slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Thursday, October 26, 2017

DK. KIGWANGALLA ATUA LOLIONDO, AFANYA KIKAO NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA YA NGORONGORO

NA MWANDISHI WETU
.................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla amewasili Makao makuu ya Wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha na kufanya mkutano maalum na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo ambapo pia atatembelea maeneo yenye migogoro. 

Waziri, Dkt.Kigwangalla amewasili katika uwanja mdogo wa Wasso uliopo tarafa ya Loliondo na kisha kukutana na viongozi hao wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mh. Rashid Mfaume Taka. 

Dk Kigwangalla baada ya kumaliza kikao hicho maalum na wakuu hao, anatarajia kutembelea maeneo yenye migogoro ili kupata picha halisi na kubaini kiini cha mgogoro wa eneo hilo la Pori Tengefu Loliondo.

Aidha, anatarajia kufanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Tarafa ya Loliondo kwa ajili ya kusikiliza kero zao mbalimbali. 

Waziri, Dkt.Kigwangalla yupo Mkoani Arusha kwa ajili ya ziara ya kikazi ambapo awali alianza kutembelea Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro ambapo pia aliweza kukutana na jamii ya wafugaji wanaoishi kwenye hifadhi ya Ngorongoro.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akishuka kwenye ndege wakati akiwasili Loliondo kufuatilia kwa kina mgogoro unaoendelea Loliondo.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiongozana na na viongozi wa Wilaya ya Ngorongoro

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na viongozi wa Wilaya ya Ngorongoro kwenye uwanja wa ndege wakati akiwasili Loliondo kufuatilia kwa kina mgogoro unaoendelea wilayani humo.

Mkuu wa Wilaya hiyo Mh. Rashid Mfaume Taka akimwakilisha Waziri Dk.Kigwangalla katika mkutano huo wa Kamati ya Ulinzi na Usalama

No comments:

Post a Comment