slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Monday, March 18, 2019

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUJA NA MKAKATI MAALUM WA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu amesema Wizara ya Maliasili na Utalii  inatarajia kuja na mkakati maalum wa kutangaza utalii ndani na nje ya nchi kwa kunadi  maeneo ya vivutio vya utalii badala ya kuinadi nchi kwa ujumla na  vivutio vyake

Pia,Amesema  maeneo hayo yatakuwa yakinadiwa  kwa mfumo wa vifurushi (Packages) hali itakayopelekea mtalii akija nchini ataweza kutembelea maeneo ya  Hifadhi,  Misitu ya Mazingira asilia pamoja na  maeneo ya utalii wa kiutamaduni.

Amesema lengo la kuja na mkakati huo ni kusaidia maeneo hayo kuweza kujulikana pamoja na kumuwezesha mtalii kuweza kuvifahamu vivutio vinavyopatikana katika eneo hilo kwa undani badala ya kuitangaza nchi kwa kujumuisha vivutio vya utalii vilivyopo  kwa ujumla wake.

Amesema mkakati huo utasaidia  kuongeza idadi ya watalii katika maeneo yenye vivutio ya utalii lakini kwa sasa yamekuwa yakipata idadi ndodgo ya watalii kwa vile yamekuwa hayafahamiki ipasavyo.

Amesema mkakati huo utalenga zaidi katika maeneo yenye utalii wa kiutamaduni pamoja na maeneo ya Misitu asilia, Ni utalii mpya ambao kwa Tanzania haufahamiki sana unaojikita kuangaliia viumbe ambao wapo hatarini kutoweka.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri huyo mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakati Kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi pamoja na Msitu Asilia wa Chome katika wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro.

Ameeleza kuwa aina hiyo ya kutangza vivutio vya utalii katika eneo fulani badala ya nchi italeta manufaa makubwa kwa Hifadhi na maeneo yale ambayo kwa sasa yamekuwa yakipokea idadi ndogo ya watalii hasa katika ukanda wa Kusini na Magharibi.

Amesema ukizungumzia utalii kwa sasa unalenga mikoa ya Kaskazini ambako zaidi ya asilimia 80 unafanyika ukanda huko huku kanda nyingine kama vile kanda ya ziwa, Magharibi pamoja na Kusini zikiwa bado idadi ya watalii wanaotembelea ni ndogo ukilinganisha na uwingi wa vivutio vya utalii vilivyopo katika maeneo hayo.

Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Shabani Shekilindi amesema Tanzania imejaliwa kuwa na vivutio vingi vya utalii lakini mapato yatokanayo na utalii hayaakisi ualisia wa vivutio vilivyopo nchini hivyo mikakati mipya ya kutangaza vivutio inahitajika.


 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii, Shabani Shekilindi (wa kwanza kushoto) akiwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu ( wa pili kushoto) wakiwa pamoja na Wajumbe wa kamati hiyo wakipewa maelezo mafupi kuhusu mradi wa kuzalisha faru weusi na mbwa mwitu kutoka kwa Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa (TANAPA) unaofanyika katika Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi wakati Kamati ilipofanya ziara katika Hifadhi hiyo iliyoko mkoani Kilimanjaro.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu akipigiwa saluti na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi wakati alipokuwa ameongozana na Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii ilipotembelea eneo hilo kwa ajili yamradi wa kuzalisha faru weusi na mbwa mwitu
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii kutembelea eneo la maradi wa kuzalisha faru weusi na mwitu katika Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi mkoani Kilimanjaro. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki.



 Baadhi ya Wajumbe wa  kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii walipotembelea ofisi ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania iliyopo katika wilaya ya  Same







SERIKALI YAPANIA UWEKEZAJI UTALII KANDA YA ZIWA



Serikali imesema kuwa itaendelea kuweka mazingira rafiki, kuwahamasisha na kuwavutia Wawekezaji watakaosaidia kuwapeleka watalii katika maeneo ya Kanda ya Ziwa ili kukuza Sekta ya Utalii Katika maeneo hayo.

Hatua hiyo inakuja baada ya kuyapandisha hadhi Mapori ya Akiba ya  ya  Burigi, Biharamulo, Kimisi,Ibanda na Rumanyika kuwa Hifadhi ya Taifa.

