slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Tuesday, December 5, 2017

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, JAPHET HASUNGA ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA KITULO, MAARUFU KAMA BUSTANI YA MUNGU

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy wakiangalia maua ya asili ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika hifadhi ya Taifa ya Kitulo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani. Hifadhi hiyo ni maarufu kwa wenyeji kama 'BUSTANI YA MUNGU'.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy (kulia) na baadhi ya viongozi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo wakiangalia maua ya asili ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika hifadhi hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa nne kulia), akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy (wa tatu kulia) na baadhi ya viongozi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia), Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kitulo, Pius Mzimbe wakiangalia maporomoko ya maji ya Mwakipembo ambayo ni kivutio cha utalii ndani ya hifadhi ya Kitulo wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Pamoja na kivutio hicho hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani. Hifadhi hiyo ni maarufu kwa wenyeji kama 'BUSTANI YA MUNGU'.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) akipata maelezo kuhusu maporomoko ya maji ya Mwakipembo ambayo ni kivutio cha utalii ndani ya hifadhi ya Taifa ya Kitulo kutoka kwa Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi hiyo, Pius Mzimbe wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy. Pamoja na kivutio hicho hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani.
Muonekano mwanana wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo. Hifadhi hii ina aina zaidi ya 350 za maua huku aina 35 yakiwa ndwele na hupatikana katika hifadhi hiyo pekee duniani. Vivutio vingine vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ni Maporomoko ya maji, ndege aina mbalimbali ambao wengine huama kutoka ulaya wakati wa baridi, wanyamapori aina Swala, Mbega na Nsya. Hata hivyo katika kutimiza mkakati wa Wizara kuboresha vivutio vya utalii, hifadhi hiyo ipo katika maandalizi ya kuanzisha makazi ya Pundamilia na wanyama wengine. Awamu ya kwanza ya kuhamisha pundamiliz 25 kutoka hifadhi ya taifa ya mikumi inatarajiwa kukamilika mwishoni mw mwaka huu. Hifadhi hiyo ni maarufu kwa wenyeji kama 'BUSTANI YA MUNGU'.
Aina mojawapo ya ua ambalo hupatikana katika hifadhi hiyo.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo, Pius Mzimbe (kushoto) akimuonyesha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) sehemu ya eneo lililochaguliwa ndani ya hifadhi hiyo kwa ajili ya kuanzisha makazi ya Pundamilia 25 watakaohamishwa kutoka Hifadhi ya Taifa ya Mikumi. Alisema kabla ya mwaka huu kuisha Pundamilia hao watakuwa wameshahamishiwa eneo hilo. Huo ni mkakati wa wizara na Serikali katika kuboresha vivutio vya utalii nchini ili kuongeza idadi ya watalii na mapato.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akisalimiana na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo alipowasili makao makuu ya hifadhi hiyo yaliyopo Makete mkoani Njombe jana.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akizungumza na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo makao makuu ya hifadhi hiyo yaliyopo Makete mkoani Njombe. Amewaaka watumishi hao kufanya kazi kwa bidii na ubunifu, kujiepusha na vitendo vya rusha, kuweka mikakati wa kudhibiti mifugo kuingia hifadhini na sio kusubiri iingie na kuanza kutangaza kuikamata au kuitaifisha, kupunguza malalamiko ya wananchi jirani na hifadhi hiyo, kuongeza idadi ya mapato ya hifadhi na kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akizungumza na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo. (Picha na Hamza Temba-Wizara ya Maliasili na Utalii)

ALICHOSEMA NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, JAPHET HASUNGA BAADA YA KUTEMBELEA MAPOROMOKO YA MTO KIMANI KATIKA PORI LA AKIBA MPANGA KIPENGELE


