slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Tuesday, July 19, 2016

WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. KASSIM MAJALIWA AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII, AAGIZA MAUZO YA VITALU VYA MASHAMBA YA MITI YAFANYIKE KWA NJIA YA MNADA

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Watumishi wa Wazara ya Maliasili na Utalii kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha LAPF, Kijitonyama jijini Dar es salaam Julai 18, 2016 .
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza katika mkutano huo.
 Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi akizungumza katika Mkutano huo.
 Baadhi ya Watumishi wa Wizar ya Maliasili na Utalii wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha LAPF, Kijitonyama jijini Dar es salaam Julai 18, 2016 .
Baadhi ya Waandishi wa Habari na Watumishi wa Wizara ya Maliasi na Utalii katika Mkutano huo.
Picha ya pamoja kati wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa (katikati waliokaa) na Viongozi pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Maliasili na Utalii.
____________________________________

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Majaliwa Kassim Majaliwa ameuagiza uongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii kubadilisha mfumo wa uvunaji wa vitalu vya miti kwenye mashamba ya Serikali ili kuweka uwazi kwenye biashara hiyo na kuipatia zaidi Serikali mapato.

Mhe. Majaliwa alisema hayo jana kwenye Mkutano na Viongozi pamoja na Watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kisenga uliopo Kijitonayama Jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia mabadiliko hayo, Mhe. Majaliwa alisema kuwa utaratibu uliokuwa ukitumika hapo awali wa kuuza miti kwenye mashamba ya Serikali kwa njia ya vibali hauna tija kwakuwa umekuwa ukiikosesha Serikali mapato na kuwanufaisha wafanyabiashara wachache.

“Utaratibu wa sasa wa kutumia vibali unatuletea migongano ndani ya Wizara na kuikosesha Serikali mapato, hivyo ni lazima tuubadilishe” Aliongeza Majaliwa.

Aliuagiza Uongozi wa Wizara kufanya marekebisho kwenye utaratibu huo na kuweka utaratibu wa mnada ili kuweka uwazi zaidi na kuondoa manung’uniko kwenye biashara hiyo. “vibali visitishwe, mnada uanze  kama inavyofanyika kwenye mitiki” Alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Hivi karibuni Mhe. Majaliwa alisitisha utoaji wa vibali vya uvunaji wa miti kwenye mashamba matano yanayomilikiwa na Serikali kutokana na kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Majaliwa aliagiza mabadiliko ya haraka katika vizuizi vya ukaguzi wa Maliasili ambavyo amesema vimekuwa havina tija na kuagiza baadhi yake vifutwe kabisa. Miongoni vya vizuizi alivyoagiza vifutwe ni Kibaha Stendi, Kimanzichana na Mbagala, pia aliagiza kuimarishwa kwa kituo cha Vikindu, Kibiti na Vigwaza.

Mhe. Majaliwa aliwaagiza wataalamu wa Wizara ya Maliasili na Utalii kushirikiana na Tamisemi kwa ajili ya kuweka mfumo mzuri wa kuhifadhi na kuvuna mazao ya misitu yaliyopo katika Halmashauri na kutenga Misitu ya Asili tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo kumekuwepo muingiliano katika kutekeleza majukumu hayo jambo linalopelekea uharibifu wa misitu. 

Hapo awali Mhe. Majaliwa alieleza lengo kuu la Mkutano huo kuwa ni katika utaratibu wake wa kawaida aliojiwekea wa kutembelea Wizara na kuzungumza na watumishi kwa ajili kukumbushana majukumu yao, kuangalia changamoto mbalimbali na kuzitafutia ufumbuzi. Aliwaasa watumishi wa Wizara ya Maliasili kuwa wazalendo, waadilifu, waaminifu na kuongeza uwajibikaji ili kuiwezesha Serikali kufikia malengo yake ya kuwahudumia vizuri wananchi.

