slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Monday, February 4, 2019



MANGI MELI REMAINS In Old Moshi the head of Chief Meli is missing. A strong figure of resistance, he fought bravely against the German colonialists and was hanged in 1900. His head is said to have been shipped to Germany, where thousands of human skulls are still stored in museum depots. The grandson of Chief Meli has been searching for the head for more than 50 years, until now without success. Yet traces of Chief Meli can be found in songs, stories and archives. This has formed the basis for a Tanzanian-German collaboration where an animated video sculpture and re-examined historical photographs portray the life story of Meli – and his legacy today. Mangi Meli Remains premiered in Berlin, November 2018 and will display in Dar es Salaam before concluding in Old Moshi, March 2019 where it will remain as a place of remembrance and a placeholder for Chief Meli’s missing head. A Flinn Works (DE) production with Mr. Isaria Meli (TZ), Old Moshi Cultural Tourism (TZ), BSS Projects (TZ/UK), ArtEver (TZ) in cooperation with Ethnologisches Museum Berlin and Tieranatomisches Theater at Humboldt University Berlin. Supported by Senatsverwaltung für Kultur und Europa, Goethe Institute Tanzania and Between Bridges.


Tuesday, January 1, 2019


NAIBU WAZIRI MHE,KANYASU AWAFUNDA WATUMISHI WA  TFS PAMOJA NA WANANCHI


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu amewaonya wananchi  wanaofanya shughuli za kibinadamu ndani ya Hifadhi za Misitu nchini kuacha tabia ya kuwashambulia Watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wanapokuwa wanatekeleza majukumu yao.

Onyo hili linakuja ikiwa zaidi ya watumishi watano wa TFS  katika mikoa ya Pwani, Tabora ,Kigoma pamoja Kilimanjaro wakiwa wamepoteza maisha yao kwa kushambuliwa na wananchi wakati wakiwa wanatekeleza majukumu yao.

Aidha, Mhe.Kanyasu amewapiga marufuku watumishi wa TFS kujichukulia sheria mkononi kwa kuwapiga wananchi wanapobainika kutenda makosa.

"Watumishi wa TFS hamruhusiwi   kumpiga Mwananchi mnapomkamata ndani ya Hifadhi au akiwa anasafirisha mazao ya Misitu kinyume na sheria, atakayebainika sheria itachukua mkondo wake.

Ametoa  onyo hilo wakati akizungumza na wananchi  kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika  katika kata ya Mgusu  wilayani  Geita mkoani Geita ikiwa ni ziara yake ya kutatua migogoro ya mipaka kwenye msitu wa Hifadhi Geita iliyopo baina ya Vijiji ambapo jumla ya hekta 4,462.95 zimefutwa kwa tangazo la Serikali.


Amesema shughuli za uhifadhi ni lazima zifanyike kwa ushirikishwaji kati ya wananchi na watumishi wa TFS.

" Uhasama unaozidi kujengeka kati yenu  hauna tija katika uhifadhi shirikianeni" amesisitiza Mhe.Kanyasu.

Aidha,  Mhe . Kanyasu amewataka wananchi kuheshimu na kuzifuata sheria za uhifadhi ya Misitu nchini huku akiwataka  watumishi kujiepusha na migongano kati yao na wananchi.

Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu amewataka wananchi wafuate sheria kwa kulipia vibali kwa TFS pale wanapokuwa na mahitaji ya mazao ya Misitu badala ya kusubilia mpaka wakamatwe.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe.Josephat Maganga amemueleza Naibu Waziri huyo kuwa hali ya Misitu katika wilaya hiyo ni mbaya kufuatia shughuli za kibinadamu zinazoendelea kufanyika Misitu hiyo.

Hata hivyo, Mkuu huyo wa Wilaya  hiyo Mhe.Maganga alisema kufuatia hali hiyo tayari  Kamati ya Ulinzi na Usalama kwa kushirikiana TFS wameshaanza kufanya  doria ya kuwaondoa wafugaji na wakulima waliovamia  Hifadhi.

