slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Tuesday, August 16, 2016

KATIBU MKUU WIZARA YA MALIASILI NA UTALII, MAJ. GEN. GAUDENCE MILANZI AFUNGA MAFUNZO YA JESHI USU KWA WAHIFADHI WA TANAPA NA NGORONGORO WILAYANI MLELE, MKOA WA KATAVI

Gwaride la wahitimu wa mafunzo ya kijeshi kwa askari na maafisa wa Hifadhi za Taifa likiingia katika viwanja vya mazoezi katika kambi ya mafunzo ya Mlele wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi akipokea salamu ya utii kutoka kwa askari wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (hawapo pichani) wakati wa ufungaji mafunzo kwa askari na maafisa hao yaliyofanyika katika kambi ya mafunzo ya Mlele mkoani Katavi 


Askari na Maafisa wa Hifadhi wakipita kwa heshima mbele ya mgeni rasmi kwa mwendo wa pole na haraka wakati wa ufungaji wa mafunzo ya kijeshi waliyopata katika kambi ya mafunzo ya Mlele mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya kubadili utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuendeshwa katika mfumo wa jeshi usu kutoka mfumo wa kiraia.Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi akikagua gwaride wakati wa kufunga mafunzo kwa askari wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro yaliyofanyika katika kambi ya mafunzo ya Mlele mkoani Katavi 


Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi(kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi wakipokea salamu za heshima kwa kupiga saluti wakati gwaride likipita mbele kwa heshima wakati wa ufungaji wa mafunzo kwa askari wa shirika la Hifadhi za Taifa,(TANAPA) na Maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya taifa Ngorongoro.

Bendi ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) ikipita mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa ufungaji wa mafunzo ya kijeshi kwa askari na maafisa wa Hifadhi ,Mafunzo yaliyofanyika katika kambi ya Mlele mkoani Katavi.
Askari na Maafisa wa Hifadhi za Taifa wakionesha umahiri katika matumizi ya silaha wakati wakionesha kwa vitendo mafunzo ya kijeshi waliyopata katika kambi ya Mlele mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya kubadili utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuendeshwa katika mfumo wa jeshi usu. 

Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Witness Shoo (kushoto) pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Uhifadhi Mtango Mtahiko wakifuatilia maonesho ya matumizi ya silaha kutoka kwa wahitimu hao.
Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete akisherehesha wakati wa ufungaji wa mafunzo ya kijeshi kwa askari na Maafisa wa Hifadhi waliyopata katika kambi ya Mlele mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya kubadili utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuendeshwa katika mfumo wa jeshi usu.

Askari na Maafisa wa Hifadhi wakionesha umahiri katika matumizi ya silaha wakati wakionesha kwa vitendo mafunzo ya kijeshi waliyopata katika kambi ya jeshi ya Mlele mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya kubadili utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuendeshwa katika mfumo wa jeshi usu.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi,Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi pamoja na Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ,Freddy Manongi wakifuatilia maonesho hayo. 





Askari na Maafisa wa Hifadhi wakionesha umahiri katika matumizi ya silaha wakati wakionesha kwa vitendo mafunzo ya kijeshi waliyopata katika kambi ya Mlele mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya kubadili utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuendeshwa katika mfumo wa jeshi usu. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi akitizama matundu ya risasi zilizolengwa na mmoja wa askari wa uhifadhi waliohitimu mafunzo ya kijeshi katika kambi ya Mlele mkoani Katavi.Kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi. 
Wakufunzi wa Mafunzo ya kijeshi kwa maofisa na askari wa Hifadhi za Taifa wakitambulishwa mbele ya mgeni rasmi,(hayupo pichani). 
Mhifadhi kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Lilian Magoma akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wenzake wa mafunzo ya kijeshi yaliyofanyika katika kambi ya Mlele iliyopo mkoani Katavi.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi akitunuku vyeti kwa askari na maafisa wa uhifadhi waliohitimu mafunzo ya kijeshi katika kambi ya Mlele mkoani Katavi. 
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Getrude Lyatuu akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo. 

Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro,Freddy Manongi akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo. 

Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori Alexander Songorwa akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA)Allan Kijazi akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo. 
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akimkaribisha Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi kuzungumza na wahitimu wa mafunzo ya kijeshi kwa askari na maofisa wa Hifadhi za Taifa . 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo kwa askari na maofisa wa Hifadhi za Taifa. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi na viongozi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi na viongozi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii wakiwa katika pichaya pamoja na wahitimu wa mafunzo ya kijeshi yaliyofanyika katika kambi ya Mlele mkoani Katavi. Na Dixon Busagaga wa Michuzi

Thursday, August 11, 2016

PROF. MAGHEMBE AZINDUA KITABU CHA KUHAMASISHA ULINZI WA TEMBO NA FARU (TEMBO - FARU WANA HAKI YA KUISHI TANZANIA)

Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Mhe. Ally Hassan Mwinyi (kulia) akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kitabu cha kuhamasisha ulinzi wa Tembo na Faru pamoja na kupiga vita ujangili kilichoandikwa na Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini Mkoa wa Dar es Salaam jana katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwl. J.K. Nyerere, Dar es Salaam. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe akionesha kitabu hicho kwa wajumbe walioshiriki hafla hiyo kama ishara ya kukizindua rasmi kwa niaba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.
Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Mhe. Ally Hassan Mwinyi (kulia) akiteta jambo na Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akimkabidhi Mwanasiasa Mkongwe nchini ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa chama cha CUF, Prof. Ibrahim Lipumba nakala ya kitabu hicho. Wapili kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhad Mussa Salum.
Picha ya pamoja.

------------------------------------------------------------------

Rais Mstaafu wa Awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Ally Hassan Mwinyi ametoa wito kwa watanzania kuongeza juhudi katika kusaidiana na Serikali kupiga vita ujangili hapa nchini.


Wito huo umetolewa jana jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa kitabu cha “Tembo-Faru wana haki ya kuishi Tanzania” kilichoandaliwa na Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini Mkoa wa Dar  es salaam na kuzinduliwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe kwa niaba ya Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli.

Rais mstaafu huyo, amesema kumekuwa na tatizo la mauaji ya wanyamapori hapa nchini ambayo ni dhambi na ni kinyume na kusudio la Mungu kwa kuwa wanyama hao wana haki ya kuishi kama viumbe wengine.

“Kumekuwa na matukio mengi ya uuaji wa wanyamapori ikiwemo tembo na faru na hivyo kupunguza rasilimali ya taifa kwa vizazi vijavyo na pia kitendo hicho ni kinyume na kusudio la Mungu hivyo ni vizuri kuwatunza, kuwapenda, kuwaendeleza na kuwalinda wanyama hao kwani ni moja ya vivutio vinavyochangia pato la Taifa” aliongeza Rais Mstaafu  Mwinyi.

Kwa upande wake Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe amesema kuwa Tanzania ni nchi ya pili kwa kuwa na mbuga nzuri na bora duniani baada ya nchi ya Brazil na kusisitiza ni muhimu kwa watanzania wote kutunza rasilimali za taifa ikiwemo mbuga za wanyama na wanyamapori.


Aliongeza kuwa wanyamapori ni muhimu sana katika maisha ya kila mtanzania kwa kuwa kupitia utalii wanachangia asilimia 17.5 ya pato la taifa na asilimia 25 ya mapato yote ya fedha za nje (foreign currency) hivyo hakuna budi kwa kila mtanzania kupiga vita ujangili ambao.
Alisema kuwa jumuiya ya ujangili ni kubwa ambayo inahusisha  makundi mbalimbali ikiwemo watengenezaji wa silaha za kuua tembo, waagizaji wa meno ya tembo, wasambazaji na watu mashuhuri ambao wanatumia nyumba zao kuhifadhina kununua meno ya tembo.


Kitabu cha “Tembo-Faru wana haki ya kuishi Tanzania” kimetayarishwa na kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini Mkoa wa Dar es salaam kikiwa na lengo la kuwaelimisha waanadamu juu ya umuhimu wa kutunza mazingira na viumbe vilivyopo kwa faida yao na vizazi vijavyo.


Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye ni Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Mussa Salum alisema jumla ya vitabu 5,000 vimechapishwa kwa ufadhili wa shirika la kimataifa la WILDAID, Jumla ya nakala milioni 20 zinahitajika kuchapishwa katika lugha tofauti na kusambaza katika nchi mbalimbali duniani na hivyo kuwaomba wadau mbalimbali kuchangia gharama za uchapishaji huo ambao kwa kila kitabu kimoja kinagharimu dola kimarekani 12.


Akizungumzia uchangiaji huo, Waziri Maghembe alisema kuwa Mfuko wa Hifadhi ya Wanyamapori Tanzania (TWPF) utachangia milioni 20 kuwezesha uchapishaji wa vitabu hivyo na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kuunga mkono juhudi za vingozi wa dini na Serikali katika kulinda na kuhifadhi Malisili za taifa kwa kuchangia uchapishaji wa kitabu hicho na kulinda Malisili za taifa.

Sunday, August 7, 2016

KATIBU MKUU WIZARA YA MALIASILI NA UTALII, MAJ. GEN. GAUDENCE MILANZI AONGOZA WATUMISHI WA WIZARA HIYO KUMUAGA ALIYEKUWA MKURUGENZI WA UTAWALA NA RASILIMALI WATU, SAID MSAMBACHI

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza katika hafla fupi iliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi, Said Msambachi (kulia) aliyestaafu rasmi kwa mujibu wa sheria tarehe 16 Juni, 2016. Hafla hiyo ilifanyika juzi tarehe 05 Agosti, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa Selous, Makao Makuu wa Wizara hiyo, Jengo la Mpingo, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi (kulia) akitoa nasaha zake kwa watumishi wa Wizara hiyo katika hafla fupi ya kumuaga iliyoandaliwa na watumishi hao tarehe 05 Agosti, 2016. Aliwaasa watumishi hao kutekeleza majukumu yao kwa kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na uaminifu kama chachu ya maendeleo yao kazini. Aliwataka pia kufanya kazi kwa ushirikiano kujiepusha na majungu, vitendo vya rushwa na ubaguzi pahala pa kazi. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maj. Gen. Gaudence Milanzi.
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi, Ziana Mlawa (kushoto) akitoa shukurani kwa niaba ya watumishi wote kwa ushirikiano walioupata kutoka kwa Bw. Said Msambachi (kulia) katika kipindi chote cha miaka mitano alichofanya kazi katika Wizara hiyo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu, Idara ya Utawala na Utumishi, Aurelia Matagi, akitoa ufafanuzi wa ratiba na kuongoza utambulisho katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi na Mama Msambachi wakikata Keki ya kuagwa waliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo.
Taswira ya keki hiyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (wa tatu kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala, Said Msambachi (wa pili kulia) risiti ya friji (pichani kulia) aliyozawadiwa na watumishi wa Wizara hiyo.
 Baadhi ya watumishi wa Wizara hiyo katika hafla hiyo.
 Baadhi ya watumishi wa Wizara walioshiriki hafla hiyo.
 Baadhi ya watumishi wa Wizara katika hafla hiyo.
 Sehemu ya watumishi katika hafla hiyo.
 Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza na watumishi walihudhuria hafla hiyo.
 Picha ya pamoja kati ya Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (wa pili kushoto, msatari wa mbele), Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Said Msambachi (wa tatu kushoto), Mkurugenzi anayekaimu nafasi yake kwa sasa ambaye pia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Ziana Mlawa (kulia), Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu, Aurelia Matagi na Watumishi wa Wizara walioshiriki hafla hiyo (mstari wa pili na wa tatu nyuma) .
Picha ya pamoja kati ya Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi (katikati) na Mkurugenzi anayekaimu nafasi yake kwa sasa ambaye pia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Ziana Mlawa (kulia) na Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu, Aurelia Matagi (kushoto).

Monday, August 1, 2016

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI, ENG. RAMO MAKANI AONGEA NA WANANCHI WA KONDOA VIJIJINI KUHUSU UTATUZI WA MGOGORO WA PORI LA AKIBA MKUNGUNERO

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (kulia) akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Keikei Wilayani Kondoa jana kwa ajili ya kusikiliza kero zao mbalimbali kuhusu Pori la Akiba Mkungunero. Wananchi hao wameiomba Serikali iwape maeneo kwa ajili ya Kilimo, Ufugaji na Makazi kutokana na uhaba wa ardhi katika maeneo hayo. 

