slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Friday, October 21, 2016

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, PROF. JUMANNE MAGHEMBE AAHIDI KUFANYA MABADILIKO MAKUBWA CHUO CHA TAIFA CHA UTALII

Waziri wa Maliasili Na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe akizungumza na watumishi wa Chuo cha Taifa cha Utalii Kampasi ya Bustani pamoja na waandishi wa habari alipotembelea chuo hicho juzi.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe (wanne kushoto) akikagua sehemu ya jiko katika chuo hicho.
Picha ya pamoja kati ya Waziri wa Maliasili Na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe na viongozi pamoja na watumishi wa chuo hicho.
________________________________________

Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, ameahidi kuibadili Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Taifa cha Utalii na kuifanya kuwa Bodi ya Utawala.

Alisema lengo la mabadiliko hayo ni kuhakikisha Chuo hicho kinatoa wataalamu wenye sifa na viwango vinavyostahiki kufanya kazi ndani na nje ya nchi.

Waziri Maghembe ametoa kauli hiyo juzi alipotembelea chuo hicho na kuangalia namna ya kukiboresha na kukifanya kiwe cha ushindani.


Aidha, Prof.Maghembe ameutaka uongozi wa chuo hicho kuondoa jina la Wakala ambalo limekuwa likitumika na chuo hicho badala yake kiitwe Chuo cha Taifa cha Utalii ili kionyeshe hadhi yake kitaifa na kimataifa huku akisisitizia suala la ubunifu katika uendeshaji na kuongeza mapato badala ya kulalamika kukabiliwa na changamoto nyingi ambazo chuo kingeweza kuzitatua.


Amekitaka chuo hicho kuwa cha mfano kwa kuwafundisha wanafunzi k maadili mema kwa kuwa wafanyakazi wengi wa mahoteli nchini wamelalamikiwa kuwa na sifa za udokozi hivyo kuwafanya watu wenye mahoteli kuajiri wafanyakazi kutoka nje ili kuepuka fedheha hiyo.


"Baadhi ya wahudumu katika hoteli zetu wamekuwa na tabia ya udokozi, hii ni sifa mbaya kwa wageni kwani huharibu taswira ya hoteli"


Aliutaka uongozi wa chuo hicho kuwa na mitaala yenye kutoa mafunzo ya kupika vyakula vya asili ili kuenzi utamaduni wa Mtanzania na kuendeleza utalii wa kiutamaduni.

No comments:

Post a Comment