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa pili kushoto) akionyeshwa njia ya kuelekea kwenye maporomoko ya maji ya mto Kimani na Kaimu Meneja wa Pori la Akiba la Mpanga Kipengele, Stanslaus Odhiambo (katikati) alipotembelea maporomoko hayo katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe. Maporomoko hayo ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika pori hilo yana urefu wa mita zaidi ya 70. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa pili kushoto) akionyeshwa maporomoko ya maji ya mto Kimani na Kaimu Meneja wa Pori la Akiba la Mpanga Kipengele, Stanslaus Odhiambo (katikati) alipotembelea maporomoko hayo jana katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe. Maporomoko hayo ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika pori hilo yana urefu wa mita zaidi ya 70. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune kwenda eneo la maporomoko ya maji ya mto Kimani ambayo yapo ndani ya Pori la Akiba la Mpanga Kipengele katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe. Maporomoko hayo ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika pori hilo yana urefu wa mita zaidi ya 70
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) akiangalia maporomoko ya maji ya mto Kimani alipotembelea Pori la Akiba la Mpanga Kipengele katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe. Maporomoko hayo ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika pori hilo yana urefu wa mita zaidi ya 70.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa pili kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania, David Kanyata (kushoto) na baadhi ya wafanyakazi wa Pori la Akiba la Mpanga Kipengele alipotembelea  maporomoko ya maji ya mto Kimani ambayo yapo ndani ya pori hilo katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe. Maporomoko hayo ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika pori hilo yana urefu wa mita zaidi ya 70
Maporomoko ya Maji ya Mto Kimani ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika Pori la Akiba la Mpanga Kipengele katika Wilaya ya Makete mkoani Njombe. Maporomoko hayi yana urefu wa mita zaidi ya 70.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune wakiangalia moja fuvu la mnyamapori katika moja ya pango ambalo ambalo Chief Mkwawa alilitumia kujificha wakati wa vita na wakoloni alipotembelea Pori la Akiba la Mpanga Kipengele katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe. 
Picha ya pamoja. (Picha na Hamza Temba)

Sunday, December 3, 2017

IJUE BARABARA YA LAMI AMBAYO NI KIVUTIO CHA UTALII NCHINI, SERIKALI KUBORESHA MAZINGIRA YA KIVUTIO HICHO

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) akiongozwa na Meneja wa shamba la Miti Kawetire, Arnorld Shoo kukagua moja ya eneo katika shamba hilo ilipopita barabara ya lami ambayo ipo juu zaidi ya nyingine nchini ikiwa na urefu (Altitude) wa mita 2961 kutoka usawa wa bahari wakati wa zaira yake ya kikazi jana mkoani Mbeya. Alisema Serikali itaboresha mazingira ya eneo hilo ili yatumike kama kivutio cha utalii nchini.
Bofya kitufe cha PLAY kuangalia VIDEO

Na Hamza Temba, Mbeya
........................................................
Serikali imesema itaboresha mazingira ya kivutio cha utalii cha barabara ya lami ambayo ipo juu zaidi kutoka usawa wa bahari kuliko barabara zote nchini ili kupanua wigo wa vivutio vya utalii na kuongeza idadi ya watalii na mapato.

Hayo yameelezwa jana na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga baada ya kutembelea shamba la miti la Kawetire wilayani Mbeya na kujionea sehemu ya barabara ya lami inayopita katikati ya shamba hilo katika mlima Kawetire kwenye safu za milima ya Mbeya.

Eneo hilo la barabara hiyo ambayo hupitisha magari kutoka Jijini Mbeya kwenda katika Wilaya ya Chunya na Mikoa ya Singida na Tabora lina urefu (Altitude) wa mita 2961 kutoka usawa wa bahari katika Latitude 08’ 35 S na Longitude 33’ 25 E.

“Hatutaki ule utalii wa kutegemea wanyamapori pekee, hii sasa ni sehemu ya aina nyingine ya utalii ambayo ni lazima tuiboreshe tuweke kibao kizuri tuweke mazingira mazuri pamoja na kukitangaza ili watanzania na watalii kutoka nje waweze kutembelea hapa,” alisema Hasunga.

Alisema ili kufikia lengo liliwekwa na Serikali la kuongeza idadi ya watalii kufikia milioni mbili mwaka 2020 na milioni 8 mwaka 2025 vivutio vyote vya utalii vilivyopo nchini vitatambuliwa, kuimarishwa na kuviwekea miundombinu itakayowavutia watalii kuvitembelea.

