MANGI MELI REMAINS In Old
Moshi the head of Chief Meli is missing. A strong figure of resistance, he
fought bravely against the German colonialists and was hanged in 1900. His head
is said to have been shipped to Germany, where thousands of human skulls are
still stored in museum depots. The grandson of Chief Meli has been searching
for the head for more than 50 years, until now without success. Yet traces of
Chief Meli can be found in songs, stories and archives. This has formed the
basis for a Tanzanian-German collaboration where an animated video sculpture
and re-examined historical photographs portray the life story of Meli – and his
legacy today. Mangi Meli Remains premiered in Berlin, November 2018 and will
display in Dar es Salaam before concluding in Old Moshi, March 2019 where it
will remain as a place of remembrance and a placeholder for Chief Meli’s
missing head. A Flinn Works (DE) production with Mr. Isaria Meli (TZ), Old
Moshi Cultural Tourism (TZ), BSS Projects (TZ/UK), ArtEver (TZ) in cooperation
with Ethnologisches Museum Berlin and Tieranatomisches Theater at Humboldt
University Berlin. Supported by Senatsverwaltung für Kultur und Europa, Goethe
Institute Tanzania and Between Bridges.
slider gif
kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ
Monday, February 4, 2019
Tuesday, January 1, 2019
NAIBU WAZIRI MHE,KANYASU AWAFUNDA WATUMISHI WA TFS PAMOJA NA WANANCHI
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu amewaonya
wananchi wanaofanya shughuli za
kibinadamu ndani ya Hifadhi za Misitu nchini kuacha tabia ya kuwashambulia
Watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wanapokuwa wanatekeleza
majukumu yao.
Onyo hili linakuja ikiwa zaidi ya watumishi watano wa TFS katika mikoa ya Pwani, Tabora ,Kigoma pamoja
Kilimanjaro wakiwa wamepoteza maisha yao kwa kushambuliwa na wananchi wakati
wakiwa wanatekeleza majukumu yao.
Aidha, Mhe.Kanyasu amewapiga marufuku watumishi wa TFS kujichukulia
sheria mkononi kwa kuwapiga wananchi wanapobainika kutenda makosa.
"Watumishi wa TFS hamruhusiwi
kumpiga Mwananchi mnapomkamata ndani ya Hifadhi au akiwa anasafirisha
mazao ya Misitu kinyume na sheria, atakayebainika sheria itachukua mkondo wake.
Ametoa onyo hilo wakati
akizungumza na wananchi kwenye mkutano
wa hadhara uliofanyika katika kata ya
Mgusu wilayani Geita mkoani Geita ikiwa ni ziara yake ya
kutatua migogoro ya mipaka kwenye msitu wa Hifadhi Geita iliyopo baina ya
Vijiji ambapo jumla ya hekta 4,462.95 zimefutwa kwa tangazo la Serikali.
Amesema shughuli za uhifadhi ni lazima zifanyike kwa ushirikishwaji kati
ya wananchi na watumishi wa TFS.
" Uhasama unaozidi kujengeka kati yenu hauna tija katika uhifadhi shirikianeni"
amesisitiza Mhe.Kanyasu.
Aidha, Mhe . Kanyasu amewataka
wananchi kuheshimu na kuzifuata sheria za uhifadhi ya Misitu nchini huku
akiwataka watumishi kujiepusha na
migongano kati yao na wananchi.
Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu amewataka wananchi wafuate sheria kwa
kulipia vibali kwa TFS pale wanapokuwa na mahitaji ya mazao ya Misitu badala ya
kusubilia mpaka wakamatwe.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe.Josephat Maganga amemueleza
Naibu Waziri huyo kuwa hali ya Misitu katika wilaya hiyo ni mbaya kufuatia
shughuli za kibinadamu zinazoendelea kufanyika Misitu hiyo.
Hata hivyo, Mkuu huyo wa Wilaya
hiyo Mhe.Maganga alisema kufuatia hali hiyo tayari Kamati ya Ulinzi na Usalama kwa kushirikiana
TFS wameshaanza kufanya doria ya
kuwaondoa wafugaji na wakulima waliovamia
Hifadhi.
Katika hatua nyingine, Diwani ya Kata ya Mgusu, Pastory Lugusa
amemuomba Naibu Waziri huyo kumegewa
eneo la Hifadhi kwa vile idadi ya wakazi
wa kata hiyo imeongezeka hali inayopelea kukosa maeneo kwa ajili ya malisho na Kilimo.
