slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Friday, December 29, 2017

SERIKALI YASIKIA KILIO CHA WADAU WA SEKTA YA UWINDAJI WA KITALII NCHINI, YAONGEZEA MIAKA MIWILI YA UMILIKI WA LESENI ZA VITALU

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara yake mjini Dodoma jana kwa ajili ya kujadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta hiyo ikiwemo utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuanzisha utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mej. Jen. Gaudence Milanzi na Naibu Katibu Mkuu, Dk. Aloyce Nzuki (kulia).  

Na Hamza Temba, Dodoma
...............................................................
Serikali imesikia kilio cha wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii nchini na kuamua kuongeza muda wa miaka miwili ya umiliki wa leseni za vitalu 95 vya uwindaji wa kitalii ambazo zilikuwa ziishe muda wake tarehe 31 Desemba mwaka huu (2017).

Uamuzi huo umefikiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla wakati wa kikao cha majumuisho na watendaji wa Wizara hiyo muda mfupi baada ya kumalizika kwa mkuano wa wadau wa sekta hiyo ulioandaliwa na Wizara hiyo mjini Dodoma jana.

Akizungumzia uamuzi huo Dk. Kigwangalla alisema, lengo ni kuwapa muda wawekezaji hao ili waweze kujiandaa na mabadiliko ya mfumo mpya wa utowaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada ikiwemo kurudisha baadhi ya gharama za uwekezaji walizoweka katika vitalu hivyo.

Awali akizungumza katika mkutano huo wa wadau Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Kampuni za Uwindaji wa Kitalii nchini, Michael Mantheakis alimuomba Waziri Kigwangalla kuwaongezea muda wa umiliki wa leseni zao kuanzia miaka mitano au mitatu na nusu ili waweze kurudisha gharama za uwekezaji walizowekeza katika vitalu hivyo ikiwemo ujenzi wa miundombinu, makambi na vifaa vyake pamoja na maji.

Hata hivyo, Waziri Kigwangalla aliweka wazi msimamo wa Serikali wa kutimiza azma yake ya kuingia kwenye utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada na kusema kuwa kamwe haitorudi nyuma na kwamba utekelezaji wa zoezi hilo hauwezi kusubiri muda mrefu kiasi hicho.

Akizungumzia kuhusu hatua ya utekelezaji wa utaratibu huo, Waziri Kigwangalla alisema kwa sasa taratibu za kuandaa Sheria za usimamizi zinaendelea na zinatarajiwa kukamilika mwezi Februari 2018 pamoja na kanuni zake zinazotarajiwa kukamilika mwezi Aprili 2018.

Aidha, alisema mfumo maalumu wa kielektroniki unaandaliwa ambapo maombi yote ya leseni za umiliki wa vitalu vya uwindaji kwa njia ya mnada yatafanyika kwa uwazi kwa njia ya mtandao.

Alisema baada ya kukamilika kwa taratibu zote na mfumo huo mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada na maombi kuwasilishwa, mnada wa kwanza utaanza tarehe 1 Julai, 2018 kwa kuanza kunadi vitalu 61 ambavyo kwa sasa havina wawekezaji.

Mnada wa pili utafanyika mwaka 2020 baada ya kuisha kwa muda huo wa nyongeza wa miaka miwili ukihusisha vitalu 95 vilivyoongezewa muda wa umiliki wa leseni pamoja na vitalu vingine endapo vitabaki katika mnada huo wa kwanza kwa sababu mbalimbali.

Alisema sheria na kanuni zinazoandaliwa hivi sasa zitazingatia mambo muhimu ikiwemo kuwapa nafasi watanzania wenye mitaji midogo kuweza kuingia kwenye biashara hiyo pamoja na kuweka adhabu kali dhidi ya wafanyabiashara watakaohujumu biashara hiyo kwa makusudi.

Mkutano huo wa siku moja ulihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi, Naibu Katibu Mkuu, Dk. Aloyce Nzuki, wakurugenzi, wakuu wa vitengo na wakuu wa taasisi zilizopo chini ya wizara hiyo na waandhishi wa habari.