Akizungumza kwenye mkutano uliohusisha  Wizara Maliasili na Utalii  na Wawekezaji kutoka maeneo mbalimbali nchini, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amesema kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Sekta binafsi kwa kuwa sekta hiyo ni injini ya Utalii nchini.

Amesema kuwa mkutano huo una umuhimu mkubwa Katika maendeleo ya sekta hiyo kwa kuwa Serikali  inapata  nafasi ya kuwaelezea Wawekezaji fursa mbalimbali  zinazopatika katika Ukanda huo pamoja na kusikia changamoto zao.

Amesema kufuatia kufanyika kwa mkutano huo Sekta Binafsi itakuwa na kila sababu ya kuwekeza katika Ukanda huo baada ya Serikali kuendelea kuweka mazingira rafiki kwa Uwekezaji

Amesema Serikali imeendelea kuweka Miundombinu wezeshi ambayo imekuwa chachu ya kurahisisha watalii na wageni mbalimbali kutembelea maeneo ya hifadhi.

Mhe.Kanyasu ameyataja maeneo yaliyoboreshwa  kuwa  ni  Barabara,   Uwanja wa ndege wa Mwanza pamoja na  Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Chato ambao umefunguliwa.

Hata hivyo, Mhe.Kanyasu amesema kuwa licha ya   kuwa Tanzania imekuwa ikifanya vizuri kwenye shughuli za Uhifadhi, lakini katika Uendelezaji Utalii bado jitihada za makusudi zinahitajika.

"Tuna vivutio vingi vya utalii lakini idadi ya watalii wanaotembelea vivutio hivyo hairidhishi, tunahitaji kuongeza juhudi katika kuwahamasisha watalii wa ndani na nje ya nchi kutembelea maeneo hayo" Amesisitiza

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo ambaye alikua mwenyeji wa mkutano huo, Prof.Adolf Mkenda amesema kupitia mkutano huo kutasaidia kuchagiza idadi ya watalii kuongezeka kwa kutembelea vivutio vya utalii vinavyopatikana katika ukanda huo.

Amesema kufanyika kwa mkutano huo ni muendelezo wa kutawanya fursa za uwekezaji wa sekta ya utalii nchi nzima.

Akichangia hoja kwenye mkutano huo, Mwenyekiti wa Chama cha Wasafirishaji Watalii ( TATO)Wilbard Chamburo ameiomba Serikali iangalie uwezekano wa kutobadili  mara kwa mara sera na mipango ya kukuza masuala ya Utalii kwa kuwa kuwa hali hiyo inayochangia kuwakatisha tamaa Wawekezaji.

Amesema Wawekezaji wanataka kuwekeza mahali ambako wana uhakika wa kupata  faida itayowasaidia kujiendesha kibiashara pamoja na kulipa kodi stahiki za serikali.

Katika mkutano huo, Wakuu wa mikoa yote ya Kanda ya Ziwa wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Mhe.John Mongela walikua miongoni mwa Washiriki.



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akizungumza  kwenye ufunguzi wa mkutano wa siku moja uliofanyika jana jijini Mwanza  baina ya Wizara ya Maliasili na Utalii  na Wawekezaji kutoka maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kuhamasisha Utalii Ukanda wa Ziwa




Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella (wa kwanza kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Hifdadhi za Taifa.Alllan Kijazi (kulia) kabla ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine  (wa pili kushoto)  Kanyasu kufungua mkutano baina ya Wizara hiyo na Wawekezaji  uliofanyika jijini Mwanza.


Baadhi ya washiriki wa mkutano baina ya Wizara ya Maliasili na  Utalii hiyo na Wawekezaji  uliofanyika jijini Mwanza'



 Baadhi ya Wawekezaji wakubwa walioshiriki mkutano wa kuhamasisha utalii kanda ya Ziwa.



Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akizungumza  kwenye  mkutano wa siku moja uliofanyika jana jijini Mwanza  baina ya Wizara ya Maliasili na Utalii  na Wawekezaji kutoka maeneo mbalimbali nchini ka lengo la kuhamasisha Utalii Ukanda wa Ziwa




Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu (mbele) akiwa ameongozana na Naibu waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu (wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongela(katikati)

Thursday, March 7, 2019

WAZIRI KIGWANGALA ATOA MSIMAMO VITA DHIDI YA UJANGILI,


 Waziri wa Maliasili na Utalii,  Dkt. Hamisi Kigwangala amewataka Watanzania kuondokana na dhana iliyojengeka miongoni mwao kuwa watumishi wa Wizara hiyo hususan  wahifadhi wa  wanyamapori na Misitu  ni watu katili  wanaowatesa Wananchi.