Katika hatua nyingine, Diwani ya Kata ya Mgusu, Pastory Lugusa amemuomba  Naibu Waziri huyo kumegewa eneo la Hifadhi  kwa vile idadi ya wakazi wa kata hiyo imeongezeka hali inayopelea kukosa maeneo kwa ajili  ya malisho na Kilimo.

Kwa upande wake Meneja wa Misitu  wa  wilaya wa TFS, Fedy Ndandika amemuhakikishia Naibu Waziri kuwa  watashirikiana na wananchi hata hivyo tayari wameanza kutoa elimu ya umuhimu wa uhifadhi kwa jamii zinazozunguka Hifadhi


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu  akiwa na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Geita mkoani Geita akipewa maelezo na Meneja wa Misitu  wa  wilaya wa Wakala wa Huduma ya Misitu Tanzania (TFS) Fedy Ndandika wakati alipotembelea eneo la Manga lililokuwa limevamiwa na wakulima ambayo ni moja ya eneo la Msitu wa Hifadhi  Geita
 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akizungumza na wananchi  kwenye mkutano wa hadhara katika kata ya Mgusu, Halmashauri ya wilaya ya  Geita mkoani Geita akiwasisitiza wananchi umuhimu wakufuata  sheria na kuacha tabia ya kuvamia Hifadhi za Misitu
 Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu wakati wa mkutano huo wa hadhara.

 Mkazi wa kata ya Mgusu, Anaeli Mbokile akizungumza mbele ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiwasilisha ombi  la kumegewa eneo la Hifadhi ya Msitu Geita ili liweze kutumika kwa ajili ya malisho na makazi baada ya wakazi wa kata ya Mgusu idadi ya kuongezeka.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiteta jamabo na baadhi ya wanachama wa CCM  wakati alipomaliza mkutano wa hadhara katika  kata ya Mgusu mkoani Geita. 

Sunday, December 30, 2018




NAIBU WAZIRI MHE.KANYASU AWATAKA WANANCHI WANAOISHI NDANI YA HIFADHI YA MISITU KULIPA TOZO BILA SHURUTI

NA LUSUNGU HELELA-MWANZA

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Costantine Kanyasu amewataka wananchi wanaoishi na kufanya shughuli za uzalishaji mali ndani  ya Hifadhi ya misitu ya Visiwa vya  Kome  na Maisome vilivyoko wilayani Sengerema mkoa wa Mwanza kulipa tozo za serikali bila kulazimishwa.



Kauli hiyo ameitoa  wakati alipokuwa akizungumza na wakazi wanaoishi ndani ya Hifadhi ya  Msitu wa Shigala ulioko Kome Mchangani ambayo ni kambi ya wavuvi wakati alipofanya ziara ya kutatua kero zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.



Mbunge wa Jimbo la Buchosa Dkt. Charles Tizeba amemueleza  Naibu Waziri hiyo kuwa kumekuwepo na changamoto ya ulipaji  tozo kubwa hata kama mtu ana eneo dogo na ndipo wananchi walilazimika kugoma kulipa tozo hiyo kwa lengo la kupata msaada zaidi.



Amefafanua kuwa mtu anayemiliki hekari moja  anatakiwa kulipa Tsh.425,000 kwa mwaka lakini hata mtu anayemikili eneo dogo la mita 20 naye anatakiwa kulipa kama wa hekari moja  kitendo kilichowafanya wananchi hao kushindwa kulipa na kusubili maelekezo ya wizara husika.



Mmoja wa wananchi wanaoishi ndani ya Hifadhi hiyo,Juma Ramadhani amemwomba Naibu Waziri kuangalia upya sheria hiyo ili wananchi wapate nafuu ya kulipa na serikali iweze kupata mapato yake.



Kaimu Meneja wa TFS Kanda ya Ziwa, Thomas Moshi amesema kuwa tozo hizo zipo kwa mujibu wa sheria kinachotakiwa ni wananchi kulipa na siyo kugomea kulipa tozo hizo na wanapofanya hivyo wanakwenda kinyume na matakwa ya sheria ya hifadhi ya misitu.