Aidha aliuagiza uongozi wa shamba hilo kushirikiana na wakala wa huduma za barabara –Tanroads katika kuboresha mazingira yanayozunguka eneo hilo ikiwa ni pamoja na kuweka bango la kisasa la kutambulisha eneo hilo, kujenga bustani na maeneo rafiki ya kupumzikia kwa ajili ya kuwavutia watalii kutembelea eneo hilo na kupiga picha.

Mbali na kivutio hicho aliuagiza uongozi wa shamba hilo kutobomoa majengo ya kale yaliyotumiwa na wakoloni katika shamba hilo na badala yake yatumike kwenye utalii wa mambo ya kale sambamba na utalii wa misitu ya kupandwa inayopatikana pia katika shamba hilo.

Hata hivyo alisema kupitia mradi wa REGROW wa kuendeleza utalii kanda ya kusini Serikali imepokea mkopo wa masharti nafuu wa dola za Kimarekani milioni 150 sawa za zaidi ya bilioni 340 za kitanzania kutoka benki ya dunia kwa ajili ya kusaidia kuboresha miundombinu ya vivutio vya ukanda huo.

Kwa upande wake Meneja wa shamba hilo, Arnorld Shoo alisema eneo hilo la barabara limekuwa ni kivutio cha kipekee cha utalii katika shamba hilo ambapo pia hupata mapato kupitia watu na vikundi mbalimbali ikiwemo wanakwaya na wanafunzi ambao hufika eneo hilo kwa ajili ya kupiga picha za kumbukumbu.  
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) na Meneja wa shamba la Miti Kawetire, Arnorld Shoo wakiangalia bango linaloonesha eneo katika shamba hilo ilipopita barabara ya lami ambayo ipo juu zaidi ya nyingine nchini ikiwa na urefu (Altitude) wa mita 2961 kutoka usawa wa bahari wakati wa zaira yake ya kikazi jana mkoani Mbeya. Alisema Serikali itaboresha mazingira ya eneo hilo ili yatumike kama kivutio cha utalii nchini.

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI, JAPHET HASUNGA ATOA MIEZI MITATU WANANCHI WALIPWE FIDIA WAPISHE ENEO LA HIFADHI

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) akizungumza na watumishi wa Pori la Akiba Mpanga Kipengele alipotembelea makao makuu ya pori hilo jana katika Wilaya ya Wangin'ombe mkoani Njombe. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania, David Kanyata na Kaimu Meneja wa pori hilo, Stanslaus Odhiambo.

Na Hamza Temba, Mbarali - Mbeya
.......................................................................................
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga ametoa miezi mitatu kwa uongozi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA kukamilisha malipo ya fidia ya shilingi milioni 771.6 kwa kaya 308 za Kitongoji cha Machimbo ili ziweze kupisha eneo la hifadhi katika Pori la Akiba la Mpanga Kipengele.

Naibu Waziri Hasunga ametoa agizo hilo jana katika mkutano wa hadhara baada kutembelea kitongoji hicho katika Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya wakati wa ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kutatua migogoro kwenye maeneo ya hifadhi mkoani humo.

“Kaimu Mkurugenzi (TAWA) kama unavyoona wananchi hawa wapo tayari kupisha eneo hili la hifadhi, wanachosubiri ni malipo yao ya fidia, naagiza mpaka ifikapo mwezi Februari mwakani (2018) wawe wameshalipwa fidia zao, na ikiwezekana hata ndani ya mwezi Januari wawe wameshalipwa,”alisema Hasunga.

Awali akiwasilisha taarifa ya pori hilo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, David Kenyata alisema wakati pori hilo linaanzishwa mwaka 2002 kwa Tangazo la Serikali Na. 483 wananchi wa kitongoji hicho na vitongoji vingine walikuwa ndani ya eneo hilo la hifadhi.

Alisema mazungumzo yalishafanywa kupitia vikao halali vya uongozi wa viijiji na halmashauri ambapo wananchi hao waliridhia kulipwa fidia ili kuachia maeneo hayo ya hifadhi.

