slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Friday, February 9, 2018

MKUTANO WA MAWAZIRI WA SEKTA YA MALIASILI NA MAZINGIRA WA JUMUIYA YA AFRIKA YA MASHARIKI WAFANYIKA LEO JIJINI ARUSHA

 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba wakati wa mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Mazingira wa Nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliohitimishwa leo katika ukumbi wa EAC jijini Arusha. Mkutano huo ulilenga kujadili na kusaini makubaliano mbalimbali ya namna bora ya kusimamia sekta hizo katika nchi wanachama. 
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba (kulia) akisaini baadhi ya makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Mazingira wa Nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliohitimishwa leo katika ukumbi wa EAC jijini Arusha. Mkutano huo ulilenga kujadili na kusaini makubaliano mbalimbali ya namna bora ya kusimamia sekta hizo katika nchi wanachama. Wanaoshuhudia ni Mawaziri wa Mazingira kutoka Uganda na Kenya.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia), Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba (wa pili kulia) na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Bi. Katerina Rangnitt wakiangalia baadhi ya michoro ya katuni za kuhamasisha uhifadhi wa mazingira muda mfupi baada mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Mazingira wa Nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliohitimishwa leo katika ukumbi wa EAC jijini Arusha. Mradi huo ya katuni unafadhiliwa na Serikali ya Sweden kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba wakimsikiliza mmoja ya wachora katuni za kuhamasisha uhifadhi wa mazingira muda mfupi baada mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Mazingira wa Nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliohitimishwa leo katika ukumbi wa EAC jijini Arusha. Mkutano huo ulilenga kujadili na kusaini makubaliano mbalimbali ya namna bora ya kusimamia sekta hizo katika nchi wanachama. 
 Picha ya pamoja ya baadhi ya wajumbe wa mkutano huo.
(PICHA ZOTE NA HAMZA TEMBA-WMU)

Thursday, February 8, 2018

WIZARA YA MALIASILI, ARDHI NA TAMISEMI KUAMUA HATMA YA MGOGORO WA PORI LA AKIBA MKUNGUNERO – DK. KIGWANGALLA



Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikengwa, Mohammed Tabahi aliyekuwa akimunesha mpaka wa kijiji hicho na Pori la Akiba Mkungunero wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.

Na Hamza Temba - Kondoa, Dodoma
..........................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla jana tarehe 7 februari, 2018 ametembelea Pori la Akiba Mkungunero katika Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma na kuwataka wananchi wanaozunguka pori hilo kusubiri uamuzi wa Serikali  utakaoshirikisha Wizara yake,  Wizara ya Ardhi na Tamisemi katika kujibu maombi yao ya kutaka kupewa sehemu ya ardhi katika pori hilo kwa ajili ya kuendesha shughuli za kibinadamu.

Dk. Kigwangalla ambaye aliongozana na Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo, alitembelea vijiji vinne vya Ikengwa, Keikei Tangini, Keikei na Kisondoko na kufanya mikutano ya hadhara kwa ajili ya kujiridhisha na  kujifunza juu ya mgogoro uliopo baina ya vijiji hivyo na Pori la Akiba Mkungunero.

"Nimefika hapa leo kujifunza juu ya mgogoro huu, nimejionea hali halisi lakini pia nina maelezo ya wataalamu ambayo yapo kwenye maandishi naomba niende nikayasome, niyatafakari ili niweze kushauriana na wenzangu na mwisho wa siku tuweze kuja na suluhu ya namna ya kuondokana na changamoto ambazo zimekuwepo.

"Niwaombe sana wakati Serikali inaendelea kutafuta suluhu ya mgogoro huu ni vema tukafuata sheria zilizopo, tuzingatie mipaka iliyowekwa ili tusiingie kwenye migogoro, lakini kwa sasa siwezi kwa namna yeyote ile kutamka neno la kujibu maombi ya mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji na wananchi yaliyotolewa hapa leo.

"Kama Serikali tutakaa, Wizara yangu, Wizara ya Ardhi na Tamisemi ili tujue kiini cha mgogoro huu tufanye uamuzi kuwa ni maeneo gani yaongezwe katika hifadhi kwa ajili ya wananchi au ni vitongoji vipi vifutwe, tutaleta majibu, na jambo hili tutalifanya kwa uadilifu mkubwa bila kumuonea mtu ili kumaliza mgogoro huu," alisisitiza Dk. Kigwangalla.