Oktoba 22 mwaka huu (2017) wakati akiongoza kikao cha wadau wa sekta ya Maliasili na Utalii mjini Dodoma, Waziri Kigwangalla alitangaza kufuta leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii zilizokuwa zianze mwezi Januari, 2018 ili kupisha utarartibu mpya wa utoaji wa leseni hizo kwa njia ya mnada ikiwa ni mkakati wa Serikali wa kuimarisha sekta hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara yake mjini Dodoma jana kwa ajili ya kujadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta hiyo ikiwemo utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuanzisha utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Dk. Aloyce Nzuki.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla.
Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Kampuni za Uwindaji wa Kitalii nchini, Michael Mantheakis (kulia) akiwasilisha mapendekezo yake katika mkutano wa wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii mjini Dodoma jana kwa ajili ya kujadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta hiyo ikiwemo utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuanzisha utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada.
Mdau wa sekta ya uwindaji wa kitalii, Dk. Licky Abdallah akizungumza katika mkutano huo. 
Mdau wa sekta ya uwindaji wa kitalii ambaye pia ni mmilikia wa kampuni ya uwindaji wa kitalii ya Bushman Hunting Safaris, Talal Abood akiwasilisha mapendekezo yake katika mkutano huo. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akisikiliza kwa makini mapendekezo ya wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara yake mjini Dodoma jana. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi.
Baadhi ya wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii wakiwa katika mkutano huo. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii katika mkutano uliondaliwa na Wizara yake mjini Dodoma jana kwa ajili ya kujadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha sekta hiyo ikiwemo utekelezaji wa azma ya Serikali ya kuanzisha utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada. Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mej. Jen. Gaudence Milanzi na Naibu Katibu Mkuu, Dk. Aloyce Nzuki (kushoto kwake). 
Baadhi ya watendaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii na Taasisi zake wakiwa katika mkutano huo. 

Friday, December 22, 2017

Wizara ya Maliasili yatoa miche laki moja katika Kampeni ya Kuufanya Mji wa Dodoma kuwa Kijani

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania- TFS, Prof. Dos Santos Silayo (kushoto) kuhusu utaratibu wa kupanda mti wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuufanya mji wa Dodoma kuwa wa Kijani iliyofanyika kwenye chanzo cha maji bonde la Makutupora, Mjini Dodoma Desemba 21, 2017.

Kupitia TFS, Waziri Kigwangalla aliahidi kutoa miche ya miti laki moja kwa manispaa ya Dodoma na miche mingine 650,000 kwa wilaya zote za Mkoa wa Dodoma.

Dk. Hamisi Kigwangalla ameteua wajumbe wengine wa Kamati ya Kuandaa Maadhimisho ya Mwezi Maalum wa Urithi wa Tanzania.


Tuesday, December 19, 2017

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla atengua uteuzi wa wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.


STATEMENT OF THE HIGH COMMISSION OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA ON ALLEGATIONS RELATING TO POACHING IN THE RUAHA NATIONAL PARK AND ADJACENT GAME RESERVES


STATEMENT OF THE HIGH COMMISSION OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA ON ALLEGATIONS RELATING TO POACHING IN THE RUAHA NATIONAL PARK AND ADJACENT GAME RESERVES

General
This statement relates to a letter received at the High Commission from ITV News on 13.12.2017. The letter informed that ITV News was going to broadcast a report on 18.12.2017 relating to poaching in the Ruaha National Park and adjacent game reserves. The letter said that in compiling its report ITV News had  “spoken to a number of people including Dr. Colin Beale who has researched this issue on behalf of TAWIRI” and that the allegations  “are supported by research and by interviews with credible sources”.

We are unable to comment on the people interviewed since we do not know who they are as yet – but we can confirm that key people in the ministry responsible for natural resources in Tanzania, such as the Minister, Permanent Secretary or relevant Directorates and others who would have given valuable information on the matter were not interviewed by ITV News.