“Ninyi ni watu muhimu sana katika utoaji wa huduma kwa wananchi, tekelezeni majukumu yenu kwa uadilifu wa hali ya juu. Kamilisheni malengo yenu kulingana na mpangokazi wenu mliojiwekea” Alisema Mhe. Majaliwa.

Kwa upande wake Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe alisisitiza watumishi wa Wizara hiyo kuhakikisha kuwa wanalinda misitu kule iliko na sio kusubiri katika vituo na kukamata rasilimali zake ambazo zimevunwa isivyo halali na kuzitoza faini, kinyume chake rasilimali hizo zilipiwe kihalali kabla ya kuvunwa. Aliahidi pia kuisuka upya Idara ya Misitu. 

Thursday, July 14, 2016

WAZIRI WA MALIASILI, PROF. JUMANNE MAGHEMBE AONANA NA BALOZI WA FINLAND HAPA NCHINI, PEKKA HUKKA

Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe (katikati) akizungumza na Balozi wa Finland  hapa nchini, Pekka Hukka (kulia) alipotembelewa na Balozi huyo ofisini kwake, Mpingo House taerehe 12 Julai, 2016. Kushoto ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa TFS, Richard Kamwenda.
 Balozi wa Finland hapa nchini, Pekka Hukka (kulia), akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Waziri wa Maliasili Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kulia) alipomtembelea ofisini kwake kujadili mambo mbalimbali yanayohusu Uhifadhi wa Maliasili na uendelezaji wa sekta ya Misitu nchini. Kushoto ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa TFS, Richard Kamwenda.

Tuesday, July 12, 2016

WAZIRI WA MALIASILI PROF. JUMANNE MAGHEMBE AONANA NA BALOZI WA UJERUMANI HAPA NCHINI MHE. EGON KONCHANKE

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akimkaribisha Balozi wa Ujerumani hapa nchini, Mhe. Egon Konchanke alipomtembelea jana tarehe 11 Julai, 2016 ofisini kwake, Mpingo House, Jijini Dar es Salaam kujadili mambo mbalimbali yanayohusu sekta ya Maliasili nchini.
Waziri Maghembe (kulia) akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Balozi Konchanke (kushoto).
Balozi Konchanke (kushoto) akimueleza jambo Prof. Maghembe (kulia) katika mazungumzo hayo.
Balozi Konchanke (kushoto) akimuonesha Waziri Maghembe (kulia) ramani ya Hifadhi ya Taifa ya Katavi ambayo Balozi huyo ameahidi kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuendeleza utalii wake kwa pamoja na ule wa Mkoa wa Kigoma (Hifadhi ya Mahale)
Waziri Maghembe (kulia) akizungumza katika kikao hicho.

______________________________________


Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeweka wazi msimamo wake kuwa haitauza meno yake ya Tembo yaliyohifadhiwa kwa kuwa kufanya hivyo ni kuongeza upatikani wa meno hayo kwenye soko hivyo kuchochea biashara haramu ya ujangili.

Hayo yamesemwa jana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe alipokuwa kwenye mazungumzo ya na Balozi wa Ujerumani hapa nchini, Egon Konchanke ofisini kwake Mpingo House, Jijini Dar es Salaam.

Balozi Konchanke alimueleza Prof. Maghembe kuwa, mwezi Septemba mwaka huu (2016), Wanachama wa Mkataba wa Kimataifa unaosimamia biashara ya Viumbe vilivyo hatarini kutoweka vya wanyama na mimea (CITES) watakutana nchini Afrika ya Kusini kujadili mambo mbali mbali ikiwemo baadhi ya nchi wanachama ikiwemo Namibia kutaka kuuza Meno yake ya Tembo yaliyohifadhiwa ili kujipatia kipato.

Katika maelezo yake Balozi Konchanke alimuomba Prof. Maghembe kutoa msimamo wa Serikali ya Tanzania kuhusu hoja hiyo ya kuuza meno ya tembo yaliyohifadhiwa kutokana na matukio ya Ujangili na vifo asilia vya wanyama. “Ni upi msimamo wa Tanzania katika kuelekea mkutano huo kuhusiana na uamuzi wa nchi kama Namibia wa kuuza meno yake ya tembo yaliyohifdhiwa?” aliuliza Balozi Konchanke.