Awali akimkaribisha Waziri huyo kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Ikengwa, Mbunge wa jimbo hilo, Dk. Ashatu Kijaji alisema kutokana na ukweli kuwa Serikali ya awamu ya tano inasikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi, ni vema Waziri huyo akatumia hekima na kuangalia uwezekano wa kuwapa wananchi hao Kilomita 12 za mraba kutoka kwenye hifadhi hiyo kwa ajili ya kuendesha shughuli zao za kibinadamu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikengwa, Mohammed Tabahi alisema mgogoro baina ya vijiji hivyo na Pori la Akiba Mkungunero ulinza mwaka 2006 kufuatia zoezi la kuanzishwa kwake  pamoja na lile na uwekagi wa vigingi vya mpaka  na vijiji jirani kutoshirikisha wananchi na viongozi wa halmashauri za vijiji hoja ambayo ilipigwa na Meneja wa Pori hilo, Emannuel Bilaso

Aidha alisema wananchi wa vijiji hivyo wanakabiliwa na uhaba wa maeneo ya kilimo na ufugaji, hivyo akamuomba Waziri huyo pamoja na Serikali kwa ujumla kutumia busara  kuwamegea wananchi wa vijiji hivyo eneo la Kilomita 12 za mraba kwa ajili ya shughuli za kilimo na ufugaji.

Naye Meneja wa Pori hilo, Emannuel Bilaso alisema Pori la Akiba Mkungunero lilianzishwa kwa tangazo la Serikali Na. 307 la mwaka 1996 baada ya kupandishwa hadhi kutoka Pori Tengefu. Alisema mchakato wa kupandisha hadhi pori hilo ulishirikisha wananchi na viongozi wa vijiji na wilaya ambapo mihutasari mbalimbali ilisainiwa.

Alisema pori hilo linakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazochochea mgororo huo ikiwemo kijiji kimoja cha Kisondoko  kusajiliwa kimakosa ndani ya hifadhi hiyo pamoja na malalamiko mbalimbali ya wananchi kuwa hawakushirikishwa kwenye uanzishwaji wa pori pamoja na madai mengine kuwa pori hilo limeingilia mipaka ya vijiji hivyo.

Pori la Akiba Mkungunero ambalo lina ukubwa wa Kilimita za Mraba 557.9 lina umuhimu mkubwa kiuchumi na kiikolojia kwa kuwa ni chanzo muhimu cha mto Tarangire ambao ni uhai wa hifadhi ya Taifa ya Tarangire na ikolojia nzima ya ziwa Manyara. Pori hilo pia ni sehemu ya mapito na mazalia ya wanyamapori pamoja na makazi ya wanyamapori adimu duniani.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kondoa muda mfupi baada ya kuwasili wilayana humo jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa ramani ya Pori la Akiba Mkungunero na Mrasimu Ramani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, Peter Nyange (kulia) wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa mipaka ya Pori la Akiba Mkungunero na Mrasimu Ramani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, Peter Nyange (kulia) wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa tatu kulia) akiteja jambo na Meneja wa Pori la Akiba Mkungunero, Emannuel Bilaso wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pili kulia) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikengwa, Mohammed Tabahi wakati wa ziara yake ya kikazi jana katika Pori la Akiba Mkungunero Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akipokea mabango ya malalamiko kutoka kwa wananchi wa kijiji cha Kisondoko kuhusu Pori la Akiba Mkungunero na vijiji jirani wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kisondoko wilayani Kondoa jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa mipaka ya Pori la Akiba Mkungunero na mmoja wa wahifadhi wa Pori hilo wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.

Wednesday, February 7, 2018

SERIKALI ILIVYODHAMIRIA KUFUNGUA UTALII WA KANDA YA KUSINI


Na Hamza Temba - Dodoma
..........................................................
Serikali imeanza utekelezaji wa mkakati wa kupanua wigo wa vivutio vya utalii nchini unaohusisha upanuzi wa maeneo ya kijeografia yenye vivutio pamoja na mazao ya utalii ili sekta hiyo ichangie zaidi kwenye pato la taifa na kuondoa umaskini katika jamii.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla wakati akijibu hoja mbalimbali za wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii katika kikao cha Bunge kinachoendelea mjini Dodoma.