As regards Dr. Colin Beale, we value his expertise in spatial statistical analysis but we are not aware of the research he is said to have done on behalf of TAWIRI. We know, however, that TAWIRI conducted censuses for three years consecutively from 2013-2015. In that exercise TAWIRI did, amongst other activities, undertake aerial surveys whereby Dr. Beale was invited at the end of the censuses for spatial statistical analyses. The analyses started in mid-2016 running into 2017.

Like many other countries in the East African region, Tanzania has been affected by elephant poaching and also by illegal wildlife trade.  In the years mentioned TAWIRI conducted the censuses both as part of its monitoring mandate as well as to scientifically check trends in poaching. This has been a serious concern since the early 2010s when it was observed that the elephant population in the country had dramatically declined. While poaching has always been one of the government’s serious concerns, the 2013-2015 censuses exercise was not driven by any assumption that there was collusion between our game rangers and poachers or illegal wildlife traders.

Major Findings of the Spatial Analyses from the Censuses

1.      Aerial surveys observed that many elephant carcasses were located close to water holes indicating that they were specifically targeted as they came to drink water.
2.      About 15 ranger posts were surveyed. Out of these the survey observed that in three posts an unusually high number of carcasses were found fairly close - technically meaning within a radius of up to about ten kilometers.
3.      More elephants were killed during the wet season when travel by road is difficult. The Ruaha-Rungwa ecosystem has an area of over 50,000 square kilometers of predominantly woodlands. These areas are largely patrolled by car with foot patrols done as circumstances permit.

Allegations

1.      That an unknown number of rangers in the national park were complicit in the illegal wildlife trade in that they passed information to poachers and co-operated with them in other ways.
2.      That a small number of rangers in the national park may have been directly involved in poaching themselves.
3.      That an unusually high number of elephant carcasses were found in close proximity to some ranger posts.
4.      That these activities occurred under the watch of the SPANEST program which was partly funded by UNDP and GEF and which trained, equipped and otherwise supported the rangers in Ruaha at that time.

Comments/Observations

            The TAWIRI census exercise did indeed establish a sharp decline in the population of elephants in the Ruaha-Rungwa ecosystem in the three years mentioned. In 2013, for instance, there was an estimation of 20,090 elephants while  in 2014 they were estimated at only 8,272.  A slightly higher number was recorded in 2015 with 15,836 elephants. Standard sampling showed that in 2013 the number of elephant carcasses estimated from an aerial survey was 3,496 in 2013; 3,296 in 2014 and 2,863 in 2,863. In the absence of a major disease outbreak one may assume that this trend was due to human activity - poaching for illegal wildlife trade.
             
            For allegations 1 and 2 - whether this particular development in the Ruaha-Rungwa ecosystem was a result of game rangers’ involvement in poaching or illegal wildlife trade is not something that the Ministry or TAWIRI can confidently attest to. But it is obvious that in a basket of fish there could be one or two bad ones – however this should not be taken as an institutionalized system that operated with the tacit knowledge of the authorities.
             
For allegation 3  - that an unusually high number of carcasses were found around some ranger posts. This was in fact one of the findings from the TAWIRI conducted aerial survey. That the carcasses were within close proximity of the ranger posts could lead one to assume that there was collusion between the game rangers and poachers.  This is a possibility  - but there could be other factors too. It is well known, for example, that ecologically the concentration of carcasses can be attributed to activity pattern, habitat selection and availability of drinking water. The three ranger posts where large numbers of carcasses were found are close to the main perennial source of water, the Great Ruaha River, and also adjacent to community areas. Records have shown high concentration of elephants and other species in these areas. And the fact is, when animals, particularly elephants, are wounded in community Wildlife Management Areas (WMAs) that are close to the park, they tend to take refuge back in the park. Some of these would die in areas along the river and close to the ranger posts – explaining for the high number of carcasses there. In the absence of any one known single cause it is our view the presence of an unusually high number of carcasses around these posts is an issue for further investigation.

