slider gif

slider gif

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

kilimanjaro CAN ONLY B CLIMBED FROM TZ

Tuesday, January 30, 2018

SERIKALI YAINGIZA MIL 30.9 KUPITIA MAUZO YA MENO YA VIBOKO

No automatic alt text available.
Serikali imepata mapato ya Shilingi Milioni 30.9 kupitia mauzo meno ya viboko vipande 12,467 vyenye uzito wa kilo 3,580.29 ambayo yameuzwa kupitia mnada wa hadhara uliofanyika katika ofisi ndogo za Wizara ya Maliasili na Utalii katika Jengo la Mpingo Jijini Dar es Salaam.

Mnada huo ulioratibiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania chini ya usimamizi wa Wizara ya Fedha na Mipango ulijumuisha makampuni 19 yenye Leseni za Nyara Daraja la Kwanza ambapo kampuni ya On Tours Tanzania Limited iliibuka mshindi kwa kutoa dau la Shilingi milioni 30.9.

Mwakilishi wa kampuni hiyo, Grey Kilas alilipa asilimia 25 papo hapo kwa mujibu wa masharti ya mnada huo na kuahidi kulipa asilimia 75 ya kiasi kilichobakia ndani ya siku 14 zijazo.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA, Mabula Misungwi alisema biashara hiyo haiwezi kuchochea ujangili kwa vile meno hayo yanauzwa kwa wafanyabiashara maalum wenye leseni za nyara daraja la kwanza.

Mabula alisema meno hayo yalianza kukusanywa tangu mwaka 2004 ambapo kipindi cha huko nyuma yalikuwa yakiuzwa kwa makampuni yenye leseni za nyara kwa utarartibu tofauti na ulioanza kutumika mwaka huu ambao ni kupitia mnada wa hadhara.

Naye Mwakilishi wa Kampuni iliyonunua meno hayo, Grey Kilas aliwashukuru wasimamizi wa mnada huo kwa kuuendesha kwa uwazi wa hali ya juu ambapo ulitoa fursa kwa kila mfanyanyabiashara hatimaye ukamuwezesha kuibuka mshindi.

Akizungumzia kuhusu soko, Kilas alisema meno hayo huuzwa nchini Japan, Marekani na Hongkong ambapo hutumika kutengeneza mapambo, sanamu pamoja na vishikizo vya nguo.

Kwa mara mwisho biashara hiyo ya kuuza meno ya viboko ilifanyika mwaka 2004.
Image may contain: food


No comments:

Post a Comment