slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Wednesday, January 25, 2017

TAARIFA KWA UMMA: KUWASILISHA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA YA NYARA (TROPHY DEALER’S LICENCE - TDL) KWA MWAKA 2017

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
 TAARIFA KWA UMMA

KUWASILISHA MAOMBI YA LESENI YA BIASHARA YA NYARA (TROPHY DEALER’S LICENCE - TDL) KWA MWAKA 2017

Wizara ya Maliasili na Utalii inawajulisha wananchi wanaotaka kufanya Biashara ya Nyara kuwasilisha maombi yao kwa Mkurugenzi kwa kujaza Fomu za Maombi ya Leseni zinazopatikana na kupitishwa na Maafisa Wanyamapori wa Wilaya husika.  Fomu hizo pia zinapatikana kwenye Ofisi ya Matumizi Endelevu ya Wanyamapori zilizopo Morogoro (Jengo la TAFORI), Dar Es Salaam, na Arusha.

Hakuna Leseni za Daraja lolote au Mnyama yeyote, kwa Mwaka 2017 zitakazotolewa kwa madhumuni ya ukamataji na usafirishaji wa Wanyamapori hai nje ya nchi.  Aidha, Tangazo hili linafuta Tangazo lililotolewa tarehe 06/12/2016 katika vyombo mbalimbali vya habari.

Fomu za mwombaji zinatakiwa kujazwa na kuwasilishwa kwa Maafisa Wanyamapori wa Wilaya ndani ya siku 45 tangu tarehe ya Tangazo hili.

Meombi ya Leseni kwa Mwaka 2017 ni kwa Daraja zifuatazo:-

DARAJA
MAELEZO
1.
Biashara ya Meno ya Kiboko au Ngiri ambayo hayajatengenezwa, nzima au kipande
2.
Biashara ya ngozi za wanyamapori isipokuwa ngozi za Pimbi na Mbega
3.
Biashara ya ngozi ya Pimbi
5.
Biashara ya kukata na kutengeneza ngozi za Chui, Simba, Mondo au ngozi nyingine za wanyamapori jamii ya Paka.
6.
Biashara ya kukata na kutengeneza ngozi za wanyamapori isipokuwa za Pimbi na Mbega pamoja na kutengeneza vitu kutokana na nyara hizo.
7.
Biashara ya nyara zilizotengenezwa
8.
Biashara ya kuhifadhi nyara mbalimbali ili zisiharibike mapema
10.
Biashara ya mikia ya wanyamapori isipokuwa ya Tembo, Faru, na Mbega na vitu vinavyotokana na nyara hizo.
11.
Wakala wa kusafirisha nyara kwa ujumla isipokuwa Wanyama hai.
17.
Bustani ya Wanyamapori
18.
Mashamba ya kufuga wanayamapori (isipokuwa kwa nia ya kusafirisha Wanyamapori hai nje ya nchi).
19.
Vituo vya Karantini (isipokuwa kwa nia ya kusafirisha wanyama hai nje ya nchi).
20.
Ranchi za wanyamapori (isipokuwa kwa ajili ya kusafirisha wanyamapori hai nje ya nchi)
21.
Aina yoyote ya biashara ya nyara ambayo haikutajwa kwenye daraja la 1-20 isipokuwa kusafirisha wadudu na viumbe wengine hai nje ya nchi.


Mwombaji anatakiwa kuwasilisha fomu ya maombi ya leseni pamoja na uthibitisho wa yafuatayo:-

1.                  Endapo mwombaji ni mtu binafsi anatakiwa awasilishe hati ya usajili  wa jina la biashara (Certificate of Registration of Business name) au iwapo mwombaji ni Kampuni awasilishe Katiba ya Kampuni (Memorandum and Articles of Association) na Hati ya utambulisho wa mlipa kodi (Tax payer Identification Number).

2.                  Uthibitisho wa kuwa na Wakamataji wenye elimu ya Uhifadhi wa Wanyamapori kutoka kwenye Chuo kinachotambulika na Serikali.

3.                  Uthibitisho kwamba biashara ina leseni kutoka kwenye Mamlaka husika.

4.                  Mpango wa biashara (business plan) unaoruhusu biashara inayotarajiwa kufanywa na uthibitisho wa mtoaji.

5.                  Uthibitisho wa malipo ya Ada ya maombi ya leseni ya (TZS. 5,000/=) ambayo haitarudishwa (Non-Refundable).  Fedha hizo zilipwe kupitia Benki ya NBC Samora Avenue, Akaunti Na. 012103011903 ya “SELOUS GAME RESERVE au CRDB Tanzania Wildlife Management Authority Akaunti Na. 0150319566100 TAWA”

6.                  Mwombaji asiwe na rekodi ya kupatikana na hatia ya kuvunja Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009 na

7.                  Kwa mwombaji wa shughuli za ufugaji wa Wanyamapori, Ada ya Maombi ya Leseni ya Ufugaji itategemea aina ya ufugaji kama ifuatavyo:-

i)                    Bustani ya Wanyamapori; Ada ya Maombi ni Dola za Kimarekani 150 kwa mzawa, mzawa kwa kushirikiana na Mgeni Dola za Kimarekani 250.

ii)                  Mashamba ya Ufugaji Wanyamapori; Ada ya Maombi ni Dola za Kimarekani 200 kwa mzawa na kwa mzawa akishirikiana na mgani ni Dola za Kimarekani 500.

iii)                Ranchi za Wanyamapori Ada ya Maombi ni Dola za Kimarekani 500 kwa mzawa na kwa kushirikiana na mgeni ni Dola za Kimarekani 1000.
  

KATIBU MKUU
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

23 JANUARI, 2017

No comments:

Post a Comment