For allegation 4 - the project on Strengthening Protected Areas Network in Southern Tanzania  - SPANEST – the Ministry acknowledges the valuable support extended to our country under SPANEST. It should be remembered, nonetheless, that this project commenced in 2013 just at the time that TAWIRI had started conducting the censuses, and it did in fact help support the 2013 one. It should also be mentioned that training, capacity building and other kind of support rendered was a process that could not necessarily lead to immediate success. In the course of time the project proved to be very useful and our game rangers have progressively continued to improve their skills, work capacity and ethics with a clearly positive impact on the fight against poaching and illegal wildlife trade. This is evidenced by a remarkable decline in the number of fresh elephant killings. Statistics show that the number of elephants killed has dropped from 92 in 2012 to 18 in 2016. In this period there has been no recorded cases in the national parks with only occasional incidents in game reserves.

Government Efforts

The government has been taking the issue of poaching very seriously. With the alarming downward trend of the early 2000s when Tanzania had over 120, 000 to only about 50,000 in 2015, the government could not have afforded any complacency. Between 2010 and 2015 the government conducted three major operations that showed reasonably satisfactory results in terms of arresting poaching trends, protecting the elephants and developing more integrated and robust strategies.

Conclusion

The Ministry and the government as a whole welcomes any credible study or research that will help to show the magnitude of the huge challenge of elephant poaching and illegal wildlife trade. We will follow with keen interest the report that ITV News intends to broadcast on 18.12.2017. We believe elephant protection and stopping illegal wildlife trade is not only in the interest of Tanzania but the world at large.

____________________________________________________


THE HIGH COMMISSION OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
London, 17.12.2017

Sunday, December 17, 2017

DK. KIGWANGALLA AFUNGA MAFUNZO YA 15 YA JESHI USU KWA MAAFISA WANYAMAPORI WA TAWA, TANAPA NA NGORONGORO MKOANI KATAVI


Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiwaongoza Maafisa wa Wanyamapori 87 wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania– TAWA, Shirika la Hifadhi za Taifa – TANAPA na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro kupiga gwaride la ukakamavu muda mfupi baada ya kuwatunuku vyeti vya kuhitimu mafunzo ya Jeshi Usu jana katika kituo cha Mlele mkoani Katavi. 

Na Hamza Temba-  Mlele, Katavi
...........................................................................

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla amewaagiza wahifadhi wote nchini kushirikiana na wadau wengine hasa mamlaka za Mikoa na Wilaya katika maeneo yenye uvamizi wa mifugo na migogoro ya mipaka ya hifadhi ili kutatua changamoto hizo kwa namna shirikishi ikiwa ni pamoja na kuimarisha utoaji wa elimu kwa wananchi wanaozunguka maeneo hayo.

Ametoa agizo hilo jana Disemba, 16, 2017 katika Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wakati akifunga mafunzo ya 15 ya mabadiliko ya kuelekea mfumo wa Jeshi Usu kwa Maafisa wa Wanyamapori 87 wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania– TAWA, Shirika la Hifadhi za Taifa – TANAPA na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro.

“Kazi ya ulinzi wa rasilimali zetu za asili ni yetu na tutaiendeleza, Falsafa yetu ni kuwashirikisha wadau wote, kama kuna taasisi za kiraia kwenye eneo lako la kazi, taasisi za kijamii, mamlaka za mikoa na wilaya, wananchi, halmashauri husika mshirikiane nao ili kupunguza madhara ya operesheni zetu, na zoezi hili la uhifadhi liwe endelevu,” alisema Dk. Kigwangalla.

Aidha, alitoa wito kwa wananchi wote kuendelea kuheshimu Sheria za nchi na kuacha kufanya shughuli za kibinadamu kwenye maeneo ya hifadhi ikiwemo kuingiza mifugo, kuanzisha kilimo, makazi na ukataji wa miti kwa ajili ya kuchoma mkaa na matumizi mengineyo.

Awali akizungumzia mafunzo hayo alisema, lengo ni kubadilisha utendaji katika sekta ya uhifadhi kutoka ule wa kiraia kwenda wa jeshi usu ambao utaongeza nidhamu, uwajibikaji, uadilifu na maadili kwa watumishi wote wa sekta hiyo ili waweze kusimamia ipasavyo uhifadhi endelevu wa maliasili za taifa.