Alisema kwa upande wa mkakati wa kupanua jeografia ya vivutio vya utalii nchini Serikali itafungua utalii wa ukanda wa kusini kwa kuboresha vivutio na miundombinu ambapo tayari imesaini mkataba wa mkopo nafuu kutoka benki ya dunia wa milioni 150 za kimarekani sawa na zaidi ya Shilingi bilioni 340 za kitanzania kwa ajili ya mradi wa REGROW ambao utasimamia maliasili na kuendeleza utalii wa ukanda wa kusini.

Alisema kupitia mradi huo jumla ya viwanja vya ndege 15 vitaboreshwa ndani ya Pori la Akiba la Selous na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha pamoja na uwanja wa ndege wa Nduli uliopo mjini Iringa. Maeneo mengine yatakayoboreshwa katika hatua ya kwanza ya utekelezaji wa mradi huo ni Hifadhi ya Taifa ya Udzungwa na Mikumi.

"Mradi huo utaboresha pia usafiri wa reli kwa kuimarisha kituo cha Matambwe ambacho ni kitovu cha utalii katika Pori la Akiba la Selous",. Alisema Dk. Kigwangalla.

Akizungumzia upanuzi wa mazao ya utalii, alisema sekta hiyo kwa muda mrefu imekuwa ikitegemea zaidi utalii wa wanyamapori huku ukiegemea zaidi katika ukanda wa kaskazini kwa zaidi ya asilimia 90.

Alisema kwa sasa Serikali itapanua wigo wa mazao hayo ya utalii ambapo mwezi Septemba kila mwaka utakuwa mwezi maalum wa maadhimisho ya urithi wa Tanzania (Urithi Festival) kwa ajili kuimarisha utalii wa kiutamaduni na kuhamasisha utalii wa ndani.

Alisema Serikali kupitia Wizara yake itaimarisha pia utalii wa fukwe na utalii wa mikutano.

Awali Dk. Kigwangalla alisema sekta ya Utalii ina mchango mkubwa katika uchumi wa taifa ambapo huchangia asilimia 17.6 ya pato la taifa, asilimia 25 ya mapato yote ya fedha za kigeni na asilimia 12 ya ajira zote nchini.

Alisema pamoja na mafanikio hayo sekta hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo uvamizi kwenye maeneo ya hifadhi na kuegemea zaidi kwenye vivutio vya ukanda wa kaskazini huku vivutio vya kanda nyingine vikiwa havichangii ipasavyo kwenye pato la taifa.

Tuesday, February 6, 2018

DK. KIGWANGALLA AFANYA MAZUNGUMZO NA MUWAKILISHI WA BENKI YA DUNIA NCHINI KWA AJILI YA KUBORESHA MRADI WA REGROW

Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akizungumza na Muwakilishi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania, Daniel Mira-Salama ambaye pia ni Mratibu wa Mradi wa REGROW kwa ajili ya kusimamia maliasili na kuendeleza utalii wa Ukanda wa Kusini ofisini kwake mjini Dodoma leo Januari 06, 2018 ambapo wamejadili mambo mbalimbali ya kuboresha mradi huo wakati wa utekelezaji. 

Na Hamza Temba-WMU
.......................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla leo Februari 6, 2018 ofisini kwake mjini Dodoma amekutana na kufanya mazungumzo na Muwakilishi wa Benki ya Dunia, Daniel Mira-Salama ambaye pia ni Mratibu wa Mradi wa Kusimamia Maliasili na Kuendeleza Utalii wa Ukanda wa Kusini -REGROW unaofadhiliwa kwa mkopo na benki hiyo ambapo wamejadili mambo mbalimbali ya kuboresha mradi huo wakati wa utekelezaji.

Miongoni mwa mambo waliyojadili ni kuboresha miundombinu ya barabara kuunganisha maeneo ya vivutio na miji ya ukanda huo pamoja na viwanja vya ndege ndani ya hifadhi viwe na hadhi na ubora wa kutua ndege kubwa ikiwemo za Air Tanzania. 


"Nawapongeza kwa mradi huu ambao ni mzuri sana kwenye uhifadhi lakini una mapungufu kidogo kwenye biashara ya utalii jambo ambalo ni muhimu kuangaliwa ili uwe na tija zaidi kwa jamii na taifa kwa ujumla" alisema Dk. Kigwangalla.