Kwa upande wake Meneja wa Misitu wa
wilaya wa TFS, Fedy Ndandika amemuhakikishia Naibu Waziri kuwa watashirikiana na wananchi hata hivyo tayari
wameanza kutoa elimu ya umuhimu wa uhifadhi kwa jamii zinazozunguka Hifadhi
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara katika kata ya Mgusu, Halmashauri ya wilaya ya Geita mkoani Geita akiwasisitiza wananchi umuhimu wakufuata sheria na kuacha tabia ya kuvamia Hifadhi za Misitu
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu wakati wa mkutano huo wa hadhara.
Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akiteta jamabo na baadhi
ya wanachama wa CCM wakati alipomaliza
mkutano wa hadhara katika kata ya Mgusu
mkoani Geita.
Sunday, December 30, 2018
NAIBU
WAZIRI MHE.KANYASU AWATAKA WANANCHI WANAOISHI NDANI YA HIFADHI YA MISITU KULIPA
TOZO BILA SHURUTI
NA
LUSUNGU HELELA-MWANZA
Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Costantine Kanyasu amewataka wananchi
wanaoishi na kufanya shughuli za uzalishaji mali ndani ya Hifadhi ya misitu ya Visiwa vya Kome
na Maisome vilivyoko wilayani Sengerema mkoa wa Mwanza kulipa tozo za
serikali bila kulazimishwa.
Kauli
hiyo ameitoa wakati alipokuwa
akizungumza na wakazi wanaoishi ndani ya Hifadhi ya Msitu wa Shigala ulioko Kome Mchangani ambayo
ni kambi ya wavuvi wakati alipofanya ziara ya kutatua kero zinazowakabili
wananchi wa maeneo hayo.
Mbunge
wa Jimbo la Buchosa Dkt. Charles Tizeba amemueleza Naibu Waziri hiyo kuwa kumekuwepo na
changamoto ya ulipaji tozo kubwa hata
kama mtu ana eneo dogo na ndipo wananchi walilazimika kugoma kulipa tozo hiyo
kwa lengo la kupata msaada zaidi.
Amefafanua
kuwa mtu anayemiliki hekari moja
anatakiwa kulipa Tsh.425,000 kwa mwaka lakini hata mtu anayemikili eneo
dogo la mita 20 naye anatakiwa kulipa kama wa hekari moja kitendo kilichowafanya wananchi hao kushindwa
kulipa na kusubili maelekezo ya wizara husika.
Mmoja
wa wananchi wanaoishi ndani ya Hifadhi hiyo,Juma Ramadhani amemwomba Naibu
Waziri kuangalia upya sheria hiyo ili wananchi wapate nafuu ya kulipa na
serikali iweze kupata mapato yake.
Kaimu
Meneja wa TFS Kanda ya Ziwa, Thomas Moshi amesema kuwa tozo hizo zipo kwa
mujibu wa sheria kinachotakiwa ni wananchi kulipa na siyo kugomea kulipa tozo
hizo na wanapofanya hivyo wanakwenda kinyume na matakwa ya sheria ya hifadhi ya
misitu.
Kanyasu
amewahakikishia wananchi hao kuwa suala hilo atalipatia majibu kwa haraka
lakini amewataka watu wanaomiliki hekari moja
kulipa tozo hizo kwa wakati na wale wenye maeneo madogo madogo wajiunge
katika vikundi ili waweze kuilipa pesa hiyo
Saturday, December 8, 2018
MHE KANYASU AENDESHA HARAMBEE YA KUCHANGIA UJENZI WA KITUO CHA AFYA
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,
Mhe.Constantine Kanyasu ( wa pili kushoto) akizungumza mara baada ya ibada iliyofanyika
katika ya Kanisa la Wasabato la Geita kati wakati ya harambee ya kuchangia
ujenzi wa kituo afya kinachotarajiwa
kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita
Baadhi ya waumini ibada wa Kanisa la Wasabato la
Geita kati wakifuatilia ibada kabla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya
Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita
Mchungaji na Mwenyekiti wa South Nyanza Conference, Sadoki Butoke akitoa mahubiri kwa waumini waliojumuika katika ibada ya harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita.
Baadhi ya wanakwaya wakiimba wakati wa mahubiri kabla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo afya kinachotarajiwa kujengwa katika kata ya Bombambili eneo la Magogo mkoani Geita.
Saturday, October 20, 2018
NAIBU WAZIRI MHE. JAPHET HASUNGA AONYA UKATAJI MITI OVYO MKOANI SONGWE
Naibu Waziri wa
Maliasili na Utalii, Mhe.Japhet Hasunga amewaonya watu wenye tabia ya kukata
miti ovyo kuwa Serikali hatosita kuwachukulia hatua za kisheria kutokana na
kushamiri kwa uharibifu wa misitu mkoani Songwe.
