slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Monday, July 9, 2018

WAZIRI KIGWANGALLA ATEMBELEA HIFADHI YA MSITU WA NORTH EAST MPANDA, TONGWE NA MAPOROMOKO YA NKONDWE MKOANI KATAVI

 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na uongozi wa wilaya ya Tanganyika alipotembelea wilaya hiyo jana wakati wa ziara yake ya kuimarisha uhifadhi mkoani Katavi. Kulia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Salehe Mbwana Mhando.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa ramani ya Hifadhi ya Msitu wa North East Mpanda alipotembelea msitu huo jana kwa ajili ya kuimarisha uhifadhi.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Kigwangalla akikagua moja ya eneo la chanzo cha maji yanayozalisha Maporomoko ya Nkondwe katika wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi jana, maji hayo yanapita chini ya miamba (mawe) inayoonekana. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Salehe Mhando. 
Waziri Kigwangalla akivuka kigingi alipokua akienda kuangalia maporomoko ya Nkondwe.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla na viongozi wengine wa wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi wakikagua eneo la Msitu wa Hifadhi wa North East Mpanda ambao pia una kivutio cha utalii cha Maporomoko ya Nkondwe wilayani humo.
Muonekano wa Maporomoko ya Nkondwe jana ambayo ni moja ya kivutio cha utalii, katika wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawako pichani) kuhusu Maporomoko ya Nkondwe na fursa za utalii zinazopatikana katika wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi jana. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika, Salehe Mbwana Mhando.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla na viongozi wengine wa wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi wakifurahia maporomoko ya Nkondwe ambayo ni miongoni mwa vivutio vya asili mkoani humo.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiangalia maumbo ya asili kwenye miamba iliyopo karibu na Maporomoko ya Nkondwe ambayo ni miongoni mwa kivutio cha utalii katika wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi jana.  Kushoto ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Salehe Mhando.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla na viongozi wengine wa wilaya ya Tanganyika akiwemo Mkuu wa Wilaya hiyo, Selehe Mhando (wa pili kulia) wakikagua Msitu wa Hifadhi wa North East Ugala baada ya kutembelea maporomoko ya Nkondwe.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla na viongozi wengine wa wilaya ya Tanganyika akiwemo Mkuu wa Wilaya hiyo, Selehe Mhando (kulia kwake) wakiwa wamepumzika kidogo baada ya kupanda mlima uliopo ndani ya Msitu wa Hifadhi wa North East Ugala baada ya kutembelea maporomo ya Nkondwe jana.
Msitu wa Tongwe ni moja ya misitu michache ya asili iliyohifadhiwa vizuri mkoani Katavi.

No comments:

Post a Comment