slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Monday, September 4, 2017

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII YATEMBELEA HIFADHI YA MAZINGIRA ASILIA ULUGURU NA JUMUIYA YA HIFADHI YA WANYAMAPORI YA WAMI MBIKI MKOANI MOROGORO

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (katikati) akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakati wa ziara yao ya kikazi katika eneo la Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Wami Mbiki/Ushoroba mkoani Morogoro ambayo iliyolenga kubaini changamoto mbalimbali za uhifadhi kwa ajili ya kuishauri Serikali namna bora ya kukabiliana nazo.
 Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakimsikiliza Afisa Wanyamapori Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Leonard Mayeta (wa nne kulia) wakati akitoa maelezo kuhusu Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Wami Mbiki/Ushoroba wakati wa ziara ya kamati hiyo kwenye hifadhi hiyo ambayo ililenga kubaini changamoto mbalimbali za uhifadhi kwa ajili ya kuishauri Serikali namna bora ya kukabiliana nazo.
Kaimu Mkurugenzi wa Biashara na Utalii wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Imani Nkuwi akiwasilisha taarifa ya mamlaka hiyo kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Dkt. James Wakibara mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii baada ya kutembelea eneo la Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Wami Mbiki mkoani Morogoro. 
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (kulia) na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo (wa tatu kulia) wakiongoza Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kupanda mlima katika Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru mkoani Morogoro wakati wa ziara yao iliyolenga kubaini changamoto mbalimbali za uhifadhi kwa ajili ya kuishauri Serikali namna bora ya kukabiliana nazo. 
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo (kulia) akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakati wa ziara yao ya kikazi katika Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru mkoani. 
 Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru, Cathbert Mafupa (kushoto) akitoa maelezo kwa Wajumbe wa Kamati hiyo kuhusu Hifadhi hiyo. 
 Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mary Chatanda (wa tatu kushoto) akizungumza kutaka ufafanuzi wa baadhi ya mambo kuhusu Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru wakati wa ziara ya kamati kwenye hifadhi hiyo. Wengine pichani ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (wa tatu kulia), Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhandisi Atashasta Ndetiye (wa nne kulia) na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu, Prof. Dos Santos Silayo (wa pili kulia). 
 Wajumbe wa Kamati wakikagua eneo la Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru mkoani Morogoro wakati wa ziara yao ya kikazi ya kuangalia changamoto mbalimbali za uhifadhi zinazoikabili hifadhi hiyo kwa ajili ya kuishauri Serikali namna bora ya kukabiliana nazo. 
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo (kulia) akiongoza Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kutembelea Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru. 
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki (kulia) na Wajumbe wa Kamati hiyo wakitembelea eneo la Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru. 
 Mkurugenzi wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mtango Mtahiko (kulia) ambaye alimuwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo kwenye ziara hiyo.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo (kushoto) akiwasilisha taarifa ya taasisi hiyo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii baada ya kutembelea Hifadhi ya Mazingira Asilia Uluguru mkoani Morogoro jana wakati wa ziara ya kamati hiyo iliyolenda kubaini changamoto mbalimbali za uhifadhi katika hifadhi hiyo kwa ajili ya kuishauri Serikali namna bora ya kukabiliana nazo. 
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo (kushoto) akiwasilisha taarifa ya taasisi hiyo mbele ya Kamati.

No comments:

Post a Comment