Kanyasu amewahakikishia wananchi hao kuwa suala hilo atalipatia majibu kwa haraka lakini amewataka watu wanaomiliki hekari moja  kulipa tozo hizo kwa wakati na wale wenye maeneo madogo madogo wajiunge katika vikundi ili waweze kuilipa pesa hiyo



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Costantine Kanyasu akizungumza na  wananchi wanaoishi na kufanya shughuli za uzalishaji mali ndani  ya Hifadhi ya msitu ya Kisiwa cha  Kome Mchangani ambayo ni Kambi ya Uvuvi iliyopo wilayani Sengerema mkoa wa Mwanza wakinyoosha mikono ikiwa ni ishara ya kukubali kuwa watalipa tozo za serikali bila kulazimishwa alipofanya ziara ya kutatua kero zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.
Mbunge wa Jimbo la Buchosa, Mhe. Dkt. Charles Tizeba akizungumza na wananchi wa Jimboni kwake  kwenye mkutano wa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu wa   kutatua kero za  wananchi wanaoishi ndani ya  Hifadhi ya msitu ya Kisiwa cha  Kome Mchangani ambayo ni Kambi ya Uvuvi iliyopo wilayani Sengerama mkoani Mwanza wakati wa mkutano wa hadhara uliofanya  Kome Mchangani

Mwenyekiti wa Kijiji cha Buhama kata ya Buhama, Thomas Sabuni, akizungumza  na wananchi kwenye mkutano wa hadhara kabala ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu kwa ajili ya kuzungumza na wananchi ikiwa lengo  kutatua kero za  wananchi  wa Kisiwa hicho wilaya ya Sengerama mkoani Mwanza wakati wa mkutano wa hadhara uliofanya  katika eneo la Kome mchangani
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Costantine Kanyasu akiteta jambo na Meneja wa Shamba la Buhindi , Ayoub Kigongwira wakati wa  mkutano wa hadhara uliofanyika katika Hifadhi ya msitu ya Kisiwa cha  Kome Mchangani ambayo ni Kambi ya wavuvi wakati alipofanya ziara ya kutatua kero zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.

Baadhi  ya wananchi wakifuatilia mkutano wa hadhara wa  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Costantine Kanyasu ndani  ya Hifadhi ya msitu ya Kisiwa cha  Kome Mchangani ambayo ni Kambi ya wavuvi wakati alipofanya ziara ya kutatua kero zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu (katikati) akiwa na baadhi ya viongozi wa kijiji cha Buhama  wakati alipowasili katika Hifadhi ya msitu ya Kisiwa cha  Kome Mchangani ambayo ni Kambi ya wvuvi kwa ajili ya  kutatua kero zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akiiangalia taarifa mara baada ya kukabidhiwa taarifa Mwenyekiti wa kijiji Buhama, Thomas Sabuni  wakati alipowasili katika Hifadhi ya msitu ya Kisiwa cha  Kome Mchangani ambayo ni Kambi ya wvuvi kwa ajili ya  kutatua kero zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo




Saturday, December 8, 2018

MHE KANYASU AENDESHA HARAMBEE YA KUCHANGIA UJENZI WA KITUO CHA AFYA


 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu ( wa pili kushoto)  akizungumza mara baada ya ibada iliyofanyika katika ya Kanisa la Wasabato la Geita kati wakati ya harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo  afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita


Baadhi ya waumini ibada wa Kanisa la Wasabato la Geita kati wakifuatilia ibada kabla  ya  harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo  afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita


 Mchungaji na  Mwenyekiti wa South Nyanza Conference, Sadoki Butoke akitoa mahubiri kwa  waumini waliojumuika katika ibada ya  harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo  afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita.

 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu (katikati) akiwa na baadhi ya watendaji wa mkoa wa Geita pamoja na viongozi wa  Kanisa la Wasabato la Geita wakisikiliza mahubiri kabla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo  afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita
Baadhi ya wanakwaya wakiimba wakati wa mahubiri kabla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo  afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita.

   Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akivishwa skafu na wanafunzi wa Skauti kanisa la Wasabato la Geita Kati kabla  ya Naibu Waziri huyo kuendesha harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo  afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiwa kwenye picha ya pamoja  na kamati ya Ulinzi na usalama ya mkoa wa Geita mara baada ya kusomewa taarifa ya hali ya uhifadhi wa misitu na wanyamapori kabala ya kushirikia harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo cha Afya

Saturday, October 20, 2018

NAIBU WAZIRI MHE. JAPHET HASUNGA AONYA UKATAJI MITI OVYO MKOANI SONGWE

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga akizungumza jana na wananchi kuhusu athari za ukataji miti ovyo  kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Isalalo kata ya Wasa wilayani Mbozi katika mkoa wa Songwe





NAIBU WAZIRI MHE. JAPHET HASUNGA AONYA UKATAJI MITI OVYO MKOANI SONGWE

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Japhet Hasunga amewaonya watu wenye tabia ya kukata miti ovyo kuwa Serikali hatosita kuwachukulia hatua za kisheria kutokana na kushamiri kwa uharibifu wa misitu mkoani Songwe.

Ametoa onyo hilo wakati alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Isalalo kata ya Wasa wilayani Mbozi katika mkoa wa Songwe.

Amesema kufuatia kasi ya ukataji miti ovyo unaoendelea  kwa ajili ya mbao na nishati ya mkaa katika maeneo hayo kunatishia kutoweka kwa mvua wanayoitegemea kwa ajili kilimo cha mazao ya kahawa, mahindi pamoja na mazao mengine.

Amewaeleza Wananchi hao  kuwa uharibifu huo ukiendelea utaawathiri wao wenyewe  kwa vile   mvua itakoma kunyesha katika maeneo yao.

Amewataka wakikata mti wapande miti na wale wanaokata miti kwa ajili ya Nishati ya mkaa wafuate kanuni na sheria ili kuepuka kukabiliana na Wakala wa Huduma za Misitu  Tanzania (TFS)

Aidha, Mhe. Hasunga Amewataka Wananchi hao kuwa  hata pale inapotokea wanataka kukata mti wa mwembe uliopo katika nyumba zao wanatakiwa kuomba kibali kutoka TFS.

Pia,  Waziri Hasunga amewaagiza TFS itoe miche 10,000 kwa Kata ya Wasa msimu wa mvua utakapokaribia kufuatia ombi la mwanakijji Kasian Mwanjala alilowasilisha kwa Mhe. Hasunga kuwa wanataka kupanda miti ili wanakosa miche.

"Moja ya ahadi yangu niliyoitoa kwenu ni kuhakikisha katika jimbo langu wananchi mnapata umeme, hadi sasa tayari nguzo za umeme zimeanza kuwekwa " amesema Mhe Hasunga.



 Baadhi ya Watendaji aliokuwa ameongozana nao katika mkutano huo wa hadhara katika kijiji cha Isalalo



Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga akimsikiliza huku akiwa anaandika swali analoulizwa na zungumza Ester Mwakanja kuhusiana  athari za ukataji miti ovyo  kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Isalalo kata ya Wasa wilayani Mbozi katika mkoa wa Songwe

    Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga akisoma baadhi ya ujumbe katika  karatasi  mara baada ya kumaliza mkutano wa hadhara ulioufanya katika kijiji cha Isalalo kata ya Wasa wilayani Mbozi katika mkoa wa Songwe









Sunday, October 14, 2018

TFS YAHAMASISHA UTALII WA KIIKOLOJIA KWA WATANZANIA

Afisa Misitu Mkuu kutoka Wakala wa Huduma za Misitu nchini(TFS),Arijanso Mlog akizungumza na Waandishi wa habari katika Onesho la Kimataifa la  Utalii (SITE)linaloendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.



