slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Wednesday, June 27, 2018

DK. KIGWANGALLA APOKEA TAARIFA YA AWALI YA KAMATI YA KOVA KUHUSU TUHUMA ZA MAUAJI YA TEMBO


VIDEO
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akipokea taarifa ya awali ya uchunguzi wa tuhuma za mauaji ya Tembo katika Ikolojia ya Ruaha-Rungwa ambazo ziliripotiwa na kituo cha habari cha ITV-London mwaka 2017, kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati Maalum aliyoiunda kuchunguza tuhuma hizo, Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Polisi, Suleiman Kova ofisini kwake Jijini Dodoma. Katikati ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Japhet Hasunga na Kaimu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk. Iddi Mfunda (kulia). Tuhuma hizo ziliwahusisha watumishi wa Serikali na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo Duniani (UNDP) kupitia mradi wa SPANEST waliokuwa wakiufadhili.
 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) na Naibu Waziri, Japhet Hasunga (katikati) wakipokea taarifa ya awali ya uchunguzi wa tuhuma za mauaji ya Tembo katika Ikolojia ya Ruaha-Rungwa ambazo ziliripotiwa na kituo cha habari cha ITV-London mwaka 2017, kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati Maalum aliyoiunda kuchunguza tuhuma hizo, Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Polisi, Suleiman Kova ofisini kwake Jijini Dodoma. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) na Naibu Waziri, Japhet Hasunga (wa pili kulia) wakipokea taarifa ya awali ya uchunguzi wa tuhuma za mauaji ya Tembo katika Ikolojia ya Ruaha-Rungwa ambazo ziliripotiwa na kituo cha habari cha ITV-London mwaka 2017, kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati Maalum aliyoiunda kuchunguza tuhuma hizo, Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Polisi, Suleiman Kova ofisini kwake Jijini Dodoma. Wengine ni wajumbe wa kamati hiyo, Julius Kibebe, Kresensia Swai na Emmanuel Musamba (kushoto). 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akimkabidhi Kaimu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk. Iddi Mfunda taarifa hiyo kwa ajili ya utekelezaji wa mapendekezo ya kamati hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wajumbe wa kamati maalum aliyoiunda kuchunguza tuhuma za mauaji ya Tembo ambazo ziliwahusisha watumishi wa Serikali na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo Duniani (UNDP) kupitia mradi wa SPANEST waliokuwa wakiufadhili. (Picha na Hamza Temba - Wizara ya Maliasili na Utalii).

No comments:

Post a Comment