slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Wednesday, September 28, 2016

TANGAZO KWA UMMA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA  MALIASILI NA UTALII




WAFANYABIASHARA WA UTALII KUSAJILI NA KULIPIA ADA YA LESENI YA MWAKA 2016

Wizara ya Maliasili na Utalii inawakumbusha wafanya biashara za utalii wasiokuwa na leseni ya biashara hiyo inayotolewa kwa mujibu wa sheria ya Utalii Na. 29 ya Mwaka 2008 Vifungu Na.10 na 31, kuwa wanatakiwa kusajili na kulipia ada ya leseni kwa mwaka 2016 ifikapo tarehe 31 Oktoba, 2016.

Biashara za Utalii husika ni hizi zifuatazo:

1
Kampuni za kusafirisha watalii
10
Vivutio vya kuuza bidhaa za urithi (Cultural heritage centres)
2
Kampuni za uwindaji wa kitalii
11
Wajasiriamali wa utalii wa utamaduni (Cultural tourism enterprises)
3
Wawindaji Bingwa
12
Kampuni za kukodisha vifaa vya utalii

4
Kampuni za kusafirisha watalii kwa ndege
13
Maeneo ya michezo ya burdani (Theme parks, wildlife forms. Zoo, snake parks etc)
5
Kampuni za kusafirisha watalii kwa Maputo (hot air balloon)
14
Kampuni za kukodisha magari kwa watalii
6
Kampuni za kusafirisha watalii kwa farasi
15
Kampuni za kukatisha tiketi za ndege
7
Kampuni za kusafirisha watalii kwa boti
16
Wakala wa kutoa huduma kwa watalii (tourist handling agents)
8
Kampuni za kupandisha watalii Milimani
17
Nyumba za huduma za malazi (hoteli, loji, kambi za kitalii)
9
Kampuni za utalii wa michezo ya kusisimua (tourism adventure sports)
18
Maduka ya zawadi za kitalii (Curio Chops)



i.      Wizara inachukua nafasi hii pia kusisitiza kwamba ni kosa linalostahili adhabu  kisheria kufanya biashara ya utalii bila ya kusajili na kulipia ada ya leseni kwa  mwaka husika.

ii.        Vilevile, tunapenda kuwafahamisha kuwa maombi kwa ajili ya leseni ya kufanya  biashara ya utalii kwa mwaka 2017 yameanza kupokelewa katika Ofisi zetu zilizopo Dare s Salaam, Arusha, Mwanza na Iringa.

iii.    Orodha ya wafanyabiashara ya utalii waliosajiliwa na kulipia ada za leseni  inapatikana katika tovuti ya Wizara (www.mnrt.go.tz), na katika ofisi za Wizara  zilizotajwa hapo juu.

Angalizo: Umma unatahadharishwa kutofanya biashara na kampuni za biashara za utalii ambazo hazina Leseni ya Biashara ya Utalii ya mwaka 2016, kwa kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha Sheria.


Imetolewa na:

KATIBU MKUU
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
Simu: +255 22 2864230

Barua pepe: ps@mnrt.go.tz

No comments:

Post a Comment