slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Wednesday, May 31, 2017

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, PROF. JUMANNE MAGHEMBE AFANYA MAZUNGUMZO LEO NA BALOZI WA CHINA NCHINI, DKT. LU YOUGING, MJINI DODOMA

Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akizungumza na balozi wa China nchini, Dkt. LU Youqing ofisini kwake leo mjini Dodoma ambapo wamejadili na kukubaliana mambo mbali mbali ya kuimarisha uhusiano wa China na Tanzania katika sekta ya maliasili na utalii. Miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na kuwakaribisha wawekezaji katika sekta ya viwanda vya uchakataji wa mazao ya misitu na ujenzi wa hoteli katika fukwe za Tanzania na Hifadhi za Taifa.
 Balozi wa China nchini, Dkt. LU Youqing akimueleza jambo Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe alipomtembelea ofisini kwake mjini Dodoma leo. Balozi huyo amekubali ombi la Waziri Maghembe kuwaleta wadau wa mashirika ya utalii kutoka nchini China kwa ajili ya kutembelea vivutio vya utalii vya Tanzania na kuvitangaza nchi kwao.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akimfafanulia jambo balozi wa China nchini, Dkt. LU Youqing alipomtembelea ofisi kwake leo mjini Dodoma. Waziri Maghembe kupitia balozi huyo ameipongeza Serikali ya China na Wananchi wake kwa uamuzi wake wa hivi karibuni wa kufungia biashara haramu ya meno ya tembo nchini humo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe akiagana na Balozi wa China nchini, Dkt. LU Youqing baada ya mazungumzo marefu ofisini kwake leo mjini Dodoma.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kulia), Balozi wa China nchini, Dkt. LU Youqing (kushoto), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili, Dkt. Aloyce Nzuki (kulia) na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Justa Nyange wakijadili jambo muda mfupi baada ya mazungumzo hayo. (PICHA ZOTE NA HAMZA TEMBA - WMU)

No comments:

Post a Comment