Kauli hiyo ameitoa leo wakati akifungua mkutano wa 26 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika katika Chuo cha Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi jijini Mwanza.

Amesema watumishi hao ni watu wenye utu na weledi wa hali ya juu na wanaozingatia  sheria katika kutimiza majukumu yao na hulazimika kutumia nguvu wakati wakipambana na majangili wanaokutwa katika maeneo ya hifadhi wakifanya vitendo vya ujangili.

‘’ Ulinzi wa Rasilimali za nchi ni jukumu letu sote, wizara imepewa dhamana ya kusimamia na kuongoza kwa niaba ya watanzania, kama kuna watumishi wa Wizara hii wanaowanyanyasa wananchi naomba walete ushahidi kwetu ili tuwachukulie hatua’’ amesema Dkt. Kigwangala.

Waziri Kigwangala amesikitishwa na idadi ya watumishi walipoteza maisha kwa ajali na wengine kuuwawa na majangili wakati wakipambana nao katika maeneo yote ya hifadhi  nchini na kutoa wito kwa wananchi wote wenye taarifa au ushahidi juu ya vitendo vyovyote vya kihalifu kuziwasilisha katika mamlaka zinazohusika.

Amesema kuwa Serikali haitasita kuwachukulia hatua wale wote wanaojihusisha na vitendo vya ujangili na uhalifu katika maeneo ya hifadhi na wale wote wanaoshirikiana na makundi ya watu wenye nia ovu ya kukwamisha juhudi za uhifadhi wa rasilimali za Taifa.

Ametoa wito kwa wananchi kuheshimu sheria za uhifadhi na kuepuka kuvamia maeneo ya hifadhi kwa shughuli za kijamii na ufugaji akitoa wito kwa viongozi mbalimbali wa Siasa kuunga mkono juhudi za wizara za ulinzi wa maeneo ya hifadhi kwa kuwaelimisha wananchi wanaowaongoza kujiepusha na vitendo vya uvamizi wa maeneo ya hifadhi badala ya kuwatetea.


Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof.Adolf Mkenda akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho amesema kuwa jumla ya watumishi 23 walifariki dunia  wakati wakitekeleza majukumu ya uhifadhi   na   5 walijeruhiwa na majangili wakiwa kazini.

Prof. Mkenda amesema kuwa waliofanya vitendo hivyo  hawaitakii mema Tanzania na ni maadui wa shughuli za uhifadhi nchini akiongeza kuwa Serikali itaendelea kusimama na kuwatetea watumishi na askari wa wanyamapori wanaotimiza majukumu yao kwa kuzingatia sheria.







 Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala akisisitiza jambo  wakati akizungumza na Watumishi wa Wizara hiyo kuhusu umuhimu wa kutekeleza maagizo kwa wakati yanayotolewa na Viongozi wa Wizara hiyo katika kikao cha Baraza la 26 la  Wafanyakazi wa Wizara hiyo  kilichofanyika leo Jijini Mwanza.

Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii Mhe,Constantine Kanyasu akizungumza na Watumishj wa Wizara  hiyo katika kikao cha Baraza la 26 la  Wafanyakazi kilichofanyika leo Jijini Mwanza

Katibu Mkuu wa  Maliasili na Utalii Prof, Adolf Mkenda akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo (hawapo Pichani) wakati wa ufunguzi wa baraza la 26 la Wafanyakazi wa Wizara hiyo liliofanyika  leo Jijini Mwanza.
 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla, Naibu Waziri  wa Wizara, Mhe, Constantine Kanyasu wakiwa wameshikana na watumishi wengine  hukuwakiimba wimbo wa mshikamano Daima katika Kikao cha Baraza la 26 la Wafanyakazi kilichofanyika leo jijini Mwanza.