Alisema sababu kubwa ya kuanzishwa kwa pori hilo ni pamoja na kuhifadhi vyanzo vya maji yanayotiririka kwenda mto Ruaha na kwenye mabwawa ya kidatu na mtera yanayotumika kuzalisha umeme nchini.

Akizungumzia malipo ya fidia kwa vijiji na vitongoji vilivyopo ndani ya hifadhi hiyo alisema kijiji kimoja kilishalipwa mwaka 2015 jumla ya shlingi milioni 500 na vijiji vilivyosalia vitalipwa kwa awamu ambapo kwa mwaka wa fedha 2017/2018 fedha zimetengwa kwa ajilia ya kulipa wananchi wa kitongaoji cha Machimbo ambao tayari walishafanyiwa uthamini mwaka 2015.

Awali akizungumza na watumishi wa Pori hilo katika ofisi zao zilizopo Wilaya ya Wanging’ombe mkoani Njombe, Naibu Waziri Hasunga aliwataka watumishi hao kuongeza nguvu na ubunifu kwenye kuzuia mifugo isiiingie hifadhini badala ya kusubiri iingie ndipo waikamate na kuitoza faini au kuitaifisha.

“Nyie ni watalaamu, tumieni mbinu na ubunifu wenu wote muhakikishe mnazuia mifugo isiingie hifadhini, sitaki kusikia mmekamata au mmetaifisha mifugo hifadhini, hiyo siyo sifa, sifa ni kuzuia isiingie kabisa, na nitawapima kwa hilo,” alisema Hasunga.

Aidha aliwataka watumishi hao kuimarisha uhifadhi shirikishi, kujiepusha na vitendo vya rushwa, kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma na kuongeza ubunifu utakaowezesha ongezeko la mapato ya Serikali.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri huyo aliwatembelea wananchi wanaojishughulisha na kilimo cha umwagiliaji katika Skimu ya Igomelo ambao awali waligomea zoezi la uwekwaji wa vigingi vya mpaka kwenye eneo lao na Pori la Akiba la Mpanga Kipengele kwa hofu ya kupoteza maeneo hayo.

Hata hivyo baada ya kuwaelimisha kuwa lengo la zoezi hilo ni kuiwezesha Serikali kufanya uamuzi wa mwisho wa kumaliza migogoro ya ardhi iliyodumu kwa muda mrefu baina ya vijiji na maeneo ya hifadhi nchini wananchi hao walielewa na kuahidi kushirikiana na mamlaka husika kukamilisha zoezi hilo kwa muda uliopangwa.  

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa Pori hilo, Stanslaus Odhiambo alisema pori hilo linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uwepo wa vijiji na vitongoji 13 ndani ya pori hilo, uchomaji moto maeneo ya hifadhi, ukataji miti hovyo, ujangili na uhaba wa vitendea kazi.

Pori la Akiba la Mpanga Kipengele lina ukubwa wa Kilometa za mraba 1574.25 katika wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya na Wilaya za Wanging’ombe na Makete Mkoani Njombe.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (waliokaa mbele katikati) akizungumza na watumishi wa Pori la Akiba Mpanga Kipengele alipotembelea makao makuu ya pori hilo jana katika Wilaya ya Wangin'ombe mkoani Njombe.
Baadhi ya watumishi wa Pori la Akiba Mpanga Kipengele wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili, Japhet Hasunga (hayuko pichani).
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa pili kushoto) akisalimiana na Kaimu Meneja wa Pori la Akiba la Mpanga Kipengele, Stanslaus Odhiambo muda mfupi baada ya kuwasili makao makuu ya pori hilo jana katika Wilaya ya Wanging'ombe mkoani Njombe.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akizungumza na wananchi wa Kitongoji cha Machimbo wapatao kaya 308 katika Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya jana ambapo aliiagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania kuwalipa fidia ya shilingi milioni 771.6  kabla ya Februari, 2018 ili wapishe eneo la Hifadhi katika Pori la Akiba la Mpanga Kipengele.
Baadhi ya wananchi wa kitongoji cha Machimbo wapatao kaya 308 katika Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga ambaye aliwatembelea jana na kuagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania iwalipe fidia ya shilingi milioni 771.6 kabla ya Februari, 2018 ili wapishe eneo la Hifadhi katika Pori la Akiba la Mpanga Kipengele alipowatembelea.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) akizungumza na wananchi wanaojishughulisha na kilimo cha umwagiliaji katika Skimu ya Igomelo, wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya ambao waligomea zoezi la uwekwaji wa vigingi vya mpaka kwenye eneo lao na Pori la Akiba la Mpanga Kipengele kwa hofu ya kupoteza maeneo hayo. Baada ya kuwaelimisha wananchi hao walikubali kutoa ushirikiano kwa mamlaka husika ili kukamilisha zoezi hilo.