Alisema katika kuelekea mfumo huo, Jeshi hilo litakuwa moja bila kubagua taasisi yeyote ambayo ipo chini ya Wizara yake. “Sheria ya Wanyamapori namba 5 ya mwaka 2009 inampa Waziri mamlaka ya kuunda Jeshi Usu, haikusema jeshi la TAWA, TFS, TANAPA au NGORONGORO na kwa vile hili jeshi ni langu nataka liwe moja, na tunakimbiza mchakato huu kwa haraka ukamilike kwa mujibu wa Sheria.

“Tunafarajika Mhe. Rais ameshaunga mkono na ameshatupa maelekezo, Mwenyekiti wa Kamati ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama ambaye ni Mkuu wa Jeshi la Ulinzi naye ameshasaini, ni sisi sasa tuendelee kujipanga vizuri ndani ya wizara, tuanze kuishi kwenye mfumo huo, kuanzia kwenye sare, uratibu wa mafunzo, uongozi na mfumo wa utawala,” alisema Dk. Kigwangalla.

Alisema mfumo huo wa Jeshi Usu utakuwa na mnyororo mmoja wa mamlaka (chain of comand) na kwamba utahusisha taasisi zote za uhifadhi zilizopo chini ya wizara yake kwenye sekta ya wanyamapori, misitu na mali kale. “Sijawaona watu wa misitu hapa au mambo ya kale, wote hawa ni ni muhimu, rasilimali za mali kale nazo ni muhimu sana kulindwa kwani zikiharibika hazitengenezeki tena” alisema.

Katika hatua nyingine amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuhakikisha kuwa mafunzo yote ya Jeshi Usu ambayo yanaendelea katika kituo cha Mlele, Mkoani Katavi yanaratibiwa moja kwa moja na Wizara tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo uratibu unafanywa na taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo.

Akizungumzia mafanikio ya vita dhidi ya ujangili na matunda ya mafunzo hayo alisema, “Katika siku za hivi karibuni tumepiga hatua kubwa ya kupambana na ujangili hasa wa tembo, Kwa dhati napongeza jitihada zinazofanywa na zinazoendelea kufanywa na wahifadhi, maaskari watumishi wengine na wadau wetu wote kwa ujumla ambazo zimeimarisha hali ya uhifadhi wa maliasili zetu”. 

Alisema kwa kiasi kikubwa matukio ya ujangili yamepungua na kwamba nyara nyingi zinazokamatwa katika kipindi hiki ni za zamani ambazo zilikuwa zimefichwa na majangili kwa ajili ya kuzitafutia masoko au kukimbia mikono ya sheria.

Alisema Wizara yake itaendelea kutumia mbinu za kisasa za kiitelijensia za kukabiliana na ujangili ikiwemo kutumia ndege zisizo na rubani kwa ajili ya doria na kuweka mifumo ya kisasa ya mawasiliano ambayo haitaweza kuingiliwa na majangili au watu wengine wenye nia ovu na uhifadhi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori wa Wizara hiyo, Dk. Nebo Mwina akitoa nasaha zake kwa wahitimu wa mafunzo hayo ya Jeshi Usu, aliwataka kuishi kwenye viapo vyao kwa kudumu katika ukakamavu, uhifadhi, maadili mema na nidhamu.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania – TAWA, Dk. James Wakibara aliwataka wahitimu hao kutumia mafunzo waliyopewa kufanya kazi kwa uaminifu na uadilifu kwa kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato ya Serikali, kujiepusha na rushwa na kudhibiti vitendo vya ujangili.

Mhifadhi Gloria Bidebeli kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania – TAWA akisoma risala ya wahitimu hao alisema mafunzo hayo yatawawezesha kuboresha ufanisi wa shughuli za uhifadhi kwa kutii amri na kutekeleza maagizo kwa wakati.

Mafunzo hayo ya wiki nne ambayo yalianza Novemba, 20 mwaka huu yalihusisha Mameneja wa Mapori ya Akiba na Tengefu 20, Wakuu wa Kanda wa Kikosi Dhidi ya Ujangili wanane, Maafisa Wanyamapori 29 kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania – TAWA, Wahifadhi Wanyamapori watano kutoka TANAPA na Wahifadhi Wanyamapori 26 kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro.

