slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Sunday, August 7, 2016

KATIBU MKUU WIZARA YA MALIASILI NA UTALII, MAJ. GEN. GAUDENCE MILANZI AONGOZA WATUMISHI WA WIZARA HIYO KUMUAGA ALIYEKUWA MKURUGENZI WA UTAWALA NA RASILIMALI WATU, SAID MSAMBACHI

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza katika hafla fupi iliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi, Said Msambachi (kulia) aliyestaafu rasmi kwa mujibu wa sheria tarehe 16 Juni, 2016. Hafla hiyo ilifanyika juzi tarehe 05 Agosti, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa Selous, Makao Makuu wa Wizara hiyo, Jengo la Mpingo, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi (kulia) akitoa nasaha zake kwa watumishi wa Wizara hiyo katika hafla fupi ya kumuaga iliyoandaliwa na watumishi hao tarehe 05 Agosti, 2016. Aliwaasa watumishi hao kutekeleza majukumu yao kwa kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na uaminifu kama chachu ya maendeleo yao kazini. Aliwataka pia kufanya kazi kwa ushirikiano kujiepusha na majungu, vitendo vya rushwa na ubaguzi pahala pa kazi. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maj. Gen. Gaudence Milanzi.
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi, Ziana Mlawa (kushoto) akitoa shukurani kwa niaba ya watumishi wote kwa ushirikiano walioupata kutoka kwa Bw. Said Msambachi (kulia) katika kipindi chote cha miaka mitano alichofanya kazi katika Wizara hiyo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu, Idara ya Utawala na Utumishi, Aurelia Matagi, akitoa ufafanuzi wa ratiba na kuongoza utambulisho katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi na Mama Msambachi wakikata Keki ya kuagwa waliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo.
Taswira ya keki hiyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (wa tatu kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala, Said Msambachi (wa pili kulia) risiti ya friji (pichani kulia) aliyozawadiwa na watumishi wa Wizara hiyo.
 Baadhi ya watumishi wa Wizara hiyo katika hafla hiyo.
 Baadhi ya watumishi wa Wizara walioshiriki hafla hiyo.
 Baadhi ya watumishi wa Wizara katika hafla hiyo.
 Sehemu ya watumishi katika hafla hiyo.
 Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza na watumishi walihudhuria hafla hiyo.
 Picha ya pamoja kati ya Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (wa pili kushoto, msatari wa mbele), Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Said Msambachi (wa tatu kushoto), Mkurugenzi anayekaimu nafasi yake kwa sasa ambaye pia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Ziana Mlawa (kulia), Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu, Aurelia Matagi na Watumishi wa Wizara walioshiriki hafla hiyo (mstari wa pili na wa tatu nyuma) .
Picha ya pamoja kati ya Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi (katikati) na Mkurugenzi anayekaimu nafasi yake kwa sasa ambaye pia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Ziana Mlawa (kulia) na Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali Watu, Aurelia Matagi (kushoto).

1 comment:

  1. Nampongeza Mhe. Katibu Mkuu wa Wizara kwa ubunifu wa kubadili Uhifadhi kuelekea mfumo wa Jeshi. hii itasaidia sana kuongeza nguvu kupambana na ujangili.

    ReplyDelete