Alimuomba mratibu huyo kuona namna ya kubadilisha vipengele vya utekelezaji wa mradi huo ili uweze kuwa na tija zaidi hususan suala la miundombinu ya kuunganisha hifadhi mbalimbali za ukanda huo na miji ili kurahisisha usafiri wa kufikia vivutio hivyo kwa muda mfupi na kwa wakati.



Kwa upande wake mratibu huyo alisema jambo hilo linajadilika na kwamba uendelezaji wa maeneo hayo ni mtambuka ukihusisha Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ambazo nazo zimeahidi kuboresha miundombinu ya maeneo hayo.




Mradi wa REGROW unatarajiwa kuzinduliwa rasmi tarehe 12 Februari mwaka huu Mjini Iringa na Mhe. Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan. Mwezi Agosti mwaka jana Serikali ya Tanzania ilisaini mkopo wa masharti nafuu wa Dola za Kimarekani Milioni 150 sawa na takriban bilioni 340 za Tanzania kwa ajili ya kuendeleza mradi huo.
Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangalla (katikati) akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Muwakilishi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania, Daniel Mira-Salama ambaye pia ni Mratibu wa Mradi wa REGROW kwa ajili ya kusimamia maliasili na kuendeleza utalii wa Ukanda wa Kusini ofisini kwake mjini Dodoma leo Januari 06, 2018 ambapo wamejadili mambo mbalimbali ya kuboresha mradi huo wakati wa utekelezaji. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Aloyce Nzuki. 
Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akimsikiliza Muwakilishi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania, Daniel Mira-Salama ambaye pia ni Mratibu wa Mradi wa REGROW kwa ajili ya kusimamia maliasili na kuendeleza utalii wa Ukanda wa Kusini ofisini kwake mjini Dodoma leo Januari 06, 2018 ambapo wamejadili mambo mbalimbali ya kuboresha mradi huo wakati wa utekelezaji. 
Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akiagana na Muwakilishi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania, Daniel Mira-Salama ambaye pia ni Mratibu wa Mradi wa REGROW kwa ajili ya kusimamia maliasili na kuendeleza utalii wa Ukanda wa Kusini ofisini kwake mjini Dodoma leo Januari 06, 2018 baada ya kujadili mambo kadhaa ya kuboresha mradi huo wakati wa utekelezaji. Katikati ni Mratibu wa mradi huo kutoka Tanzania, Someni Mteleka. (PICHA NA HAMZA TEMBA-WMU)

KATIKA KIPINDI CHA UONGOZI WANGU SITAJIBU MAOMBI YA KUFUTA MAENEO YA HIFADHI KWA AJILI YA MATUMIZI MENGINE - DK. KIGWANGALLA

