziri wa TAMISEMI na Mbunge wa Skonge, Joseph Kakunda (wa nne).
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akipiga jaramba alipokuwa akikagua  eneo la mradi wa umwagiliaji wa Ulua ambao ulijengwa kimakosa ndani ya eneo la Hifadhi ya Msitu wa Ipembampazi wakati wa ziara yake wilayani Skonge jana. Anayefuata ni Naibu Waziri TAMISEMI na Mbunge wa Skonge, Joseph Kakunda, Mkuu wa Wilaya ya Skonge, Peres Magiri na viongozi wengine wa wilaya hiyo. Ameiagiza Halmashauri ya wilaya hiyo kukamilisha taratibu za Tathmini ya Athari za Kimazingira ili Serikali ifanye uamuzi wa kuendelea au kusitisha mradi huo.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akipiga jaramba alipokuwa akikagua  eneo la mradi wa umwagiliaji wa Ulua ambao ulijengwa kimakosa ndani ya eneo la Hifadhi ya Msitu wa Ipembampazi wakati wa ziara yake wilayani Skonge jana. Kulia ni Naibu Waziri TAMISEMI na Mbunge wa Skonge, Joseph Kakunda. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akiongoza kupiga jaramba alipokuwa akikagua  eneo la mradi wa umwagiliaji wa Ulua ambao ulijengwa kimakosa ndani ya eneo la Hifadhi ya Msitu wa Ipembampazi wakati wa ziara yake wilayani Skonge jana. Wengine pichani ni Naibu Waziri TAMISEMI na Mbunge wa Skonge, Joseph Kakunda (Nyuma Katikati). Ameiagiza Halmashauri ya wilaya hiyo kukamilisha taratibu za Tathmini ya Athari za Kimazingira ili Serikali ifanye uamuzi wa kuendelea au kusitisha mradi huo.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akikagua eneo la mradi wa umwagiliaji wa Ulua ambao ulijengwa kimakosa ndani ya eneo la Hifadhi ya Msitu wa Ipembampazi wakati wa ziara yake wilayani humo jana. Kulia kwake Mkuu wa Wilaya ya Skonge, Peres Magiri na Naibu Waziri TAMISEMI na Mbunge wa Skonge, Joseph Kakunda (wa pili kulia). Ameigiza Halmashauri ya wilaya hiyo kukamilisha taratibu za Tathmini ya Athari za Kimazingira ili Serikali ifanye uamuzi wa kuendelea au kusitisha mradi huo.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akikagua eneo la mradi wa umwagiliaji wa Ulua ambao ulijengwa kimakosa ndani ya eneo la Hifadhi ya Msitu wa Ipembampazi wakati wa ziara yake wilayani humo jana. Anayefuata ni Mkuu wa Wilaya ya Skonge, Peres Magiri, Kaimu Mkurugenzi Mkuu TAWA, Mabula Misungwi, Naibu Waziri TAMISEMI na Mbunge wa Skonge, Joseph Kakunda na viongozi wengine wa wilaya hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akikagua eneo la mradi wa umwagiliaji wa Ulua ambao ulijengwa kimakosa ndani ya eneo la Hifadhi ya Msitu wa Ipembampazi wakati wa ziara yake wilayani humo jana. Anayefuata ni Mkuu wa Wilaya ya Skonge, Peres Magiri, Kaimu Mkurugenzi Mkuu TAWA, Mabula Misungwi, Naibu Waziri TAMISEMI na Mbunge wa Skonge, Joseph Kakunda na viongozi wengine wa wilaya hiyo.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akizungumza na uongozi wa wilaya ya Skonge wakati wa ziara yake wilayani humo jana.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mtakuja katika wilaya ya Skonge mkoani Tabora baada ya kukagua eneo la mradi wa umwagiliaji wa Ulua ambao ulijengwa kimakosa ndani ya eneo la Hifadhi ya Msitu wa Ipembampazi wakati wa ziara yake wilayani humo jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mtakuja katika wilaya ya Skonge mkoani Tabora baada ya kukagua eneo la mradi wa umwagiliaji wa Ulua ambao ulijengwa kimakosa ndani ya eneo la Hifadhi ya Msitu wa Ipembampazi wakati wa ziara yake wilayani humo jana.