Mafunzo hayo yalihusisha matumizi sahihi ya silaha, mbinu mbalimbali za kupambana na uhalifu, huduma ya kwanza, ukakamavu, sheria mbalimbali zinazosimamia maliasili, ukamataji na upekuzi wa wahalifu na jinsi ya kuwafungulia hati za mashtaka.

Tangu kuanzishwa kwa mafunzo hayo Septemba 2015 jumla wahifadhi 1468 wakiwemo Askari wa Wanyamapori na Viongozi mbalimbali kutoka TAWA, TANAPA na NGORONGORO wameshapatiwa mafunzo hayo katika kituo hicho cha Mlele.  
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pili kushoto) akikagua gwaride la Maafisa wa Wanyamapori 87 wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania– TAWA, Shirika la Hifadhi za Taifa – TANAPA na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro muda mfupi kabla ya kuwatunuku vyeti vya kuhitimu mafunzo ya Jeshi Usu jana katika kituo cha Mlele mkoani Katavi. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na Maafisa wa Wanyamapori 87 wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania– TAWA, Shirika la Hifadhi za Taifa – TANAPA na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro muda mfupi kabla ya kuwatunuku vyeti vya kuhitimu mafunzo ya Jeshi Usu jana katika kituo cha Mlele mkoani Katavi. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza wakati wa kuhitimisha mafunzo hayo. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akiteta jambo na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania, Dk. James Wakibara wakati wa hafla hiyo. Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Rachel Kasanda. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akimkabidhi cheti mmoja ya wahitimu wa mafunzo ya Jeshi Usu kati ya Maafisa wa Wanyamapori 87 wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania– TAWA, Shirika la Hifadhi za Taifa – TANAPA na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro jana katika kituo cha Mlele mkoani Katavi.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania, Dk. James Wakibara akitoa nasaha zake kwa wahitimu wa mafunzo hayo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (katikati) akipokea salamu za Jeshi Usu wakati wa kuhitimisha mafunzo hayo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akipokea salamu za Jeshi Usu wakati wa kuhitimisha mafunzo hayo. Kulia ni Mkufunzi Mwandamizi wa Mafunzo hayo, Fidelis Kapalata.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pili kulia) akiangalia onesho la kulenga shabaha liliofanywa na Maafisa wa Wanyamapori 87 wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania– TAWA, Shirika la Hifadhi za Taifa – TANAPA na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro muda mfupi kabla ya kuwatunuku vyeti vya kuhitimu mafunzo ya Jeshi Usu jana katika kituo cha Mlele mkoani Katavi. Kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Rachel Kasanda na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania – TAWA, Dk. James Wakibara. 
Maonesho ya klenga shabaha.
Maonesho ya klenga shabaha.
Maonesho ya klenga shabaha.
Baadhi ya wahitimu wa mafunzo hayo.
Baadhi ya wahitimu wa mafunzo hayo.
Mhifadhi Gloria Bidebeli kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania – TAWA akisoma risala ya wahitimu hao.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiaga baada ya hafla hiyo.
Picha ya pamoja.
Picha ya pamoja.

Wednesday, December 13, 2017

WAZIRI KIGWANGALLA AFAFANUA KUHUSU KAMATI YA KITAIFA YA KUANDAA UTAMBULISHO WA TANZANIA


TAARIFA KUHUSU KAMATI YA UTAMBULISHO WA TANZANIA (DESTINATION TANZANIA BRANDING COMMITTEE)

Salaams, 

Siku chache zilizopita mimi, Hamisi Kigwangalla, katika kutekeleza 
majukumu yangu kama Waziri wa Maliasili na Utalii, niliteua kamati ya Kitaalamu ya watu waliobobea kwenye mambo ya ubunifu wa mikakati ya masoko, 
mawasiliano, mahusiano kwa umma, utalii na biashara. Lengo kuu likiwa kuanzisha mchakato
wa kitaalam (technical) wa kuandaa utambulisho mpya wa Tanzania kwenye masoko ya kimataifa ya Utalii. Kamati hii inakusudiwa kufanya uchambuzi wa kina wa tafiti mbalimbali na kukusanya maoni kwa wadau mbalimbali muhimu kisha kuniletea mapendekezo yao. 

