slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Monday, March 18, 2019

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUJA NA MKAKATI MAALUM WA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu amesema Wizara ya Maliasili na Utalii  inatarajia kuja na mkakati maalum wa kutangaza utalii ndani na nje ya nchi kwa kunadi  maeneo ya vivutio vya utalii badala ya kuinadi nchi kwa ujumla na  vivutio vyake

Pia,Amesema  maeneo hayo yatakuwa yakinadiwa  kwa mfumo wa vifurushi (Packages) hali itakayopelekea mtalii akija nchini ataweza kutembelea maeneo ya  Hifadhi,  Misitu ya Mazingira asilia pamoja na  maeneo ya utalii wa kiutamaduni.

Amesema lengo la kuja na mkakati huo ni kusaidia maeneo hayo kuweza kujulikana pamoja na kumuwezesha mtalii kuweza kuvifahamu vivutio vinavyopatikana katika eneo hilo kwa undani badala ya kuitangaza nchi kwa kujumuisha vivutio vya utalii vilivyopo  kwa ujumla wake.

Amesema mkakati huo utasaidia  kuongeza idadi ya watalii katika maeneo yenye vivutio ya utalii lakini kwa sasa yamekuwa yakipata idadi ndodgo ya watalii kwa vile yamekuwa hayafahamiki ipasavyo.

Amesema mkakati huo utalenga zaidi katika maeneo yenye utalii wa kiutamaduni pamoja na maeneo ya Misitu asilia, Ni utalii mpya ambao kwa Tanzania haufahamiki sana unaojikita kuangaliia viumbe ambao wapo hatarini kutoweka.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri huyo mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakati Kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi pamoja na Msitu Asilia wa Chome katika wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro.

Ameeleza kuwa aina hiyo ya kutangza vivutio vya utalii katika eneo fulani badala ya nchi italeta manufaa makubwa kwa Hifadhi na maeneo yale ambayo kwa sasa yamekuwa yakipokea idadi ndogo ya watalii hasa katika ukanda wa Kusini na Magharibi.

Amesema ukizungumzia utalii kwa sasa unalenga mikoa ya Kaskazini ambako zaidi ya asilimia 80 unafanyika ukanda huko huku kanda nyingine kama vile kanda ya ziwa, Magharibi pamoja na Kusini zikiwa bado idadi ya watalii wanaotembelea ni ndogo ukilinganisha na uwingi wa vivutio vya utalii vilivyopo katika maeneo hayo.

Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Shabani Shekilindi amesema Tanzania imejaliwa kuwa na vivutio vingi vya utalii lakini mapato yatokanayo na utalii hayaakisi ualisia wa vivutio vilivyopo nchini hivyo mikakati mipya ya kutangaza vivutio inahitajika.


 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii, Shabani Shekilindi (wa kwanza kushoto) akiwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu ( wa pili kushoto) wakiwa pamoja na Wajumbe wa kamati hiyo wakipewa maelezo mafupi kuhusu mradi wa kuzalisha faru weusi na mbwa mwitu kutoka kwa Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa (TANAPA) unaofanyika katika Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi wakati Kamati ilipofanya ziara katika Hifadhi hiyo iliyoko mkoani Kilimanjaro.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu akipigiwa saluti na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi wakati alipokuwa ameongozana na Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii ilipotembelea eneo hilo kwa ajili yamradi wa kuzalisha faru weusi na mbwa mwitu
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii kutembelea eneo la maradi wa kuzalisha faru weusi na mwitu katika Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi mkoani Kilimanjaro. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki.



 Baadhi ya Wajumbe wa  kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii walipotembelea ofisi ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania iliyopo katika wilaya ya  Same







No comments:

Post a Comment