
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi akifunga mafunzo maalum ya kijeshi kwa ajili ya kupambana na ujangili kwa Askari wanyamapori katika Pori la Akiba la Rungwa mkoani Singida hivi karibuni.

Askari wanyamapori wakionesha kwa vitendo namna ya kupambana na majangili wakati wakiwakamata majangili wakati wa kuhitimisha mafunzo hayo.

Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mark Childress akizungumza wakati wa kufunga mafunzo maalumu ya ya kupambana na ujangili kwa Askari wanyamapori katika Pori la Akiba la Rungwa mkoani Singida hivi karibuni. Mafunzo hayo yatawasaidia Askari wanyamapori kupata taarifa za kitenteligensia kwa ustadi wa hali ya juu katika kupambana na kukabiliana na majangili.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa wanyamapori Tanzania ( TAWA) Bw. Martin Loibook akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo katika Pori la Akiba la Rungwa mkoani Singida hivi karibuni.

Askari wanyamapori wakionesha kwa vitendo wakati wa kuhitimu mafunzo maalumu yaliyofanyika katika Pori la Akiba la Rungwa Mkoani Singida yaliyohitimishwa hivi karibuni wakionesha namna ya kupambana na majangili wakati wakiwakamata majangili.
---------------------------------------------------------------
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi ametoa wito kwa watu wanaojihusisha na vitendo vya ujangili waache kazi hiyo mara moja na badala yake watafute kazi nyingine zitakazoweza kuwapatia kipato halali kwa kufanya hivyo wataweza kujiepusha kutiwa nguvuni na askari wanyamapori waliobobea kwa kazi hiyo.
Maj. Gen Milanzi alitoa wito huo hivi karibuni wakati wa akifunga mafunzo maalumu ya kupambana na Ujangili kwa askari wanyamapori katika pori la akiba la Rungwa mkoani Singida yaliyofadhiliwa na Marekani na yaliyotolewa na Kikosi maalum cha wanajeshi kutoka Marekani.
Amesema kuwa mafunzo hayo ni muhimu sana kwa askari wanyamapori ili kuendelea na kukabiliana na wimbi kubwa la ujangili kwa kuwa majangili wasasa wanatumia silaha za kisasa tofauti na majangili wa zamani ambao walikuwa wakitumia upinde na mishale.
Aliongeza kuwa majangili wa sasa ambao askari wanyamapori wamekuwa wakikabiliana nao maporini ni wale ambao wanatumia silaha za kivita hiyo ni lazima askari wetu wapewe mafunzo ya hali ya juu ili waweze kukabiliana nao.
Aidha Katibu Mkuu, Milanzi alisema Wizara imejipanga kuhakikisha suala la ujangili linakwisha ambapo kituo kingine cha mafunzo ya kijeshi kwa askari wanyamapori cha Mlele kilichopo Mkoani Katavi kimeanzishwa mbali na vyuo vya Pasiansi na Mweka, Likuyu Sekamaganga ambavyo pekee ndivyo vilivyokuwa vikitoa mafunzo kwa askari wanyamapori.
Aliongeza kuwa, kwa sasa Serikali imejipanga kwa kushirikiana na Interpol kuhakikisha kuwa hatakamatwa jangili tu aliyehusika kuua mnyama porini bali mtandao wote utakamatwa na kupelekwa kwenye vyombo vya sheria mahali popote.
Akizungumza na wahitimu wa mafunzo hayo, Milanzi alisema mafunzo hayo yamejikita kuwasaidia kupambana na majangili, magaidi pamoja na majambazi ambapo wao ndo watu wa kwanza kukumbana nao wakiwa porini kwani ndiko wanakotumia kujificha kwahiyo ujuzi walioupata umewaongezea ufanisi katika kulinda maliasili zilizopo kwenye maeneo yao.
Aliwataka pia wahitimu hao kufanya kazi kwa kujituma wasiishie tu kusherekea kumaliza mafunzo bali waonyeshe kwa vitendo hii itasaidia na kuipa ari Marekani pamoja na Asasi za kimataifa zenye lengo la kusaidia nchi katika vita dhidi ya Ujangili.
Kwa upande wake Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mark Childress amewataka wahitimu wazingatie mafunzo waliyopata kwa kuyafanyia kazi ili Pori la Akiba la Rungwa liwe sehemu salama kwa wanyamapori wanaopatikana katika pori hilo.
Ameahidi kuwa nchi yake itaendelea kuisaidia Tanzania kwa kuwa suala la ujangili bado ni kubwa linalohitaji ushirikiano wa pande zote ili liweze kutokomezwa.
Gwaride la wahitimu wa mafunzo ya kijeshi kwa askari na maafisa wa Hifadhi za Taifa likiingia katika viwanja vya mazoezi katika kambi ya mafunzo ya Mlele wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi akipokea salamu ya utii kutoka kwa askari wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (hawapo pichani) wakati wa ufungaji mafunzo kwa askari na maafisa hao yaliyofanyika katika kambi ya mafunzo ya Mlele mkoani Katavi
Askari na Maafisa wa Hifadhi wakipita kwa heshima mbele ya mgeni rasmi kwa mwendo wa pole na haraka wakati wa ufungaji wa mafunzo ya kijeshi waliyopata katika kambi ya mafunzo ya Mlele mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya kubadili utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuendeshwa katika mfumo wa jeshi usu kutoka mfumo wa kiraia.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi akikagua gwaride wakati wa kufunga mafunzo kwa askari wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro yaliyofanyika katika kambi ya mafunzo ya Mlele mkoani Katavi 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi(kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi wakipokea salamu za heshima kwa kupiga saluti wakati gwaride likipita mbele kwa heshima wakati wa ufungaji wa mafunzo kwa askari wa shirika la Hifadhi za Taifa,(TANAPA) na Maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya taifa Ngorongoro.
Bendi ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) ikipita mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa ufungaji wa mafunzo ya kijeshi kwa askari na maafisa wa Hifadhi ,Mafunzo yaliyofanyika katika kambi ya Mlele mkoani Katavi.
Askari na Maafisa wa Hifadhi za Taifa wakionesha umahiri katika matumizi ya silaha wakati wakionesha kwa vitendo mafunzo ya kijeshi waliyopata katika kambi ya Mlele mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya kubadili utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuendeshwa katika mfumo wa jeshi usu. 
Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Witness Shoo (kushoto) pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Uhifadhi Mtango Mtahiko wakifuatilia maonesho ya matumizi ya silaha kutoka kwa wahitimu hao.
Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete akisherehesha wakati wa ufungaji wa mafunzo ya kijeshi kwa askari na Maafisa wa Hifadhi waliyopata katika kambi ya Mlele mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya kubadili utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuendeshwa katika mfumo wa jeshi usu.
Askari na Maafisa wa Hifadhi wakionesha umahiri katika matumizi ya silaha wakati wakionesha kwa vitendo mafunzo ya kijeshi waliyopata katika kambi ya jeshi ya Mlele mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya kubadili utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuendeshwa katika mfumo wa jeshi usu.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi,Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi pamoja na Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ,Freddy Manongi wakifuatilia maonesho hayo. 