Wafanyakazi wa Huduma za Misitu nchini TFS, Wakiwaonesha wadau Mazao Mbalimbali yatokanayo na misitu ambayo ni mazuri kwa ajili ya kuimarisha afya ya Mwanadamu
Meneja Masoko na Uwekezaji wa Wakala wa Huduma za Misitu Nchini, Mariam Kobelo akieleza huduma za kitalii zilizopo ndani ya Hifadhi za Misitu zilizo chini ya TFS

Afisa Misitu Mwandamizi , Anna Lawuo Akizungumza na Waandishi wa habari  kuhusu umuhimu wa mazao yatokanayo na misitu nchini


TFS YAHAMASISHA  UTALII WA KIIKOLOJIA KWA                                      WATALII
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) imetoa wito kwa watanzania kutembelea Maeneo yaliyohifadhiwa ili kuweza kujionea namna ikolojia na uhifadhi katika misitu hiyo ilivyo na faida kwa viumbe hai na Wanadamu.



Akizungumza na Waandishi wa Habari,  Afisa Misitu Mkuu kutoka Wakala wa Huduma za Misitu nchini(TFS),Arijanso Mlog  katika Onesho la Kimataifa la  Utalii lijulikanalo kama Swahili  International Tourism Expo (SITE) linaloendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam, Mlog amesema kuwa watu wanapaswa kutemblea misitu hii ili waweze kujionea na kujifunza umuhimu wa ikolojia katika hifadhi.




"Ni vyema watu wakaja wakatembelea hifadhi ya misitu ya Amani waweze kujionea namna Misitu iliyopakana na makazi ya watu na maporoko ya maji ambayo hayakauki muda wote na kujionea maua ambayo yanaaminika katika imani kuwa ndio yalitumika wakati wa kristo na watu husafiri kutoka sehemu mbalimbali  kuyafuata kutoka maeneo ya mbali"amesema Mlog.




Kwa upande wake, Meneja Masoko na Uwekezaji wa Wakala wa Huduma za Misitu Nchini, Mariam Kobelo amewataka wdau mbalimbali  kutembelea banda lao lililopo katika   Onesho La Kimataifa la Utalii la SITE linaloendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam ili kujionea huduma zitolewazo na TFS na kujua wapi wanaweza kutembelea kwa ajili ya mapumziko yao.


Mariamu amesema kuwa Misitu inayohifadhiwa na TFS ina upekee sana , Hivyo ametoa wito kwa wanafunzi, wanasayansi na wanataaluma mbalimbali kuwa wanaweza kwenda ili kuweza  kufanyia tafiti, Mapumziko kwa wana ndoa pia wanaweza kwenda kutembea na  familia zao .




Thursday, October 11, 2018

NAIBU WAZIRI, MHE.JAPHET HASUNGA AFANYA ZIARA CHUO CHA TAIFA CHA UTALII

Add caption1.       Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (katikati) akiwa  na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka  wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Chuo mara katika Kampasi ya Bustanini   jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga(wa pili kushoto)  akizungumza na watumishi wa chuo hicho katika Kampasi ya Bustanini , jijini Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka



 Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga(wa pili kushoto)  akizungumza na watumishi wa chuo hicho katika Kampasi ya Bustanini , jijini Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka


1Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga(kulia) akizungumza na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka(kushoto)  mara baada ya Naibu Waziri huyo kufanya ziara katika chuo ambapo alizungumza na watumishi wa chuo hicho katika Kampasi ya Temeke, jijini Dar es Salaam.



Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga(kulia) akiwa ameongoza na  Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka(kushoto)  mara baada ya Naibu Waziri huyo kufanya ziara katika chuo  hicho katika Kampasi ya Temeke, jijini Dar es Salaam.



 1.       Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga(katikati) akipewa maelezo na  Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka(kushoto) kuhusiana na vyumba vipya vya kulala wageni  vilianzishwa katika chuo hicho  mara baada ya Naibu Waziri huyo kufanya ziara katika chuo  hicho katika Kampasi ya Bustanini  jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga(katikati) akipewa maelezo na  Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Sedoyeka(kushoto) kuhusiana na vyumba vipya vya kulala wageni  vilianzishwa katika chuo hicho  mara baada ya Naibu Waziri huyo kufanya ziara katika chuo  hicho katika Kampasi ya Bustanini  jijini Dar es Salaam.