Kwa kuzingatia ukweli kwamba, Maliasili na Utalii siyo Wizara ya Muungano na kwamba utalii, kimsingi ni katika mambo yatakayodumisha zaidi Muungano wetu na Umoja wetu, sababu kimkakati na kiutekelezaji hatuwezi kukwepana, na kwamba uuuzaji wa vivutio vya utalii ni katika mambo ya kufanywa kwa pamoja ili kuwa na tija kwa Taifa letu, nilipokea ushauri kwamba ni vema toka hatua za awali tuweke wajumbe wanaotokea Zanzibar, kwenye Kamati hii. 

Awali tulikuwa na fikra kwamba baada ya kazi za mwanzo kufanyika na kuwa na andiko la kitaalamu (technical proposal) la kufanyia kazi, tungeanzisha mawasiliano rasmi ndani ya Serikali zetu mbili, ambapo kungekuwa na majadiliano ngazi ya wataalam na baada ya hapo ngazi ya Mawaziri. Mpango huu bado tunao. 

Tumekuwa na utamaduni wa kufanya kazi pamoja na kwa ukaribu kwenye kutangaza vivutio vilivyopo sehemu zote mbili za Muungano na tutaendelea kufanya hivyo. Watalii wanaokuja kwenye mbuga hupenda kwenda Zanzibar kufanya utalii wa fukwe na wa kiutamaduni, na kinyume chake. Hivyo, hatuwezi kukwepa kufanya kazi pamoja.

Mimi binafsi ni muumin mkubwa na mahiri wa Muungano, na utangamano kwa ujumla wake. Pia ni muumin mkubwa wa ushirikishwaji kama zana muhimu ya kufanyia maamuzi nyeti, siwezi kuwa wa kwanza kukiuka msingi wa imani yangu kama kiongozi. Hatua stahiki itakapofika tutakaa na Waziri pacha wa Utalii wa Zanzibar kushauriana na kukubaliana. 

Dkt. Hamisi Kigwangalla, MB. 
WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII.

Sunday, December 10, 2017

DK. KIGWANGALLA - KILIO CHENU NIMEKISIKIA MIMI MWENYE MAMLAKA YA KUFANYA MABADILIKO, APONGEZWA NA WADAU WA UTALII


Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akizungumza na wadau wa utalii Jijini Arusha jana ambapo Wizara yake iliwasilisha mapendekezo ya viwango vipya vya leseni za biashara ya utalii na tozo ya ada za malazi katika viwango vya ubora wa nyota. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk. Aloyce Nzuki. 

Na Hamza Temba, Arusha
..............................................................
Wadau wa Utalii Jijini Arusha wamempongeza Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla kwa kukubali kuyafanyia kazi mapendekezo yao ya kuwaingiza wajasiriamali wadogo katika utoaji wa huduma za kusafirisha watalii nchini.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mwenyekiti wa Chama cha Waongoza Watalii Tanzania (TATO), Wilbard Chambulo wakati akichangia mapendekezo ya viwango vipya vya leseni za biashara ya utalii zilizowasilishwa kwao na Uongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii Jijini humo.

Chambulo alisema kwa muda mrefu sasa kanuni zinazotumika zinamtaka mfanyabiashara ya usafirishaji watalii awe na magari matatu kwa kiwango cha chini ikiwa ni pamoja na kulipia ada ya leseni ya Dola za Kimarekani 2,000 sawa na wafanyabiashara wengine matajiri jambo ambalo limekuwa likiwabagua wafanyabiashara wadogo.

“Tunakupongeza sana Mhe. Waziri kwa kutupa angalao hilo moja, tuliomba mwenye kagari kamoja nae aruhusiwe na apewe leseni walau ya dola 200 ili afanye biashara kidogo kidogo mwishowe atanunua gari tano na kuendelea, tunataka sisi Watanzania wote tufaidike na rasilimali zetu,” alisema Chambulo.