Friday, July 20, 2018

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, DK. HAMISI KIGWANGALLA ATEMBELEA PORI LA AKIBA MASWA

 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiangalia mandhari ya Pori la Akiba Maswa lililopo wilaya ya Meatu mkoani Simiyu wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani humo jana. Kushoto ni Mkuu wa Kanda wa Kikosi Dhidi ya Ujangili (KDU) Kanda ya Serengeti, Johnson Msella.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiangalia akioneshwa ramani ya Pori la Akiba Maswa na Meneja wa pori hilo, Lusajo Masinde (kushoto kwake) wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi katika wilaya ya Meatu mkoani Simiyu jana. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua moja ya eneo la "camp" ya kitalii katika Pori la Akiba Maswa wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi katika wilaya ya Meatu mkoani Simiyu jana. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua  mandhari ya Pori la Akiba Maswa lililopo wilaya ya Meatu mkoani Simiyu wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani humo jana. 
 Muonekano wa baadhi ya twiga katika Pori la Akiba Maswa wakati wa ziara ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla katika pori hilo jana.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiangalia mandhari ya Pori la Akiba Maswa lililopo wilaya ya Meatu mkoani Simiyu wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani humo jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiangalia mandhari ya Pori la Akiba Maswa lililopo wilaya ya Meatu mkoani Simiyu wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani humo jana. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla, viongozi wa Pori la Akiba Maswa na Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Makao wakiangalia mandhari ya Pori la Akiba Maswa lililopo wilaya ya Meatu mkoani Simiyu wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani humo jana. (Picha zote na Hamza Temba- Wizara ya Maliasili na Utalii)

AGIZO ALILOTOA WAZIRI KIGWANGALLA MKOANI SIMIYU, LIPO LA KUMTAKA MUWEKEZAJI KUSALIMISHA HATI YA KIWANJA



Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla ametoa miezi mitatu kwa muwekezaji wa hoteli ya kitalii ya Kijereshi Tented Camp kurudisha kwa Kamishna wa Ardhi hati miliki ya kipande cha ardhi chenye ukubwa wa hecta 464 kilichopo ndani ya pori hilo kwakuwa ni batili.
Aidha, amewapa siku 45 wananchi wanaoishi kinyume cha Sheria ndani ya eneo la kinga (bufer zone) za Pori la Akiba Kijereshi kuondoka kwa hiari yao wenyewe kabla ya kuanza operesheni ya kuwaondoa kwa nguvu.

Thursday, July 19, 2018

WAZIRI KIGWANGALLA AWAPA NOTISI YA SIKU 45 WALIOVAMIA PORI LA AKIBA KIJERESHI

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa mipaka ya Pori la Akiba Kijereshi na Meneja wa pori hilo, Dianna Chambi alipotembelea pori hilo jana kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi katika wilaya ya Busega mkoani Simiyu. Alitoa siku 45 kwa wananchi wote waliovamia kingo/bafa za hifadhi hiyo kuondoka kwa hiari yao. Kulia ni Mkuu wa Kanda wa Kikosi Dhidi ya Ujangili (KDU) Kanda ya Serengeti, Johnson Msella.

Na Hamza Temba-Simiyu
.........................................................

*Atoa miezi mitatu kwa Muwekezaji kurudisha Serikalini hati miliki ya kipande cha ardhi kilichopo ndani ya Pori hilo

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla amewapa siku 45 wananchi wanaoishi kinyume cha Sheria ndani ya kingo (bufer zone) za Pori la Akiba Kijereshi kuondoka kwa hiari yao wenyewe kabla ya kuanza operesheni ya kuwaondoa kwa nguvu. 

Ametoa agizo hilo jana alipotembelea pori hilo katika wilaya ya Busega mkoani Simiyu ikiwa ni muendelezo wa ziara zake mikoani kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi na kutatua changamoto zake.

Baada ya kushuhudia makazi na shughuli nyingine za kibinadam ndani ya pori hilo, Dk. Kigwangalla aliamua kutoa agizo hilo na kusema kuwa sheria za uhifadhi wa wanyamapori haziruhusu vitendo hivyo ndani ya maeneo yaliyohifadhiwa kisheria pamoja na kingo zake (buffer zone) ambazo ni mita 500 kutoka kwenye mpaka halisi wa eneo la hifadhi.

"Mpaka itakapofika tarehe 31 mwezi ujao (Septemba) wananchi wote hawa wawe wameshaondoka eneo hili kwa hiari yao wenyewe, muwatangazie na mpime eneo hili vizuri muweke alama ili wajue ni wapi wanatakiwa kuondoka.