Saturday, December 2, 2017

DK. KIGWANGALLA ATOA SIKU 30 KWA WAMILIKI WA MAGOGO YALIYOKAMATWA BANDARINI DAR KUJITOKEZA

Na Mwandishi wetu-Dar es Salaam
.............................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Kigwangalla, amefanya ziara ya kushtukiza bandari ya Dar es Salaam ambapo ameagiza Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii atangaze kujitokeza kwa wamiliki wa magogo 938 yaliyokaa bandarini kwa zaidi ya miaka 10. Kama wamiliki wasipojitokeza, magogo hayo yatakuwa mali ya Serikali.
Aidha Dkt. Kigwangalla ametoa siku 30 kwa wamiliki wa makontena 55 yanayodaiwa kuingizwa nchini kutoka Zambia kujitokeza na kuwasilisha nyaraka zao zenye kuthibitisha kama kweli yalivunwa nchini Zambia na yalivunwa wapi na kwa vibali gani vya nchi hiyo. Pia kufuatilia nyaraka za kuingiza ndani ya Tanzania. Ameagiza kitengo cha kuzuia ujangili kifuatilie kubaini uhalisia na uhalali wa taarifa hizo vinginevyo yatakuwa mali ya Serikali. 

Dkt. Kigwangalla amefanya ziara ya kushtukiza bandarini hapo kufuatia uwepo wa taarifa za uvunaji holela wa magogo nchini, ambapo kuna taarifa kuwa kuna wafanyabiashara wa kigeni wanagawa vifaa vya kuvunia bure kwa ahadi ya kuuziwa mzigo na wahusika, pia uwepo wa taarifa kwamba kuna baadhi ya watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wanatoa vibali na kugonga nembo kinyume cha taratibu za kisheria. Hali inayotishia usalama wa raslimali adimu ya misitu yetu ya asili. 

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangallaakitoa maagizo kwa uongozi wa bandari ya TPA.Baadhi ya magogo hayo yaliyokutwa katika makontena bandarini hapo.Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla wakiwa katika eneo la bandari ya nchi kavu ya Malawi Cargo. wakati wa kukagua magogo hayo.Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua baadhi ya mbao zilizokutwa bandarini hapo katika eneo la Malawi Cargo.Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua baadhi ya mbao zilizokutwa bandarini hapo katika eneo la Malawi Cargo.Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akionyeshwa nyaraka ya idadi ya makontena  katika eneo la Malawi Cargo.Zoezi la ukaguaji likiendeleaBaadhi ya magogo yaliyokutwa bandarini hapo.

Friday, December 1, 2017

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI, JAPHET HASUNGA AFUNGUA KITUO CHA MAFUNZO YA MISITU NA UCHAKATAJI WA MAGOGO MKOANI IRINGA

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) na Balozi wa Finland nchini, Mhe. Peka Huka wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa Kituo cha Mafunzo ya Misitu na Uchakataji wa Magogo kilichoanzishwa mwezi  Desemba, 2016 katika mji wa Mafinga, Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa chini ya ufadhili wa Serikali ya Finland katika hafla iliyofanyika jana mkoani humo.

Na Hamza Temba-WMU-Iringa
........................................................................
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga amefungua Kituo cha Mafunzo ya Misitu na Uchakataji wa Magogo ambacho kimeanzishwa katika Mji wa Mafinga, Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa chini ya ufadhili wa Serikali ya Finland kupitia mradi wa Panda Miti Kibiashara.