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangallah, (wa pili kulia) na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Japhet Hasunga (wa nne kulia) na viongo wakiruka viunzi wakati walipotembelea jana ili kujiridhisha kabla ya kutoa maamuzi katika eneo la msitu wa hifadhi wa Kihesa Kilolo ambao umeombwa na uongozi wa mkoa wa Iringa kufutwa ili kujenga mji mpya wa kitalii katika mkoa huo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangallah akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Ushauri wa Misitu ambao alikutana nao kwa mara ya kwanza tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo katika kikao cha tatu cha kamati hiyo kilichofanyika jana mkoani Iringa.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangallah,( wa pili kulia) Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Japhet Hasunga ( wa pili kushoto) wakiwa wameambatana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza (katikati) wakipatiwa maelezo na Mkuu wa Idara ya mipango miji wa Halmashauri ya Iringa, Wilberd Mtongani ( wa tatu kushoto) wakati walipotembelea eneo la msitu wa hifadhi wa Kihesa Kilolo ili kujiridhisha kabla ya kutoa maamuzi ya kuhaulisha eneo hilo. Wengine ni Watalaamu ni wataalamu kutoka ofisi ya Mkoa pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Ushauri wa Misitu.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangallah,( wa tatu kulia) Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Japhet Hasunga ( wa pili kushoto) wakiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Ushauri wa Misitu, Prof. Shabani Chamshama (wa kwanza kushoto) wakipatiwa maelezo na Afisa mipango miji wa Halmashauri ya Iringa, Wicliph Benda ( wa tatu kushoto) wakati walipotembelea eneo la msitu wa hifadhi wa Kihesa Kilolo ili kujiridhisha kabla ya kutoa maamuzi ya kuhaulisha eneo hilo. Wengine ni Watalaamu ni wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa.
Naibu Waziri wa Wizara Japhet Hasunga ( wa kwanza ) akiwa ameambtana na wataalam kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa wa Iringa wakiruka viunzi wakati alipotembelea jana ili kujiridhisha kabla ya kutoa maamuzi katika eneo la msitu wa hifadhi wa Kihesa Kilolo ambao umeombwa na uongozi wa mkoa wa Iringa kufutwa ili kujenga mji mpya wa kitalii katika mkoa huo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangallah,( wa pili kushoto) akiwa pamoja na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Japhet Hasunga ( wa tatu kushoto) wakioneshwa ramani ya eneo la msitu wa hifadhi wa Kihesa Kilolo na Mkuu wa Idara ya mipango miji wa Halmashauri ya Iringa Wilberd Mtongani ( wa kwanza kulia) wakati 2 walipotembelea eneo hilo kujiridhisha kabla ya kutoa maamuzi ya kuhaulisha ili kujenga mji mpya wa kitalii mkoani Iringa.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangallah,( wa kwanza kulia ) akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki Dkt. Ezekiel Mwakalukwa ( katika ) wakati walipotembelea jana eneo la msitu wa hifadhi wa Kihesa Kilolo ili kujiridhisha kabla ya kutoa maamuzi wa eneo hilo ambalo limeombwa na uongozi wa mkoa wa Iringa kuhaulishwa ili kujenga mji mpya wa kitalii katika mkoa huo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangallah, Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Japhet Hasunga pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza wakiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Ushauri wa Misitu ambapo Waziri Kigwangallah anakutana nao kwa mara ya kwanza tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo katika kikao cha tatu kilichofanyika jana mkoani Iringa.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kitaifa ya Ushauri wa Misitu wakimsikiliza Waziri Kigwangallah katika kikao cha tatu kilichofanyika jana mkoani Iringa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Ushauri wa Misitu, Prof. Shabani Chamshama akitoa neno la shukrani kwa viongozi kwa niaba ya Wajumbe wa kamati hiyo katika kikao cha tatu kilichofanyika jana mkoani Iringa.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangallah,( wa kwanza kulia ) akiwa ameambatana na wataalam wakati alipotembelea jana eneo la msitu wa hifadhi wa Kihesa Kilolo ili kujiridhisha kabla ya kutoa maamuzi wa eneo hilo ambalo limeombwa na uongozi wa mkoa wa Iringa kuhaulishwa ili kujenga mji mpya wa kitalii katika mkoa huo.
Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza ( wa pili kushoto) akiwa ameambatana na baadhi ya waandishi wa habari pamoja na wataalamu kutoka mkoani wakitembea kuangalia mipaka ya eneo la msitu wa hifadhi wa Kihesa Kilolo ambao umeombwa na uongozi wa mkoa huo kufutwa ili kujenga mji mpya wa kitalii katika eneo hilo.

 (PICHA ZOTE NA LUSUNGU HELELA-MNRT). 

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt.Hamis Kigwangallah amesema kuwa hatajibu maombi yoyote yaliyowasilishwa ofisini kwake kutoka kwa  Wakuu wa mikoa, Halmashauri pamoja na  Wakuu wa wilaya  ya kufuta maeneo ya Hifadhi ili maeneo hayo yaweze kutumika Kwa ajili ya  matumizi mengine.

Amesema kuwa maeneo hayo yalitengwa kisheria na yana umuhimu mkubwa kiuchumi na kijamii hivyo lazima yaendelee kuhifadhiwa kwa ajili ya faida ya kizazi cha sasa na kijacho. Amesema katika kipindi  cha Uwaziri wake hatajibu ombi lolote lile linalohusu kubadili matumizi ya maeneo hayo kwa vile kuwa na misitu sehemu za mijini ni sehemu ya maendeleo.

Aliyasema hayo jana mjini Iringa wakati alipokuwa akizungumza kwa mara ya kwanza na kamati ya kitaifa ya ushauri wa misitu iliyokutana kwa ajili ya kufanya kikao chake cha tatu tangu ilipoundwa mwaka jana ikiwa pamoja na kutembelea msitu wa Hifadhi wa kihesa Kilolo uliiombwa na uongozi wa mkoa kufutwa ili upate kutumika kwa kuweka miundo mbinu mipya ya mji wa kitalii.