"Na ikifika tarehe 1 Septemba kama kuna watakaokuwa wamekaidi agizo hili, basi mfanye oparesheni maalum muwaondoe na msafishe kila kitu, ni lazima ifike mahali kila mmoja aheshimu sheria za nchi" alisema Dk. Kigwangalla kuuagiza uongozi wa pori hilo.

Wakati huo huo, Waziri Kigwangalla ametoa miezi mitatu kwa muwekezaji wa hoteli ya kitalii ya Kijereshi Tented Camp kurudisha kwa Kamishna wa Ardhi hati miliki ya kipande cha ardhi chenye ukubwa wa hecta 464 kilichopo ndani ya pori hilo kwakuwa ni batili.

Aimesema pori hilo lilianzishwa mwaka 1994 wakati muwekezaji huyo anadai kumilikishwa eneo hilo mwaka 1995 jambo ambalo haliwezekani mtu binafsi kupewa hati ya kumiliki eneo lililopo ndani ya eneo jingine tena hifadhi.

Aidha, amemtaka pia muwekezaji huyo kuheshimu sheria na taratibu za uwekezaji katika eneo hilo ikiwemo kulipa ada na tozo mbalimbali.
 
Pori la Akiba Kijereshi lenye ukubwa wa kilomita za mraba 65.72 linasimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA na lilipandishwa hadhi kuwa Pori la Akiba mwaka 1994 kwa Tangazo la Serikali Na. 215 la terehe 10 Juni, 1994 na hiyo ni kutokana na umuhimu wake kiuchumi na kiikolojia hususan katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. 
 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akitoa maelekezo kwa Meneja wa Pori la Akiba Kijereshi, Dianna Chambi (wa pili) kuhusu wananchi waliovamia hifadhi hiyo alipotembelea pori hilo jana kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi katika wilaya ya Busega mkoani Simiyu.  
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua eneo la hoteli ya kitalii ya Kijereshi Tented Camp iliyopo ndani ya Pori la Akiba Kijereshi alipotembelea pori hilo jana kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi katika wilaya ya Busega mkoani Simiyu, ametoa miezi mitatu kwa mmiliki wa hoteli hiyo kurudisha hati miliki ya kiwanja chenye hekta 464 kilichopo ndani ya pori ya pori hilo kwa kamishna wa ardhi kwakuwa ni batili na aendelee kutoa huduma kwa kuzingatia sheria na taraibu za uwekezaji.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akifungua koki ya maji katika eneo la hoteli ya kitalii ya Kijereshi Tented Camp iliyopo ndani ya Pori la Akiba Kijereshi alipotembelea pori hilo jana kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi katika wilaya ya Busega mkoani Simiyu, ametoa miezi mitatu kwa mmiliki wa hoteli hiyo kurudisha hati miliki ya kiwanja chenye hekta 464 kilichopo ndani ya pori hilo kwa kamishna wa ardhi kwakuwa ni batili na aendelee kutoa huduma kwa kuzingatia sheria na taraibu za uwekezaji. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wananchi wa kijiji cha Logolambogo katika wilaya ya Itilima mkoani Simiyu alipolitembelea Pori la Akiba Maswa jana kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi na kutatua changamoto zake. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wananchi wa kijiji cha Logolambogo katika wilaya ya Itilima mkoani Simiyu alipolitembelea Pori la Akiba Maswa jana kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi na kutatua changamoto zake. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wananchi wa kijiji cha Logolambogo katika wilaya ya Itilima mkoani Simiyu alipolitembelea Pori la Akiba Maswa jana kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi na kutatua changamoto zake. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wananchi wa kijiji cha Logolambogo katika wilaya ya Itilima mkoani Simiyu alipolitembelea Pori la Akiba Maswa jana kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi na kutatua changamoto zake. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka alipowasili mkoani humo jana kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja ya kukagua shughuli za uhifadhi na kutatua changamoto zake.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua moja ya eneo la kingo/bafa la Pori la Akiba Maswa ambalo limevamiwa na wananchi kwa ajili ya shughuli kilimo alipolitembelea pori hilo jana kwa ajili ya kukagua shughuli za uhifadhi katika wilaya ya Itilima mkoani Simiyu. Kulia kwake ni Mbunge wa Itilima, Njaru Silanga na Meneja wa Pori hilo, Lusajo Masinde.