 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwa ameambatana na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Constantine Kanyasu wakati akikagua gwaride la Jeshi Usu katika Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Pasiansi


Wafanya kazi wa  Maliasili na Utalii wakiimba wimbo wa mshikamano Daima katika Kikao cha Baraza la 26 la Wafanyakazi wa Wizara hiyo kilichofanyika leo jijini Mwanza.



Monday, February 4, 2019



MANGI MELI REMAINS In Old Moshi the head of Chief Meli is missing. A strong figure of resistance, he fought bravely against the German colonialists and was hanged in 1900. His head is said to have been shipped to Germany, where thousands of human skulls are still stored in museum depots. The grandson of Chief Meli has been searching for the head for more than 50 years, until now without success. Yet traces of Chief Meli can be found in songs, stories and archives. This has formed the basis for a Tanzanian-German collaboration where an animated video sculpture and re-examined historical photographs portray the life story of Meli – and his legacy today. Mangi Meli Remains premiered in Berlin, November 2018 and will display in Dar es Salaam before concluding in Old Moshi, March 2019 where it will remain as a place of remembrance and a placeholder for Chief Meli’s missing head. A Flinn Works (DE) production with Mr. Isaria Meli (TZ), Old Moshi Cultural Tourism (TZ), BSS Projects (TZ/UK), ArtEver (TZ) in cooperation with Ethnologisches Museum Berlin and Tieranatomisches Theater at Humboldt University Berlin. Supported by Senatsverwaltung für Kultur und Europa, Goethe Institute Tanzania and Between Bridges.


Tuesday, January 1, 2019


NAIBU WAZIRI MHE,KANYASU AWAFUNDA WATUMISHI WA  TFS PAMOJA NA WANANCHI


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu amewaonya wananchi  wanaofanya shughuli za kibinadamu ndani ya Hifadhi za Misitu nchini kuacha tabia ya kuwashambulia Watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wanapokuwa wanatekeleza majukumu yao.

Onyo hili linakuja ikiwa zaidi ya watumishi watano wa TFS  katika mikoa ya Pwani, Tabora ,Kigoma pamoja Kilimanjaro wakiwa wamepoteza maisha yao kwa kushambuliwa na wananchi wakati wakiwa wanatekeleza majukumu yao.

Aidha, Mhe.Kanyasu amewapiga marufuku watumishi wa TFS kujichukulia sheria mkononi kwa kuwapiga wananchi wanapobainika kutenda makosa.

"Watumishi wa TFS hamruhusiwi   kumpiga Mwananchi mnapomkamata ndani ya Hifadhi au akiwa anasafirisha mazao ya Misitu kinyume na sheria, atakayebainika sheria itachukua mkondo wake.

Ametoa  onyo hilo wakati akizungumza na wananchi  kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika  katika kata ya Mgusu  wilayani  Geita mkoani Geita ikiwa ni ziara yake ya kutatua migogoro ya mipaka kwenye msitu wa Hifadhi Geita iliyopo baina ya Vijiji ambapo jumla ya hekta 4,462.95 zimefutwa kwa tangazo la Serikali.


Amesema shughuli za uhifadhi ni lazima zifanyike kwa ushirikishwaji kati ya wananchi na watumishi wa TFS.

" Uhasama unaozidi kujengeka kati yenu  hauna tija katika uhifadhi shirikianeni" amesisitiza Mhe.Kanyasu.

Aidha,  Mhe . Kanyasu amewataka wananchi kuheshimu na kuzifuata sheria za uhifadhi ya Misitu nchini huku akiwataka  watumishi kujiepusha na migongano kati yao na wananchi.

Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu amewataka wananchi wafuate sheria kwa kulipia vibali kwa TFS pale wanapokuwa na mahitaji ya mazao ya Misitu badala ya kusubilia mpaka wakamatwe.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe.Josephat Maganga amemueleza Naibu Waziri huyo kuwa hali ya Misitu katika wilaya hiyo ni mbaya kufuatia shughuli za kibinadamu zinazoendelea kufanyika Misitu hiyo.

Hata hivyo, Mkuu huyo wa Wilaya  hiyo Mhe.Maganga alisema kufuatia hali hiyo tayari  Kamati ya Ulinzi na Usalama kwa kushirikiana TFS wameshaanza kufanya  doria ya kuwaondoa wafugaji na wakulima waliovamia  Hifadhi.

