slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Sunday, October 14, 2018

TFS YAHAMASISHA UTALII WA KIIKOLOJIA KWA WATANZANIA

Afisa Misitu Mkuu kutoka Wakala wa Huduma za Misitu nchini(TFS),Arijanso Mlog akizungumza na Waandishi wa habari katika Onesho la Kimataifa la  Utalii (SITE)linaloendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.



Wafanyakazi wa Huduma za Misitu nchini TFS, Wakiwaonesha wadau Mazao Mbalimbali yatokanayo na misitu ambayo ni mazuri kwa ajili ya kuimarisha afya ya Mwanadamu
Meneja Masoko na Uwekezaji wa Wakala wa Huduma za Misitu Nchini, Mariam Kobelo akieleza huduma za kitalii zilizopo ndani ya Hifadhi za Misitu zilizo chini ya TFS

Afisa Misitu Mwandamizi , Anna Lawuo Akizungumza na Waandishi wa habari  kuhusu umuhimu wa mazao yatokanayo na misitu nchini


TFS YAHAMASISHA  UTALII WA KIIKOLOJIA KWA                                      WATALII
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) imetoa wito kwa watanzania kutembelea Maeneo yaliyohifadhiwa ili kuweza kujionea namna ikolojia na uhifadhi katika misitu hiyo ilivyo na faida kwa viumbe hai na Wanadamu.



Akizungumza na Waandishi wa Habari,  Afisa Misitu Mkuu kutoka Wakala wa Huduma za Misitu nchini(TFS),Arijanso Mlog  katika Onesho la Kimataifa la  Utalii lijulikanalo kama Swahili  International Tourism Expo (SITE) linaloendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam, Mlog amesema kuwa watu wanapaswa kutemblea misitu hii ili waweze kujionea na kujifunza umuhimu wa ikolojia katika hifadhi.




"Ni vyema watu wakaja wakatembelea hifadhi ya misitu ya Amani waweze kujionea namna Misitu iliyopakana na makazi ya watu na maporoko ya maji ambayo hayakauki muda wote na kujionea maua ambayo yanaaminika katika imani kuwa ndio yalitumika wakati wa kristo na watu husafiri kutoka sehemu mbalimbali  kuyafuata kutoka maeneo ya mbali"amesema Mlog.




Kwa upande wake, Meneja Masoko na Uwekezaji wa Wakala wa Huduma za Misitu Nchini, Mariam Kobelo amewataka wdau mbalimbali  kutembelea banda lao lililopo katika   Onesho La Kimataifa la Utalii la SITE linaloendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam ili kujionea huduma zitolewazo na TFS na kujua wapi wanaweza kutembelea kwa ajili ya mapumziko yao.


Mariamu amesema kuwa Misitu inayohifadhiwa na TFS ina upekee sana , Hivyo ametoa wito kwa wanafunzi, wanasayansi na wanataaluma mbalimbali kuwa wanaweza kwenda ili kuweza  kufanyia tafiti, Mapumziko kwa wana ndoa pia wanaweza kwenda kutembea na  familia zao .




No comments:

Post a Comment