Ametoa onyo hilo
wakati alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha
Isalalo kata ya Wasa wilayani Mbozi katika mkoa wa Songwe.
Amesema kufuatia kasi
ya ukataji miti ovyo unaoendelea kwa ajili ya mbao na nishati ya mkaa
katika maeneo hayo kunatishia kutoweka kwa mvua wanayoitegemea kwa ajili kilimo
cha mazao ya kahawa, mahindi pamoja na mazao mengine.
Amewaeleza Wananchi
hao kuwa uharibifu huo ukiendelea utaawathiri wao wenyewe kwa
vile mvua itakoma kunyesha katika maeneo yao.
Amewataka wakikata mti
wapande miti na wale wanaokata miti kwa ajili ya Nishati ya mkaa wafuate kanuni
na sheria ili kuepuka kukabiliana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania
(TFS)
Aidha, Mhe. Hasunga
Amewataka Wananchi hao kuwa hata pale inapotokea wanataka kukata mti wa
mwembe uliopo katika nyumba zao wanatakiwa kuomba kibali kutoka TFS.
Pia, Waziri
Hasunga amewaagiza TFS itoe miche 10,000 kwa Kata ya Wasa msimu wa mvua
utakapokaribia kufuatia ombi la mwanakijji Kasian Mwanjala alilowasilisha kwa
Mhe. Hasunga kuwa wanataka kupanda miti ili wanakosa miche.
"Moja ya ahadi
yangu niliyoitoa kwenu ni kuhakikisha katika jimbo langu wananchi mnapata
umeme, hadi sasa tayari nguzo za umeme zimeanza kuwekwa " amesema Mhe
Hasunga.
Sunday, October 14, 2018
TFS YAHAMASISHA UTALII WA KIIKOLOJIA KWA WATANZANIA
| Wafanyakazi wa Huduma za Misitu nchini TFS,
Wakiwaonesha wadau Mazao Mbalimbali yatokanayo na misitu ambayo ni mazuri kwa
ajili ya kuimarisha afya ya Mwanadamu |
| Meneja Masoko na Uwekezaji wa Wakala wa Huduma za Misitu Nchini, Mariam Kobelo akieleza huduma za kitalii zilizopo ndani ya Hifadhi za Misitu zilizo chini ya TFS |
| Afisa Misitu Mwandamizi , Anna Lawuo Akizungumza
na Waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa mazao yatokanayo na misitu
nchini |
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) imetoa wito kwa watanzania kutembelea Maeneo yaliyohifadhiwa ili kuweza kujionea namna ikolojia na uhifadhi katika misitu hiyo ilivyo na faida kwa viumbe hai na Wanadamu.
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Afisa Misitu Mkuu kutoka Wakala wa Huduma za Misitu nchini(TFS),Arijanso Mlog katika Onesho la Kimataifa la Utalii lijulikanalo kama Swahili International Tourism Expo (SITE) linaloendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam, Mlog amesema kuwa watu wanapaswa kutemblea misitu hii ili waweze kujionea na kujifunza umuhimu wa ikolojia katika hifadhi.
"Ni vyema watu wakaja wakatembelea hifadhi ya misitu ya Amani waweze kujionea namna Misitu iliyopakana na makazi ya watu na maporoko ya maji ambayo hayakauki muda wote na kujionea maua ambayo yanaaminika katika imani kuwa ndio yalitumika wakati wa kristo na watu husafiri kutoka sehemu mbalimbali kuyafuata kutoka maeneo ya mbali"amesema Mlog.
Kwa upande wake, Meneja Masoko na Uwekezaji wa Wakala wa Huduma za Misitu Nchini, Mariam Kobelo amewataka wdau mbalimbali kutembelea banda lao lililopo katika Onesho La Kimataifa la Utalii la SITE linaloendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam ili kujionea huduma zitolewazo na TFS na kujua wapi wanaweza kutembelea kwa ajili ya mapumziko yao.
Mariamu amesema kuwa Misitu inayohifadhiwa na TFS ina upekee sana , Hivyo ametoa wito kwa wanafunzi, wanasayansi na wanataaluma mbalimbali kuwa wanaweza kwenda ili kuweza kufanyia tafiti, Mapumziko kwa wana ndoa pia wanaweza kwenda kutembea na familia zao .
Thursday, October 11, 2018
NAIBU WAZIRI, MHE.JAPHET HASUNGA AFANYA ZIARA CHUO CHA TAIFA CHA UTALII
Subscribe to:
Posts (Atom)



