Katika hatua nyingine, Diwani ya Kata ya Mgusu, Pastory Lugusa amemuomba  Naibu Waziri huyo kumegewa eneo la Hifadhi  kwa vile idadi ya wakazi wa kata hiyo imeongezeka hali inayopelea kukosa maeneo kwa ajili  ya malisho na Kilimo.

Kwa upande wake Meneja wa Misitu  wa  wilaya wa TFS, Fedy Ndandika amemuhakikishia Naibu Waziri kuwa  watashirikiana na wananchi hata hivyo tayari wameanza kutoa elimu ya umuhimu wa uhifadhi kwa jamii zinazozunguka Hifadhi


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu  akiwa na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Geita mkoani Geita akipewa maelezo na Meneja wa Misitu  wa  wilaya wa Wakala wa Huduma ya Misitu Tanzania (TFS) Fedy Ndandika wakati alipotembelea eneo la Manga lililokuwa limevamiwa na wakulima ambayo ni moja ya eneo la Msitu wa Hifadhi  Geita
 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akizungumza na wananchi  kwenye mkutano wa hadhara katika kata ya Mgusu, Halmashauri ya wilaya ya  Geita mkoani Geita akiwasisitiza wananchi umuhimu wakufuata  sheria na kuacha tabia ya kuvamia Hifadhi za Misitu
 Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu wakati wa mkutano huo wa hadhara.

 Mkazi wa kata ya Mgusu, Anaeli Mbokile akizungumza mbele ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiwasilisha ombi  la kumegewa eneo la Hifadhi ya Msitu Geita ili liweze kutumika kwa ajili ya malisho na makazi baada ya wakazi wa kata ya Mgusu idadi ya kuongezeka.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiteta jamabo na baadhi ya wanachama wa CCM  wakati alipomaliza mkutano wa hadhara katika  kata ya Mgusu mkoani Geita. 

Sunday, December 30, 2018




NAIBU WAZIRI MHE.KANYASU AWATAKA WANANCHI WANAOISHI NDANI YA HIFADHI YA MISITU KULIPA TOZO BILA SHURUTI

NA LUSUNGU HELELA-MWANZA

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Costantine Kanyasu amewataka wananchi wanaoishi na kufanya shughuli za uzalishaji mali ndani  ya Hifadhi ya misitu ya Visiwa vya  Kome  na Maisome vilivyoko wilayani Sengerema mkoa wa Mwanza kulipa tozo za serikali bila kulazimishwa.



Kauli hiyo ameitoa  wakati alipokuwa akizungumza na wakazi wanaoishi ndani ya Hifadhi ya  Msitu wa Shigala ulioko Kome Mchangani ambayo ni kambi ya wavuvi wakati alipofanya ziara ya kutatua kero zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.



Mbunge wa Jimbo la Buchosa Dkt. Charles Tizeba amemueleza  Naibu Waziri hiyo kuwa kumekuwepo na changamoto ya ulipaji  tozo kubwa hata kama mtu ana eneo dogo na ndipo wananchi walilazimika kugoma kulipa tozo hiyo kwa lengo la kupata msaada zaidi.



Amefafanua kuwa mtu anayemiliki hekari moja  anatakiwa kulipa Tsh.425,000 kwa mwaka lakini hata mtu anayemikili eneo dogo la mita 20 naye anatakiwa kulipa kama wa hekari moja  kitendo kilichowafanya wananchi hao kushindwa kulipa na kusubili maelekezo ya wizara husika.



Mmoja wa wananchi wanaoishi ndani ya Hifadhi hiyo,Juma Ramadhani amemwomba Naibu Waziri kuangalia upya sheria hiyo ili wananchi wapate nafuu ya kulipa na serikali iweze kupata mapato yake.



Kaimu Meneja wa TFS Kanda ya Ziwa, Thomas Moshi amesema kuwa tozo hizo zipo kwa mujibu wa sheria kinachotakiwa ni wananchi kulipa na siyo kugomea kulipa tozo hizo na wanapofanya hivyo wanakwenda kinyume na matakwa ya sheria ya hifadhi ya misitu.