Akizungumza kwenye hotuba yake ya ufunguzi wa kituo hicho jana mjini hapa, Naibu Waziri Hasunga ameishukuru Serikali ya Finland kwa msaada huo na misaada mingine ambayo imekuwa ikiitoa katika kuimarisha sekta ya Misitu nchini toka miaka ya 1970s.  

Alisema lengo la kituo hicho ni kusaidia kutoa elimu kwa vitendo na ujuzi kwa makundi mbalimbali ambayo yapo katika mnyororo wa kuongeza thamani ya mazao ya misitu ikiwemo watu binafsi, viwanda vya misitu na taasisi za Serikali kuanzia hatua za mwanzo za upandaji wa miche ya miti hadi kwenye hatua za mwisho za uchakataji wa magogo.

Aidha, kutokana na kituo hicho kuwa chini ya mradi huo, Naibu Waziri Hasunga amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Meja Jenerali Gaudence Milanzi kuangalia uwezekano wa kukiweka kituo hicho chini ya Wizara yake ili mafunzo yanayotolewa yawe endelevu hata kama mradi husika utafikia ukiongoni.

Pia, ameagiza mitaala ya kituo hicho ipitiwe na isajiliwe kupitia Mfumo wa Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi– VETA ili yaweze kutambulika na wahitimu wapewe vyeti kulingana na mahitaji ya soko katika sekta ya viwanda vya misitu nchini.

Katika hatua nyingine amemuagiza Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki wa Wizara hiyo, Dk. Ezekiel Mwakalukwa kukagua viwanda vyote vya misitu nchini kwa ajili ya kujiridhisha kama vinakidhi vigezo vilivyowekwa na wizara ikiwemo kuwa na wafanyakazi wenye ujuzi unaostahili.

Alisema uwepo wa kituo hicho cha mafunzo utawezesha viwanda hivyo kuwapatia mafunzo kwa vitendo wafanyakazi wake ambao hawana vigezo ili waweze kukidhi vigezo na ujuzi stahiki ikiwemo kuwa na Fundi Misumeno, Fundi Mwendesha Mashine ya Kuchakata Magogo na Fundi Mitambo.

Alitoa wito kwa wananchi wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini pamoja na maeneo mengine nchini kujiunga na kituo hicho waweze kupata mafunzo ya kitaalamu na ujuzi wa kuotesha miti kwa njia za kisasa iweze kuzalisha mbao na samani zenye ubora zaidi.

Kwa upande wa Balozi wa Finland, Mhe. Peka Huka amesema nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuboresha sekta ya misitu nchini iweze kutoa mchango chanya kwa jamii na taifa ujumla.

Naye Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi amesema kituo hicho kitatoa fursa pana ya mafunzo kwa makundi mbalimbali katika sekta ya misitu nchini tofauti na vituo vingine ambavyo huitaji vigezo mbalimbali vya kitaaluma kujiunga. Alisema maelekezo yote yaliyotolewa na Naibu Waziri Hasunga yatafanyiwa kazi ili kuimarisha sekta hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema Serikali ya Mkoa wake imefurahishwa kwa kuanzishwa kwa kituo hicho cha mafunzo katika mkoa wake na kuahidi kushirikiana na mamlaka zingine kukilinda na kukiendeleza. Alisema katika maeneo aliyopanga kumpeleka Mhe. Rais kwenye ziara zake mkoani humo ya kwanza itakuwa katika kituo hicho.

Toka kuanzishwa kwake mwezi Desemba mwaka jana, 2016 mpaka sasa kituo hicho cha mafunzo kimeshaandaa na kuendesha zaidi ya kozi 20 kwa ajili ya usimamizi wa misitu, afya na usalama kazini, huduma ya kwanza, ujasiriamali na ufundishaji. Wastani wa muda wa mafunzo yanayotolewa kituoni hapo ni siku nne ambapo jumla ya washiriki 400 wameshapatiwa mafunzo hayo huku wanawake ikiwa ni asilimia 35.