Awali akiwasilisha mapendekezo ya viwango hivyo vipya vya leseni ya biashara ya utalii, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Wizara ya Maliasili na Utalii, Deogratias Mdamu alisema kwa upande wa watanzania ambao ni wajasiriamali wadogo wenye gari moja hadi magari matatu watatakiwa kulipa ada ya leseni ya dola za Kimarekani 200.

Kwa upande wa wafanyabiashara wenye magari kuanzia manne hadi kumi alisema imependekezwa walipe Dola za Kimarekani 2,000, wenye magari 11 hadi 50 Dola za Kimarekani 3,000, magari 51 hadi 100 Dola za Kimarekani 10,000 na magari 100 na kuendelea Dola za Kimarekani 15,000.

Kwa upande wa wafanyabiashara ambao sio Watanzania wenye magari 10 hadi 30 imependekezwa walipe Dola za Kimarekani 10,000, magari 31 hadi 100 Dola za Kimarekani 15,000 na magari 101 na kuendelea Dola za Kimarekani 20,000.

Kwa upande wake Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla alisema lengo la kuwasilishwa kwa mapendekezo hayo ya viwango hivyo vipya vya leseni ya biashara ya utalii kwa wadau ni kuweka ushirikishwaji na makubaliano ya pamoja ya kutekeleza kanuni hizo.

Alisema sehemu kubwa ya mapendekezo hayo imezingatia maombi na maoni ya wadau hao ambayo yaliwasilishwa kwake awali. “Kilio chenu nimekisikia mimi mwenye mamlaka ya kufanya mabadiliko, lengo kubwa la mapendekezo haya ni kuwawezesha wajasiriamali wadogo wenye gari moja waweze kuingia kwenye biashara hii ya utalii pamoja na kuongeza mapato ya Serikali na jamii kwa ujumla,” alisema Dk. Kigwangalla.

Katika hatua nyingine amewaagiza watalaamu ndani ya Wizara yake kuhakikisha wanakamilisha kanuni hizo mpya ndani ya mwa mwaka huu ili utekelezaji wake uanze mapema mwakani, 2018.

Akizungumzia wafanyabiashara wanaofanya biashara ya kuwasafirisha watalii nyuma ya pazia bila kulipia leseni, alisema Wizara yake inaandaa mfumo maalumu wa kielektroniki utakaowezesha ukaguzi wa magari kwenye mageti ya kuingilia hifadhini ili kudhibiti vitendo hivyo.


Aidha, ametoa onyo kali kwa wafanyabiashara hao na kuwataka kufanya biashara hiyo kwa weledi na kuzingatia kanuni na taratibu zilizowekwa ikiwemo kulipa ada ya leseni husika kwa mujibu wa sheria. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wadau wa utalii Jijini Arusha jana ambapo Wizara yake iliwasilisha mapendekezo ya viwango vipya vya leseni za biashara ya utalii na tozo ya ada za malazi katika viwango vya ubora wa nyota. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk. Aloyce Nzuki na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Wizara ya Maliasili na Utalii, Deogratias Mdamu (kushoto).
Baadhi ya viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii na Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo wakiwa kwenye mkutano huo.
 Baadhi ya viongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii na Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo wakiwa kwenye mkutano huo.
 Baadhi ya wadau wa Utalii walioshiriki mkutano huo.
Mwenyekiti wa Chama cha Waongoza Watalii Tanzania (TATO), Wilbard Chambulo akichangia mapendekezo ya viwango vipya vya leseni za biashara ya utalii zilizowasilishwa kwao na Uongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii katika mkutano huo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akitambulishwa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk. Aloyce Nzuki (kushoto) kwa Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Waongoza Watalii Tanzania (TATO), Merywn Nunes muda mfupi baada ya kikao na wadau wa utalii Jijini Arusha jana ambapo Wizara yake iliwasilisha mapendekezo ya viwango vipya vya leseni za biashara ya utalii na tozo ya ada za malazi katika viwango vya ubora wa nyota.