Kanyasu amewahakikishia wananchi hao kuwa suala hilo atalipatia majibu kwa haraka lakini amewataka watu wanaomiliki hekari moja  kulipa tozo hizo kwa wakati na wale wenye maeneo madogo madogo wajiunge katika vikundi ili waweze kuilipa pesa hiyo



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Costantine Kanyasu akizungumza na  wananchi wanaoishi na kufanya shughuli za uzalishaji mali ndani  ya Hifadhi ya msitu ya Kisiwa cha  Kome Mchangani ambayo ni Kambi ya Uvuvi iliyopo wilayani Sengerema mkoa wa Mwanza wakinyoosha mikono ikiwa ni ishara ya kukubali kuwa watalipa tozo za serikali bila kulazimishwa alipofanya ziara ya kutatua kero zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.
Mbunge wa Jimbo la Buchosa, Mhe. Dkt. Charles Tizeba akizungumza na wananchi wa Jimboni kwake  kwenye mkutano wa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu wa   kutatua kero za  wananchi wanaoishi ndani ya  Hifadhi ya msitu ya Kisiwa cha  Kome Mchangani ambayo ni Kambi ya Uvuvi iliyopo wilayani Sengerama mkoani Mwanza wakati wa mkutano wa hadhara uliofanya  Kome Mchangani

Mwenyekiti wa Kijiji cha Buhama kata ya Buhama, Thomas Sabuni, akizungumza  na wananchi kwenye mkutano wa hadhara kabala ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu kwa ajili ya kuzungumza na wananchi ikiwa lengo  kutatua kero za  wananchi  wa Kisiwa hicho wilaya ya Sengerama mkoani Mwanza wakati wa mkutano wa hadhara uliofanya  katika eneo la Kome mchangani
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Costantine Kanyasu akiteta jambo na Meneja wa Shamba la Buhindi , Ayoub Kigongwira wakati wa  mkutano wa hadhara uliofanyika katika Hifadhi ya msitu ya Kisiwa cha  Kome Mchangani ambayo ni Kambi ya wavuvi wakati alipofanya ziara ya kutatua kero zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.

Baadhi  ya wananchi wakifuatilia mkutano wa hadhara wa  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Costantine Kanyasu ndani  ya Hifadhi ya msitu ya Kisiwa cha  Kome Mchangani ambayo ni Kambi ya wavuvi wakati alipofanya ziara ya kutatua kero zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu (katikati) akiwa na baadhi ya viongozi wa kijiji cha Buhama  wakati alipowasili katika Hifadhi ya msitu ya Kisiwa cha  Kome Mchangani ambayo ni Kambi ya wvuvi kwa ajili ya  kutatua kero zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akiiangalia taarifa mara baada ya kukabidhiwa taarifa Mwenyekiti wa kijiji Buhama, Thomas Sabuni  wakati alipowasili katika Hifadhi ya msitu ya Kisiwa cha  Kome Mchangani ambayo ni Kambi ya wvuvi kwa ajili ya  kutatua kero zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo




Saturday, December 8, 2018

MHE KANYASU AENDESHA HARAMBEE YA KUCHANGIA UJENZI WA KITUO CHA AFYA


 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu ( wa pili kushoto)  akizungumza mara baada ya ibada iliyofanyika katika ya Kanisa la Wasabato la Geita kati wakati ya harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo  afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita


Baadhi ya waumini ibada wa Kanisa la Wasabato la Geita kati wakifuatilia ibada kabla  ya  harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo  afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita


 Mchungaji na  Mwenyekiti wa South Nyanza Conference, Sadoki Butoke akitoa mahubiri kwa  waumini waliojumuika katika ibada ya  harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo  afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita.

 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu (katikati) akiwa na baadhi ya watendaji wa mkoa wa Geita pamoja na viongozi wa  Kanisa la Wasabato la Geita wakisikiliza mahubiri kabla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo  afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita
Baadhi ya wanakwaya wakiimba wakati wa mahubiri kabla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo  afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita.

   Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akivishwa skafu na wanafunzi wa Skauti kanisa la Wasabato la Geita Kati kabla  ya Naibu Waziri huyo kuendesha harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo  afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiwa kwenye picha ya pamoja  na kamati ya Ulinzi na usalama ya mkoa wa Geita mara baada ya kusomewa taarifa ya hali ya uhifadhi wa misitu na wanyamapori kabala ya kushirikia harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo cha Afya