Katika majibu yake Prof. Maghembe alisema “Tanzania tunaungana na mataifa mengine ambayo yanapinga uuzwaji wa meno ya tembo, Kama tukiuza meno haya tutaongeza upatikanaje wake kwenye masoko, hivyo kuchochea zaidi biashara hii haramu, hatuna sababu ya kuyauza wala kuyachoma moto, ukiyachoma moto unakuwa umechoma kila kitu ikiwemo sampuli ambazo zingeweza kutumika kwenye tafiti mbalimbali zikiwemo za kutengeneza madawa ya kutibu maradhi ya wanyama hao”. Aliongeza kuwa nchi zitakazofanya hivyo zitakuwa hazijafanya jambo la busara zaidi ya kuleta maafa kwa nchi jirani ya kuongezeka kwa vitendo vya ujangili.

Wakati huo huo, Waziri Maghembe alimuomba Balozi Konchanke kuleta wawekezaji kutoka Ujerumani kwa ajili ya kuwekeza katika sekta ya Utalii na Uhifadhi hapa nchini. Balozi huyo aliahidi ushirikiano kwa Serikali ya Tanzania ambapo alisema mwishoni mwa mwezi huu wa Julai Waziri wa Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo wa Serikali ya Ujerumani Dkt. Gerd Muller atakuja nchini na wafanyabiashara kutoka nchini humo wenye nia ya kuwekeza katika sekta ya Uhifadhi na Kilimo.

Balozi Konchanke ameahidi pia kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuendeleza Utalii kwenye Mikoa ya Kigoma na Katavi kwa kuunganisha utalii wa Hifadhi ya Mahale na Hifadhi ya Katavi. Amesema kuwa eneo hilo linahitajika kuwekewa miundombinu mizuri ya barabara ili liweze kufikika kirahisi.

Kwa upande wake Waziri Maghembe amesema kuwa utalii katika Mikoa hiyo unapewa nafasi kubwa ili uweze kukua na kuliingizia zaidi taifa mapato. Ameeleza kuwa katika kukabiliana na changamoto ya usafiri zitaansishwa safari za ndege za bei nafuu mara tatu kwa wiki kutoka Dar es Salaam kwenda Mikoa ya Kigoma na Katavi kwa bei ya dola za kimarekani 150.

Akizungumzia kuhusu kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwenye huduma za Utalii wakati akijibu hoja ya Balozi Konchanke juu ya malalamiko ya watoa huduma hizo kuwa sheria hiyo imekuja ghafla na inapunguza ujio wa watalii nchini, Waziri Maghembe alisema sheria hiyo imepitishwa na bunge na watoa huduma hao walishataarifiwa toka mwaka jana (2015) juu ya mabadiliko ya sheria hiyo kwa ajili ya kufanya maandalizi ya mabadiliko yake. Aliongeza kuwa ili Serikali ijiendeshe inahitaji mapato na kwamba watalii wanalipa kodi hivyo na watoa huduma nao wanahitajika kulipa kodi.

Katika hatua nyingine Balozi Konchanke aliomba ufafanuzi kwa Waziri Maghembe juu utaratibu mpya wa mashirika ya umma kupeleka fedha zote za makusanyo hazina na kwamba kama wahisani wakichangia kuendeleza mashirika hayo ikiwepo TANAPA na TAWA, pengine lengo lao litakuwa halijafikiwa na hivyo kuwa vigumu kujiendesha. Akijibu hoja hiyo Waziri Maghembe alisema kumekuepo na uelewa hafifu juu ya utaratibu huo ambao kimsingi Mamlaka hizo ikiwemo TANAPA na TAWA zitapelekea fedha zao hazina na kuzitumia pale itakapohitajikwa kwa mujibu wa mpango kazi wao.