slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Monday, March 25, 2019

SERIKALI KUNYANG'ANYA HOTELI ILIZOZIBINAFSISHA




Serikali imeanza ukaguzi wa hoteli za Kitalii ilizozibinafsisha  kwa Wawekezaji na wale watakaobainika kuziendesha chini ya kiwango, watanyang'anywa na kupewa wawekezaji wengine walio tayari kuziendesha kwa manufaa ya kukuza utalii nchini.

Hatua hiyo inafanyika kufuatia  kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa watalii na wadau mbalimbali wa utalii juu ya  huduma  zisizoridhisha zinazotolewa na hoteli hizo.

Akizungumza mara baada ya kukagua baadhi ya hoteli za Kitalii ikiwemo ya   Soronera na Lobo, zilizo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara, Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe Constantine Kanyasu  amesema lengo la kubinafsishwa kwa Hoteli hizo ilikuwa  ni kuboresha huduma.

Pia,  Hoteli ya Musoma ya mkoani Mara  pamoja na Ngorongoro Wildllife iliyopo ndani ya Mamlaka ya Eneo la Ngorongoro ni  miongoni mwa hoteli   zilizofanyiwa ukaguzi.

Amesema  Mwekezaji asiyefanya hivyo atanyang'anywa umiliki ili apewe mwekezaji   mwingine mwenye uwezo wa kutoa huduma bora.

 Aidha, amesema  kumekuwa na tuhuma kwa baadhi ya hoteli zilizobinafsishwa kukwepa kodi ya tozo ya huduma pamoja kuwalipa wafanyakazi wazawa mishahara midogo huku wale wa kigeni wakilipwa mishahara mikubwa kwa kazi ya aina moja.

Mhe. Kanyasu amesisitiza kuwa, Serikali ilizibinafsisha hoteli hizo ili zilete mapinduzi katika nyanja ya ajira, huduma bora kwa watalii, kodi pamoja kuziboresha ili zikidhi soko la watalii kwa sasa.

Akizungumza mara baada ya kukagua hoteli hizo,Mhe Kanyasu amebainisha  baadhi vitu alivyoviona ikiwemo uchakavu wa miundombinu pamoja na udanganyifu wa idadi ya watalii wanaofikia katika hoteli hizo .

Amesema Wizara  itapeleka idadi ya hoteli zitakazobainika kwenda kinyume  ili Msajiri wa Hazina  aweze kuzifutia  umiliki.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Kanyasu  amewataka viongozi wa Hoteli hizo kukaa na kuona ni namna watakavyoongeza idadi ya Watanzania wanaotembelea hifadhi na kupata mapumziko katika Hoteli hizo.

 Kuhusu Tozo ya huduma ya Mapato amezielekeza Halmashauri mbalimbali ikiwemo ya Serengeti kupata taarifa sahihi kutoka  Hifadhi za Taifa ( TANAPA)

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya  Serengeti,  Victor Tonesha  amesema changamoto inayoikabili Halmashauri hiyo ni ya  kushindwa kubaini kiwango halisi cha fedha zinazotolewa na Wawekezaji hao.




Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,  Constantine Kanyasu (katikati)  akizungumza na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya y Serengeti ikiongozwa na  Mkuu wa wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu  mara baada ya kukagua hoteli ya Soronera  iliyopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti  mkoani Mara kwa lengo la kubaini hoteli zilizobinafsishwa na serikali ambazo zimekuwa hazifanyi vizuri.

  


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,  Constantine Kanyasu (kulia) akiwa pamoja na  Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa ( TANAPA), Martin Looiboki wakiwa wameambatana kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya  Serengeti  wakiwa katika hoteli ya Soronera  iliyopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti  mkoani Mara wakiwa wanaikagua kwa lengo la kubaini hoteli zilizobinafsishwa na serikali ambazo zimekuwa hazifanyi vizuri.



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,  Constantine Kanyasu (kulia) akizungumza na Meneja wa Hoteli ya Soronera,Asram Narwat  katika jiko la hoteli hiyo wakati Naibu Waziri huyo alipokuwa akiikagua hoteli ambayo ni miongoni mwa hoteli ambazo zilibinafsishwa na Serikali kwa Wawekezaji kwa lengo la kuboresha Huduma kwa watalii. Hoteli hiyo ipo ndani ya Hifadhi ya Serengeti mkoani Mara kwa  lengo la kukagua ili  kubaini hoteli zilizobinafsishwa na serikali ambazo zimekuwa hazifanyi vizuri.





Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,  Constantine Kanyasu (kulia) akiwa pamoja na  Mkuu wa  wa wilaya  ya Serengeti, Nurdin Babu wakiongozwa na  Meneja wa Hoteli  ya Soronera, Asram Narwat katika Hoteli ya Soronera  iliyopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti  mkoani Mara, Hoteli hiyo ipo ndani ya Hifadhi ya Serengeti mkoani Mara kwa  lengo la kukagua ili  kubaini hoteli zilizobinafsishwa na serikali ambazo zimekuwa hazifanyi vizuri



Muonekanao wa hoteli ya Soronera kwa upande wa ndani kati vyumba vya hoteli hiyo iliyopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara amabayo ni moja ya Hoteli ilyobinafsishwa na Serikali kwa Wawekezaji.


No comments:

Post a Comment