Katika kikao hicho ambacho Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alishiriki, Waziri Kigwangallah  alimuomba Mkuu huyo awafikishe ujumbe Wakuu wa mikoa wengine  ambao walituma na wanaotarajia kutuma maombi ya namna hiyo kuwa yeye  hatakaa ayajibu hadi pale  tu yule  aliyemteua ampe maelekezo na si vinginevyo"

Amesema kuwa  Halmashauri nyingi nchini kila zikiona maeneo ya Hifadhi zimekuwa zikifikiria kubadili matumizi ya maeneo hayo ili yatumike kwa shughuli zingine za maendeleo kama vile kupima viwanja ili kuwauzia wananchi kwa lengo la kukusanya mapato.

"Ofisin kwangu kuna maombi mengi mno ambayo hata sielewi nianze na lipi na niache lipi, nasema sitajibu ombi lolote lile" alisisitiza Waziri Kigwangallah. Aidha, Waziri Kigwangallah mara baada ya kuzungumza na kamati hiyo alitembelea eneo la hifadhi ya msitu huo huku akiwa ameongoza na kamati hiyo pamoja na Uongozi wa Mkoa wa huo .

Katika kutembelea eneo hilo, Waziri Kigwagwallah aliwashukia viongozi wa Halmashauri kwa kuanzisha dampo katika eneo hilo huku kamati ikijionea magari matatu ya taka yakiendelea kumwaga uchafu kwenye eneo hilo jambo ambalo ni kinyume na sheria za uhifadhi.

Naye Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Japhet Hasunga  aliwashukia watendaji wa mkoa huo wakati walipokuwa wakipishana kutoa maelezo kuhusiana na mipaka na matumizi ya eneo hilo endapo Wizara itaridhia ombi lao la kubadili matumizi ya eneo hilo.

Kufuatia hali hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alimuhakikishia Waziri kuwa eneo hilo endapo watapewa litatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na si vinginevyo. Waziri Kigwangallah mara baada ya kutembelea eneo hilo wakati akitoa majumuisho yake, Alisema kuwa kufuatia ziara hiyo anasubili ushauri utakaotolewa na kamati ya kitaifa ya msitu ndipo atakapokuwa na jibu kuhusiana na ombi la kubadilia matumizi la eneo hilo .

Pia, Waziri Kigwangallah aliiagiza ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuhakikisha kuwa maeneo ya milima kwa vile sio moja ya maeneo ya hifadhi  yaongezwe katika eneo la hilo lengo likiwa ni kuzuia uharibifu wa uoto wa asili unaoendelea katika maeneo hayo.

Awali, Mwenyekiti wa Kamati hiyo wakati akitoa neno la shukrani alimhakikishia Waziri kuwa watamshauri jambo lolote lile  linalohusu misitu bila kujali litamfurahisha au litamuudhi, kitakachoangaliwa hapo ni maslahi mapana ya taifa.

Katika hatua nyingine ,Waziri Kigwangallah  ameitaka Wakala wa Huduma za Misitu nchini  (TFS) kuanza kuweka nguvu nyingi katika kuhifadhi misitu baadala ya kuvuna na kufanya biashara ya mazao ya misitu. Alisema licha ya kuwa TFS imekuwa ikifanya vizuri katika baadhi ya maeneo  lakini katika suala la kuhifadhi misitu imekuwa kama vile  sio kazi yake " yenyewe kazi yake imekuwa ni kuvuna kilichopandwa, kuuza na kukusanya mapato yatokanayo na mazao ya misitu" alisema. 

Wakati huo huo, Waziri Kigwangallah amesema Wizara inakusudia kuchukua misitu yote iliyo chini ya vijiji na Halmashauri kwa vile zimeshindwa kuisimamia ipasavyo na hivyo kupelekea sehemu kubwa ya nchi kugeuka kuwa jangwa.

Mbali na hilo amewaonya wananchi wanaowazuia watendaji  kuweka vigingi katika mipaka ya hifadhi, huku wengine wamekuwa wakivingoa na wengine kuhamisha vigingi hivyo kutoka eneo moja hadi jingine kuwa  waache tabia hiyo moja la sivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.