slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Monday, May 30, 2016

BAJETI YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII (2016/2017) YAPITISHWA NA BUNGE

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 25 Mei, 2016 limekubali kupitisha bajeti ya Wizara ya Maliasili ikiwa na makadirio ya mapato na matumizi ya jumla ya Sh. 135,797,787,000 kwa mwaka 2016/2017. Kati ya fedha hizo, Sh. 118,051,105,000 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Sh. 17,746,682,000 ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo. Fedha za Matumizi ya Kawaida zinajumuisha Sh. 59,592,676,000 za Mishahara ya watumishi na Sh.58,458,429,000 za Matumizi Mengineyo. Fedha za Miradi ya Maendeleo zinajumuisha Sh. 15,746,682,000 fedha za nje na Sh.2,000,000,000 fedha za ndani. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (Mb) akijibu hoja mbalimbali za wabunge wakati wa kuwasilisha Hotuba ya Bajeti ya Wizara (2016/2017) katika bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 24-25 Mei, 2016.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (Mb) na Naibu Waziri, Eng. Ramo Makani (Mb) wakipongezwa na baadhi ya wabunge ndani ya ukumbi wa bunge baada ya kujibu hoja mbalimbali na kufanikisha kupitishwa kwa bajeti ya Wizara.

Picha ya pamoja kati ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (Mb), Naibu Waziri, Eng. Ramo Makani (Mb), Katibu Mkuu, Maj. Gen. Gaudence Milanzi, Naibu Katibu Mkuu, Angelina Madete, Vingozi wa Idara na Vitengo pamoja na Viongozi wa Taasisi mbalimbali za Wizara hiyo muda mfupi baada ya Bajeti ya Wizara kupitishwa na Bunge tarehe 25 Mei, 2016 nje ya Ukumbi wa Bunge, Dodoma.

No comments:

Post a Comment