Naibu Waziri Makani aliwaomba wananchi hao kuwa na subira wakati huu Serikali inapoenda kushuulikia maombi yao ambapo tayari imeshaundwa tume ambayo ipo chini ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kukusanya takwimu mbali mbali ikiwemo mahitaji halisi ya ardhi na idadi ya watu ambapo zitatumika katika kutatua changamoto zilizopo. 

Alieleza kuwa Serikali ya awamu ya tano imepanga kutatua kero mbalimbali za  wananchi ambapo tayari migogoro yote ya ardhi nchini imeshaorodheshwa kwa ajili ya kutafutiwa ufumbuzi wa kudumu, ambapo kitaundwa kikosi kazi cha kitaifa kitakachohusisha Wizara ya Ardhi, Kilimo, Maliasili, Tamisemi, Sheria na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira.

Eng. Makani alisema kuwa Tanzania bado ina maeneo mengi ambayo yanaweza kutumika kwa ajili ya kilimo na ufugaji, hivyo kumega hifadhi ili kukabiliana na tatizo uhaba wa ardhi itakuwa jambo la mwisho kufanyika baada ya maeneo mengine kuzingatiwa. Aliitaka tume iliyoundwa kukamilisha kazi yake haraka ili changamoto hiyo iweze kupatiwa ufumbuzi na mamlaka husika.

Pori la Akiba Mkungunero lilitangazwa rasmi na Tangazo la Serikali la mwaka 1996 na zoezi la kutafsiri mipaka husika likafanyika mwaka 2006. Tangu hapo ukaanza mgogoro kati ya wananchi na hifadhi kwa madai kuwa baadhi ya vitongoji vya vijiji vyao halali vipo ndani ya hifadhi hiyo. 
Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini, Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji (kulia) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango akizungumza na wananchi wa Jimbo lake wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika jana katika kijiji cha keikei Wilayani Kondoa.

 Dkt. Kijaji aliwasilisha kero na changamoto mbalimbali za wananchi wake, moja ikiwa ni uhaba wa maeneo kwa ajili ya kilimo na ufugaji,  maeneo ya vijiji halali vilivyopimwa kudaiwa kuwemo ndani ya hifadhi na mahusiano mabaya kati ya wananchi wake na watumishi wa Pori la Akiba Mkungunero. 

Akijibu changamoto hizo, Naibu Waziri Makani aliahidi kuzifanyia kazi kwa mujibu wa sheria za nchi na taratibu zilizowekwa mara baada ya tume iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa kukamilisha kazi yake na kukabidhi taarifa na mapendekezo yake Wizarani.  Aliongeza kuwa kumega maeneo ya hifadhi haiwezi kuwa jibu pekee la changamoto zinazowakabili wananchi bali wanaweza kutumia maeneo madogo waliyonayo kwa kuweka mipango mizuri ikawa na tija zaidi kwa taifa na watu wake.
Mwananchi wa Kijiji cha Kisondoko, Khalifa Othman akiwasilisha kero zake wakati wa mkutano huo. Kilio chake kikubwa kilikuwa kupatiwa maeneo kwa ajili ya ufugaji na kilimo. Kulia aliyesimama ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa Vijijini ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kwadelo, Omari Kariati. Kushoto ni Naibu Waziri, Eng. Ramo Makani.
  Mkazi wa Kijiji cha Kisondoko Wilayani Kondoa akitoa kero zake kwenye Mkutano huo. Aliiomba Serikali kuzisaidia jamii za Wabarbaij na Wamang'ati kupata maeneo ya kulima na kufuga kwakuwa kwa sasa jamii hizo zimetengwa na hazina kabisa maeneo kwa ajili ya shughuli hizo, "Sisi Wamang'ati hatuna hata kipande cha ardhi na tukifa hatujui tutazikwa wapi" alieleza. 
 Naibu Waziri Makani akiendelea kuongoza mkutano huo. Alifikisha salam za Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli kwa wananchi hao ambapo aliwataka, Kudumisha amani ya nchi yetu, kutumia amani hiyo kufanya kazi kwa bidii na kuzalisha zaidi kukuza uchumi wa taifa letu. 
Baadhi ya wajumbe walioshiriki mkutano huo.