Aidha kwa sasa jumla ya wanafunzi 40 kutoka Chuo cha Misitu Olmotonyi na Chuo cha Viwanda vya Misitu Moshi wanapatiwa mafunzo kwa vitendo katika kituo hicho.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akipanda mti wa kumbukumbu muda mfupi baada ya kufungua rasmi Kituo cha Mafunzo ya Misitu na Uchakataji wa Magogo kilichoanzishwa katika mji wa Mafinga, Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa chini ya ufadhili wa Serikali ya Finland. Kutoka kushoto wa tatu ni Balozi wa Finland nchini, Mhe. Peka Huka, Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza. 
Balozi wa Finland nchini Tanzania, Mhe. Peka Huka akipanda mti wa kumbukumbu muda mfupi baada ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) kufungua rasmi Kituo cha Mafunzo ya Misitu na Uchakataji wa Magogo kilichoanzishwa mwezi Desemba, 2016 katika mji wa Mafinga, Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa chini ya ufadhili wa Serikali ya Finland. Kutoka kulia wa tatu ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Christina Mndeme na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi jana muda mfupi baada ya kufungua rasmi Kituo cha Mafunzo ya Misitu na Uchakataji wa Magogo kilichoanzishwa mwezi  Desemba, 2016 katika mji wa Mafinga, Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa chini ya ufadhili wa Serikali ya Finland. Wengine pichani ni Balozi wa Finland nchini, Mhe. Peka Huka (wa pili kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Christina Mndeme. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (wa pili kushoto) ambaye alikuwa mgeni rasmi akiwasilisha hotuba  yake wakati wa hafla hiyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi (kushoto) akitoa salamu za shukurani muda mfupi jana baada ya Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Japhet Hasunga (wa tatu kushoto) kufungua rasmi Kituo cha Mafunzo ya Misitu na Uchakataji wa Magogo kilichoanzishwa mwezi Desemba, 2016 katika mji wa Mafinga, Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa chini ya ufadhili wa Serikali ya Finland. Wengine kushoto kwake ni Balozi wa Finland nchini Tanzania, Mhe. Peka Huka, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Christina Mndeme. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akimsikiliza Mshauri wa Masuala ya Misitu kutoka sekta binafsi, Sangito Sumari wakati akitoa maelezo juu ya miche ya kisasa ya miti iliyoboreshwa muda mfupi baada ya kufungua rasmi Kituo cha Mafunzo ya Misitu na Uchakataji wa Magogo kilichoanzishwa mwezi  Desemba, 2016 katika mji wa Mafinga, Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa chini ya ufadhili wa Serikali ya Finland. Kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza na Balozi wa Finland nchini, Mhe. Peka Huka. 
 Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk. Ezekiel Mwakalukwa (kulia) akiongoza hafla hiyo ya ufunguzi.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (wa pili kulia) akiangalia mbao zinavyoandaliwa katika moja ya karakana ya kituo hicho. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mhe. Christina Mndeme (wa tatu kulia).
Baadhi ya wanafunzi kutoka Chuo cha Misitu Olmotonyi na Chuo cha Viwanda vya Misitu Moshi (wanaopunga mikono) ambao wanapatiwa mafunzo kwa vitendo katika kituo hicho.

NATIONAL GEOGRAPHIC TRAVELER HAS NAMED RUAHA NATIONAL PARK AS AMONG THE BEST PLACES YOU NEED TO VISIT IN 2018

National Geographic Traveller has named Ruaha National Park, Tanzania as among the best places in the World you will need to visit in 2018 (Best Trips 2018).

WHY GO NOW: Help protect endangered African lions.

Ruaha, Tanzania’s largest park, is home to about one-tenth of the world’s endangered African lions. Sustainable tourism initiatives help visitors see the big cats—some grouped in prides of 30 or more—and support wildlife preservation in and around the park.

FUN FACT: The African lion population has decreased by 90% over the last century.

Other places named includes;

Harar, Ethiopia
Jujuy Province, Argentina
Tbilisi Georgia
Sydney Australia
Oaxaca Mexico
Vienna Austria
North Shore, Oahu, Hawaii
Malmö, Sweden
Jordan, Trail
Dublin, Ireland
Madagascar
Santiago, Chile
Phnom Penh, Cambodia
Cleveland, Ohio
Tétouan, Morocco
Seoraksan NationalPark, South Korea
Albania
San Antonio, Texas
Labrador  Canada
Friesland, Netherlands