Askari na Maafisa wa Hifadhi wakionesha umahiri katika matumizi ya silaha wakati wakionesha kwa vitendo mafunzo ya kijeshi waliyopata katika kambi ya Mlele mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya kubadili utendaji kazi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuendeshwa katika mfumo wa jeshi usu.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi akitizama matundu ya risasi zilizolengwa na mmoja wa askari wa uhifadhi waliohitimu mafunzo ya kijeshi katika kambi ya Mlele mkoani Katavi.Kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi.
Wakufunzi wa Mafunzo ya kijeshi kwa maofisa na askari wa Hifadhi za Taifa wakitambulishwa mbele ya mgeni rasmi,(hayupo pichani).
Mhifadhi kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Lilian Magoma akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wenzake wa mafunzo ya kijeshi yaliyofanyika katika kambi ya Mlele iliyopo mkoani Katavi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi akitunuku vyeti kwa askari na maafisa wa uhifadhi waliohitimu mafunzo ya kijeshi katika kambi ya Mlele mkoani Katavi.
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Getrude Lyatuu akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo. 
Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro,Freddy Manongi akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo. 
Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori Alexander Songorwa akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akimkaribisha Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi kuzungumza na wahitimu wa mafunzo ya kijeshi kwa askari na maofisa wa Hifadhi za Taifa .
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo kwa askari na maofisa wa Hifadhi za Taifa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Meja Jenerali Gaudence Milanzi na viongozi wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.



